Joannah
JF-Expert Member
- May 8, 2020
- 18,447
- 42,559
Comment yako Ina make sense.City...
City...
Okello anabebeshwa mzigo si wake.
ASP haikuwa na uwezo wa kupindua serikali.
Mipango yote ilifanyika Dar es Salaam ikisimamiwa na Oscar Kambona na Abdullah Kassim Hanga.
Waliweka kambi Kipumbwi ambako waliwaweka Wamakonde kutoka shamba la Mkonge la Sakura kwa ajili ya kuwavusha kuingia Zanzibar kuIpigIa kura ASP na kushiriki katika mapinduzi.
Kambi hii ilikuwa chini ya Ali Mwinyi Tambwe akiwa District Commissioner wa Tanga na Regional Commissioner Jumanne Abdallah.
Waliopewa kazi ya kuchagua vijana wa kuletwa kambini Kipumbwi walikuwa Victor Mkello kiongozi wa chama cha wakata mkonge na Mohamed Omar Mkwawa kijana wa Kidigo kutoka Tanga aliyepatakuwa mwanachama hodari wa ASP.
Ali Mwinyi Tambwe wakati wa ukoloni aliwatumikia Waingereza kama "mole" wao ndani ya TAA kisha TANU.
Mkwawa yeye ndiye aliyekuwa akiwavusha hawa Wamakonde kuwaingiza Zanzibar usiku kwa majahazi wote wamevaa kama wavuvi wa Kidigo.
Kipumbwi yote ilikuwa imezuiwa kwa watu kuingia ovyo.
Hawa Wamakonde ndiyo walioua Waarabu wengi wakulima wa kawaida tu waliokuwa mashambani Zanzibar.
Mpango huu ulifanyika kwa siri kubwa sana.
Mzanzibari aliyepata kufika Kipumbwi inasemekana ni Jimmy Ringo ambae aliuliwa baada ya mapinduzi kama walivyouliwa wana ASP wengine.
John Okello hakuwa katika mipango hii.
Kilichompa umaarufu ni kule yeye kupewa radio kutangaza kuwa serikali imepinduliwa na Karume arejee Zanzibar kukalia kiti chake.