Kwanza nianze kuhakikisha hii habari kuwa ni kweli hata East Africa Radio wameirusha mda si mrefu. Alex Massawe anakabiliwa na tuhuma za mauwaji ya mfanyabiashara ambayo pia Papaa Msofe anahusika. Habari zilizopo ni kuwa mfanyabiashara aliyeuliwa alikopa fedha (inasemekana ni kama mil 200, ila sina uhakika na hii amount) kutoka kwa ALex massawe na akaweka bond nyumba yake iliyopo maeneo ya magomeni. Akamkabidhi Alex masawe hati ya nyumba ikiwa ni sehemu ya mkataba wa mkopo huo. Mfanyabiashara alipotaka kurizudisha zile fedha Alex massawe akawa anapiga chenga hataki kuzipokea kwa madhumuni ya kuupitisha muda riba iwe kubwa jamaa ashindwe kulipa halafu ajihalalishie kuichukua nyumba. Marehemu akawa mjanja akaenda kuiwakilisha zile fedha kwa mwanasheria aliyewafungia mkataba wa mkopo. Baada ya Alex massawe kuona anazidiwa ujanja ndo akaanza kutumia mabavu na kumuuzia ile nyumba Papaa msofe ilihali akijua hana umiliki halali. Baada ya mfanyabiashara kuuawawa, papaa msofe ndo akawa anaighasi familia ya marehemu kuwa hiyo nyumba kashauziwa hivyo watoke na atakuja kuwatoa kwa nguvu. Mke wa marehemu akaenda moja kwa moja kwa Said Mwema na kuilezea habari nzima nzima tangu makubaliano ya mkopo na kuuliwa kwa mumewe na vitisho anavyopata toka kwa wauwaji wa mumewe. Kifupi hili ndo saga lenyewe na kesi ya Papa msofe ilikuwa haiwezi kwenda popote hadi alex massawe atapopatikana kwa sababu ni mtuhumiwa mkuu pia kwenye kesi hii.