Cmp
Sioni tatizo kwenye hili, kwasababu hii ni kama bonus kwa wafanyakazi ambao wapo huko. Kua kama nafasi zimetoka alfu wao wana ndugu zao au rafiki basi wanaweza waunganisha.
Kila mfanya kazi, lazima awe anapewa upendeleo kwenye eneo lake la kazi. Mfano, mfanyakazi wa tanesco atakatwa kkwa kiwango kidogo, mfanyakazi wa Crdb atapewa mda mrefu wa kulipa kodi akichukua mkopo nk...
Mfanyakazi wa kampuni / shirika / taasisi flani ni sawa na mtoto wa hiyo taasisi, kwaiyo lazima awe na nafasi za upendeleo tofauti na wale ambao sio wafanyakazi wa iyo taasisi. Ni sawa tu na ambavyo mzazi anavyoweza kumjali / hudumia mwanae mwenyewe na yule wa jirani. Lazima tofauti iwepo.
Kama mtu unafanya kazi kwenye taasisi flani na unapanda nafasi za upendeleo, kwanini ndugu zako, marafiki na majirani wasinufaike?