Being_neutral
JF-Expert Member
- Jan 9, 2024
- 379
- 720
Mzee Mohamed andika tujifunze.Mgeni,
ASP na Umma Party walikuwako wababe si Okello.
Okello alivuna kwenye "Mob Psychology."
Alikuwa mfano wa Musiba aliyekuwa anazungumza kwenye mitandao ya kijamii.
Ushamsikia tena Musiba?
Okello alipokutana na Hashil Seif (huyu ni comrade kasoma Cuba) ndani ya ndege Okello hakuweza kufanya lolote alisalimu amri.
Hakuweza kumkabili Hashil.
Wako wababe kutoka ASP ukihadithiwa unyama wao mwili utakusisimka.
Watu wenye uwezo wa kumzika mtu yu hai.
Nilikuwa nataka kuandika kuhusu kubakwa kwa binti mdogo wa Kihindi wakati mama yake anabakwa....
Nashindwa kuandika maneno ya huyu mama kuomba salama ya mwanae...
Aliyenihadithia ni kati ya hao washenzi...
Wengi mnaandika msiyoyajua.