engmtolera
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 5,149
- 1,441
Wakubwa kwa hili la Vodacom kwa kweli halikuwa la busara. Lakini ni aibu kwa Serikali kuifanya vodacom kuwa Bangusilo (Mbuzi wa kafara) kwa uzembe wake yenyewe!!! Yenyewe ndiyo ilikua katika nafasi ya kuzuia janga hilo lisitokee!!! Leo hii PM anasema Serikali itajifunza kutoka katika janga hilo... huo si upuuzi jamani??!!! Kama hawakujifunza kwa lile la MV Bukoba.... mpaka waje kujifunza si tutakua tumekwisha wote??!!
ndugu yangu si unajuwa tena kila siku sisi tunajifunza tu,likitokea lingine tena tutasema bado tunajifunza,sijui ni mpaka lini tutakuwa tayari kupambana na majanga
ama kwa kuwa ni serikali ya umoja wa kitaifa kwa hiyo bado wanajifunza tu kwani wao hawakuwepo serikalini wakati la bukoba latokea