Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
1984- Masange JKT (Tabora) (Operesheni Nguvu Kazi) mlipuko wa baruti katika kutishia simba wala watu. Walijeruhiwa Luteni Usu Msange, Mwangupile (alikatwa mkono) na wengine kunusurika miongoni mwao mwandishi mashuhuri Chemi Che Mponda.
Januari 5, 1999 Bomu lalipuka pembeni ya Ofisi ya CCM, Kata ya Bulele, Muleba huko Kagera, jengo laharibiwa upande.
Disemba 25, 2005 Bomu laua 1, na watano wajeruhiwa kijiji cha Mlela Kigoma
Disemba 27, 2006 Bomu la mkono lalipuka Kurasini kwenye eneo la kukusanyia vyuma chakavu, mmoja afariki, 5 wajeruhiwa. Baada ya uchunguzi zaidi Mengine 43 yaligundilika kiwanda cha Quaim Steel Mills Changombe, Dar na lingine moja lililookotwa ndani ya kiwanda cha Dabaga.
Mshangao mkubwa ni pale bomu mojawapo lilipokutwa linatumika kama mfuniko wa rejeta ya kijiko cha kupakia/kupakua mizigo ndani ya ghala la Hahrour Enterprises.
Oktoba 15, 2007 Bomu laua 4 wa familia moja huko Bukoba baada ya mtoto kuokota bomu hilo na kuliweka motoni akidhania kiazi. Mmoja ajeruhiwa.
Disemba 10, 2007 Watoto 3 wauawa na bomu Makutopora Dodoma, 6 wajeruhiwa
Mei 20, 2008 Kundi la Majambazi wapatao 15 wavamia basi walilipua kwa mabomu kwenye msitu wa Kimisi, Karagwe huko Kagera. 2 wauawa papo hapo. Mmoja ni askari mwenye silaha aliyekuwa akilisindikiza basi hilo. Aliuawa kishujaa lakini jina lake halikuimbwa kwa sifa kama alivyofanyiwa yule aliyeokoa mamilioni pale Ubungo!
Juni 9, 2008 - Helikopta ya Jeshi yaanguka na kulipuka, watu sita wafariki
Novemba 12, 2008, Mama na Mtoto wauawa na Bomu Kilosa wakiwa shambani.
Disemba 21, 2008 Watoto 4 wa jamii ya Kimasai walipuliwa na Bomu kijiji cha Embokoi, Siha huko Kilimanjaro karibu na bonde la Kilelepori ambapo Polisi hufanyia mazoezi ya silaha za moto
Januari 3, 2009 Bomu lalipuka Kambi ya Raha, mji wa Bomangombe huko Hai Kilimanjaro, 2 wajeruhiwa.
Feb 13, 2009 Washtakiwa 2 walipukiwa na Bomu Mahakamani Kasulu, Kigoma na mmoja kujeruhiwa katika jitihada za kutaka kutoroka.
Aprili 29, 2009- Mlipuko mkubwa wa mabomu ya kawaida na makombora watokea ghala ya silaha ya JWTZ kikosi cha 511 Mbagala ambapo watu 15 wauawa na zaidi ya 600 wajeruhiwa.
Januari 5, 1999 Bomu lalipuka pembeni ya Ofisi ya CCM, Kata ya Bulele, Muleba huko Kagera, jengo laharibiwa upande.
Disemba 25, 2005 Bomu laua 1, na watano wajeruhiwa kijiji cha Mlela Kigoma
Disemba 27, 2006 Bomu la mkono lalipuka Kurasini kwenye eneo la kukusanyia vyuma chakavu, mmoja afariki, 5 wajeruhiwa. Baada ya uchunguzi zaidi Mengine 43 yaligundilika kiwanda cha Quaim Steel Mills Changombe, Dar na lingine moja lililookotwa ndani ya kiwanda cha Dabaga.
Mshangao mkubwa ni pale bomu mojawapo lilipokutwa linatumika kama mfuniko wa rejeta ya kijiko cha kupakia/kupakua mizigo ndani ya ghala la Hahrour Enterprises.
Oktoba 15, 2007 Bomu laua 4 wa familia moja huko Bukoba baada ya mtoto kuokota bomu hilo na kuliweka motoni akidhania kiazi. Mmoja ajeruhiwa.
Disemba 10, 2007 Watoto 3 wauawa na bomu Makutopora Dodoma, 6 wajeruhiwa
Mei 20, 2008 Kundi la Majambazi wapatao 15 wavamia basi walilipua kwa mabomu kwenye msitu wa Kimisi, Karagwe huko Kagera. 2 wauawa papo hapo. Mmoja ni askari mwenye silaha aliyekuwa akilisindikiza basi hilo. Aliuawa kishujaa lakini jina lake halikuimbwa kwa sifa kama alivyofanyiwa yule aliyeokoa mamilioni pale Ubungo!
Juni 9, 2008 - Helikopta ya Jeshi yaanguka na kulipuka, watu sita wafariki
Novemba 12, 2008, Mama na Mtoto wauawa na Bomu Kilosa wakiwa shambani.
Disemba 21, 2008 Watoto 4 wa jamii ya Kimasai walipuliwa na Bomu kijiji cha Embokoi, Siha huko Kilimanjaro karibu na bonde la Kilelepori ambapo Polisi hufanyia mazoezi ya silaha za moto
Januari 3, 2009 Bomu lalipuka Kambi ya Raha, mji wa Bomangombe huko Hai Kilimanjaro, 2 wajeruhiwa.
Feb 13, 2009 Washtakiwa 2 walipukiwa na Bomu Mahakamani Kasulu, Kigoma na mmoja kujeruhiwa katika jitihada za kutaka kutoroka.
Aprili 29, 2009- Mlipuko mkubwa wa mabomu ya kawaida na makombora watokea ghala ya silaha ya JWTZ kikosi cha 511 Mbagala ambapo watu 15 wauawa na zaidi ya 600 wajeruhiwa.