Alex Massawe kakamatwa!


Amekamatwa baada ya kuchelewa kuwasilisha fungu la kumi kwa watawala ama imekuwaje. Mwaka 2006 wakati Kikwete anajenga uzoefu wa kuishi jumba jeupe umma wa Watanzania uliambiwa kuwa mtu huyo huyo (AM)amewekwa chini ya uangalizi wa polisi-ccm; sijui huo uangalizi uliisha vipi na lini hadi leo awe mtu wa kutafutwa na polisi wa kimataifa.

EE MWENYEZI MUNGU LINUSURU TAIFA LAKO LINALOELEKEA KUANGAMIA NA KUYEYUKA HARAKA KAMA BONGE LA BARAFU MIKONONI MWA MTAWALA WAKE
 
Hazidishiwi mwenye kudhulumu ila hasara.
 
Hivi anavyosafiria na passport/hati za kusafiria za bandia, alisahau kuwa huwa wanacheki na alama za vidole au?

Kama kakamatiwa Dubai sawa,pale kuna security ambayo sijawahi kuona popote duniani, yaani mtu unapimwa macho utafikri uko hospitali.
 
AM Rais wa watu wa kule kwetu...the real role model....anajiita mfanyabiashara ingawa si kweli anafanya biashara...anakwiba!
 
Mfanyabiashara maarufu nchini, Alex Massawe ambaye alikuwa anatafutwa na Polisi wa Tanzania kwa muda mrefu, amekatwa Dubai, Falme za Kiarabu (UAE). Mkuu wa la Shirika la Polisi la Kimataifa (Interpol), Tawi la Tanzania, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Gustav Babile aliliambia gazeti hili jana kwamba Massawe alikamatwa kati ya Juni 20 na 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dubai akitokea Afrika Kusini.
 
Mshahara wa dhambi ni mauti,alex massawe alifikiri pesa yake itashinda hata mkono wa Mungu
 
Facilitator unataka more source!
Kuhusu passport fake aliyokamatwa nayo Dubai?
Akitaka ahonge $•••,•••,•••lakini jamaa wakamtolea nje
I was in Dubai when this happened, Na Kwa vile ninamfahamu Alex Massawe since 1995, Na dhuluma zake zikiwepo kununua MAGARI ya wizi etc I have full dossier
Hint! Mnamkumbuka John Supper? Aliyekuwa hapa Dar miaka ya nyuma Kama jambazi?
Subirini kitabu changu title:
Mtandao Na umaarufu Wa Mapedejee Wa Tanzania
Author •••••••••
Publisher•••••••
Year 2013
 



HABARI YA PILI YA JINSI ALEX MASSAWE ALIVYO NASWA NA MYEGO WA POLISI DUBAI!!!


Dar es Salaam. Mfanyabiashara maarufu nchini, Alex Massawe ambaye alikuwa anatafutwa na Polisi wa Tanzania kwa muda mrefu, amekatwa Dubai, Falme za Kiarabu (UAE).
Mkuu wa la Shirika la Polisi la Kimataifa (Interpol), Tawi la Tanzania, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Gustav Babile aliliambia gazeti hili jana kwamba Massawe alikamatwa kati ya Juni 20 na 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dubai akitokea Afrika Kusini.
Babile alisema hivi sasa walikuwa wanaandaa taratibu za kumrudisha nchini ambako amekuwa akisakwa kwa muda mrefu.
“Ombi la kuleta mhalifu nchini kutoka nje ya nchi (extradition request), lina hatua ndefu. Unajua kuna mlolongo wa taratibu za kutekeleza ili Massawe aletwe. Kwanza lazima Polisi wa Tanzania watoe tangazo kwa Interpol kuhusu kumsaka mtu huyo ili aletwe,” alisema Babile.
Alisema Massawe alikamatwa wakati akifanya taratibu za ukaguzi baada ya kuwasili UAE.
“Maofisa wa Usalama wa uwanja wa ndege walimuuliza kuwa wewe ndiye Alex Massawe? Alikana lakini alielezwa kuwa alama za vidole vinaonyesha anaitwa hivyo,” kilidokeza chanzo cha habari hizi kwa simu kutoka Dubai. Hata hivyo, Babile alisema hakuwa na taarifa za Massawe kukutwa na pasi bandia za kusafiria.
Massawe ambaye anamiliki majumba na biashara ya utalii katika Miji ya Arusha, Dar es Salaam na Moshi, inadaiwa kwamba alikutwa na pasi tatu bandia za kusafiria zilizokuwa na majina tofauti wakati alama zake za vidole zilionyesha anaitwa Alex Massawe.
“Maofisa wa Usalama wa uwanja wa ndege walimuuliza kuwa wewe ndiye Alex Massawe? Alikana lakini alielezwa kuwa alama za vidole vinaonyesha anaitwa hivyo,” kilidokeza chanzo cha habari hizi kwa simu kutoka Dubai. Hata hivyo, Babile alisema hakuwa na taarifa za Massawe kukutwa na pasi bandia za kusafiria.
Uvumi wa Aprili
Mapema Aprili 27, mwaka huu kulikuwa na habari kwamba Massawe amekamatwa katika mji mmojawapo ulioko katika Pwani ya Afrika Kusini.
Habari hizo za kukamatwa kwa Massawe, ambaye pia hufadhili masuala ya kisiasa na michezo, zilisambaa kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii ya Facebook, Twitter na Jamii Forum. Kulikuwa kuna mkanganyiko wa taarifa huku wengine wakidai alinaswa akiwa ndani ya boti huko Afrika Kusini, wengine wakidai alikamatwa wakati akijaribu kuingia Msumbiji akitokea Malawi.
Akizungumzia hilo Babile alisema huo ulikuwa ni uzushi na baada ya kuzisikia taarifa hizo walifuatilia katika maeneo aliyohusishwa kukamatwa na kubaini kwamba hapakuwa na ukweli wowote
Kwa nini Massawe anatafutwa
Aprili 4 mwaka huu, mfanyabiashara huyo alitajwa mahakamani katika kesi ya mauaji ya mfanyabiashara Onesphory Kituly ambaye aliuawa katika mazingira ya kutatanisha Novemba 6, 2011 akiwa nyumbani kwake Magomeni, Dar es Salaam.

Katika kesi hiyo ambayo mshtakiwa wa kwanza ni mfanyabiashara maarufu, Abubakar Marijani ‘Papaa Msofe’ na mshtakiwa mwingine, Makongoro Joseph Nyerere alitoa malalamiko mbele ya Hakimu Mkazi, Agnes Mchome baada ya Wakili wa Serikali, Mwanaisha Kombo kudai upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kuomba tarehe mpya ya kuitaja. Mshtakiwa huyo, aliomba jalada la kesi yao lipelekwe mahakamani hapo kwa ajili ya kulifanyia kazi na kutuhumu kuwa ndugu wa marehemu Kituly hawataki maendeleo ya kesi yao hadi Massawe akamatwe.
 
Huyu jamaa kaishapoteza roho za watu wengi sana.
 

Ebana bora uwa expose maana wanatusumbua sana hawa kila tukiwasha radio wanatajwa wao kumbe waizi
 


Wanaua watu wengi sana hawa. Huyu Massawe ni jambazi na anajulikana tena kuna tetesi alikuwa anakula na baadhi ya vigogo wa polisi (sina uhakika, ni tetesi) na ndiyo maana alikuwa anafanya maasi na hakamatwi. Nchi yetu kwa kweli jeshi la polisi linatumaliza kwani wanashirikiana na majambazi kwa maovu huku Pinda akiwapa support ya kutunyanyasa.
 

Kama huu ndo ukweli wenyewe bora haya majambazi yanyongwe. Upapaa mwingi kumbe majambazi, shame upon them.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…