Ajali ya Meli: SMZ yakataa misaada ya VODACOM

Ajali ya Meli: SMZ yakataa misaada ya VODACOM

Inasikitisha sana katika hili suala jinsi ambavyo VTL walivyochemsha katika suala hili. Watendaji wao hasa wa masoko wamesaahu suala la 'corporate social responsibility' na hasa katika janga hili la kitaifa. Naona picha za mama masoko akijirusha kuelekea MC zimeondolewa kule 'kata kona'
 
Inasikitisha sana katika hili suala jinsi ambavyo VTL walivyochemsha katika suala hili. Watendaji wao hasa wa masoko wamesaahu suala la 'corporate social responsibility' na hasa katika janga hili la kitaifa. Naona picha za mama masoko akijirusha kuelekea MC zimeondolewa kule 'kata kona'

Wakati VODACOM wakionja shubiri ya mchezo huu mchafu. Ofisi ya PM nao wajipange kwa majibu na Maamuzi Mazito. Chimbuko la tatizo hili ni usimamizi mbovu wa sheria na mipango isiyotekelezeka.
 
Pale Billicanas club watu waliendelea kujirusha kama kawaida.
Kama ni kususia basi wengi waingie kwenye mtego huu.
Nadhani haya ni mambo ya masikini jeuri tu.
Kama hii habari ni kweli, inashangaza waziri au wananchi kutosema chochote kuhusu waliofanya uzembe na kujaza meli na wanakataa misaada ambayo ingeboresha maisha ya wajeruhi.
This is an attack to the wrong enemy.
 
Nashauri SMZ waende mbali zaidi ya hapo kwa kuipiga BAN Vtl isioperate Zanzibar .
 
Wakati VODACOM wakionja shubiri ya mchezo huu mchafu. Ofisi ya PM nao wajipange kwa majibu na Maamuzi Mazito. Chimbuko la tatizo hili ni usimamizi mbovu wa sheria na mipango isiyotekelezeka.

Kwanini Vodacom imebebeshwa lawama nyingi kwa kutositisha onesho walilodhamini badala ya kuwabebesha lawama waliosababisha ajali ambao ni serikali ya ccm? Hapa pana mashaka.

Pili, katika kipindi hiki ambacho ccm wanavuana magamba, na baadhi ya wahusika wanaokwaruzana na wenzao ndani ya ccm wanahisa VODACOM, siwezi kuzuia hisia kuwa hapa pana mchezo mchafu. Nina mashaka na Move hii dhidi ya vodacom.

Sijasema vodacom hawajakosea - walikosea, japokuwa sijajua, wao kama wafadhili tu, uwezo wao wa kusitisha ghafla kitu ambacho walishaingia mkataba na wahusika wengine, ambao hata hivyo hawalaumiwi kabisa ktk sakata hili, kitu ambacho kinashangaza sana.

Mbona wanaosema tuwasusie vodacom, hawasemi tususie kuangalia TBC ambao walikuwa wanatumia kodi zetu kuonesha wanaokata viuno badala ya kututaarifa maafa ya kitaifa. Mashaka mengine haya.
Ninawaza tu, nina hitaji kueleweshwa pia.
 
Mimi nitasoma tu kwanza nione nini hasa kinatokea .Viodacom mh
 
bongo bana!!! sasa wamkomoa nani? VODACOM au WAHANGA??? walioukataa huo msaada ni wale ambao hawajapatwa na dhoruba

Laiti kama vodacom wangepeleka msaada moja kwa moja kwa wahanga sidhani kama wangeukataa.

kuna watu wameanza kuleta SIASA HAPO!!!

chukuwa msaada wape waathirika wenyewe ndo waukatae sio nyie ma MIDDLE Man
 
Nashauri SMZ waende mbali zaidi ya hapo kwa kuipiga BAN Vtl isioperate Zanzibar .


Barubaru.

Vodacom ikipigwa ban Zanzibar haitaathiri mapato yao hata kidogo soko la Zanzibar ni sawa na wilaya ya Muheza Tanga.Nakushangaa sana unaacha kuwakomalia waliosababisha ajali unakimbilia Vodacom.Kwani nani kakwambia Vadacom ni suala la muungano acheni uchuro.
 

Barubaru.

Vodacom ikipigwa ban Zanzibar haitaathiri mapato yao hata kidogo soko la Zanzibar ni sawa na wilaya ya Muheza Tanga.Nakushangaa sana unaacha kuwakomalia waliosababisha ajali unakimbilia Vodacom.Kwani nani kakwambia Vadacom ni suala la muungano acheni uchuro.

hapo wanaweka mambo ya serikali tatu
 
Sioni logic ya kukataa 'ubani' wa Vodacom na kuwalaumu kiasi hicho kwa sababu;
Vodacom hawakuwa wadhamini pekee katika shindano hilo. Kulikua na wadhamini wengine kama Ngorongoro, TANAPA, Star TV, Giraffe Ocean View Hotel na wengineo. Kwa nini lawama ziende kwa Vodacom pekee? Hata kama Vodacom ndio mdhamini mkuu lakini bado sio haki kupewa lawama zote wakati yeye ni mdhamini kama wengine na sio muandaaji???

Vodacom hajachangia lolote katika kutokea kwa maafa yale, uzembe ulianzia serikalini ambako waliruhusu ile boti/meli kutoka bandarini wakati wakijua ilibeba mzigo mkubwa zaidi ya mara 2 ya uwezo wake wa kawaida. Wao hawajaomba msamaha, hawajafukuzwa walipoenda kuangalia wahanga, misaada yao imepokelewa na pia wengine wameenda kujinufaisha kisiasa kwa makosa waliyoyafanya wenyewe.

Lawama nyingine kubwa inabidi ziende serikalini pia kwa sababu walitaarifiwa mapema kabisa meli ilipokua inaanza kuzama, laiti kama wangekua na utaratibu mzuri wa kukabiliana na majanga watu wengi wangeokolewa na vifo vichache sana vingeripotiwa. Kuchelewa kwao kupeleka kikosi cha uokoaji ndio sababu kubwa ya kutokea vifo vingi kiasi kile. Ingekua imetokea maandamano ya kuwalaumu wao huko Z'bar wangeenda muda ule ule tena kwa boti ya kasi ili kwenda kuwalipua kwa mabomu ya machozi na kuwapiga risasi ila kwa sababu ilikua haiwahusu hawakuona umuhimu, kwa kosa hilo ilibidi walaumiwe vikali na kuwajibishwa. Kwa maana hiyo, sioni sababu ya kulaumiwa kwa Vodacom ili hali wasababishaji na waliofanya uzembe wa wazi hawajalaumiwa.

Taarifa zaidi zilisambaa mida ya mchana, ingawa mpaka mida ya jioni wengi walikua hawajajua kilichotokea. Hakukuwa na uwezekano wa kutangaza kuhairishwa kwa tukio lile mida ya jioni wakati watu wengi kutoka sehemu mbalimbali nchini walikua wamefika kwa ajili ya tukio lile. lakini pia hata maombolezo yalikua bado hayajatangazwa siku ile, hata wewe msomaji hapa nina uhakika 'ulispend' wik end yako kwa furaha as if hakuna kilichotokea.

Hakuna haja ya kuwalaumu Vodacom kwa tukio lile ambalo lilizingatia na kutambua vifo vilivyotokea na walianza tukio lile kwa maombolezo kwa namna ambayo imeelezwa kwenye 'press release' yao. Hata hivyo, tukio lilisheheni watu wengi ambao pia kama ndio hivyo walistahili kulaumiwa kwa kuhudhuria huku wakijua kulikua na maombolezo.

Ninaomba kumalizia kwa kuwatahadharisha; inawezekana kuna watu ambao wanaitumia nafasi hii ya udhamini wa Vodacom kujinufaisha kibiashara. Wanadhamini wanafiki na wazushi ili kupunguza soko la Vodacom kibiashara, wanatumia njia nzuri ila wakati huu sio muafaka kuwafanyia hivyo Wazanzibar na WaTz kwa ujumla katika kipindi hiki cha majonzi. Mshikamano kati yetu sote bila kujali tuliitumia vipi siku ya jumamosi ndo utakaotupitisha salama ila tukianza kulaumiana kwa mtindo huo mwishoni watu wa Zanzibar watatuzuia wabara kwenda kule kisa tuliendelea na kazi siku ambazo wao walikua wanaomboleza. Hivyo, ninawashauri wale wote wanaopandikiza hizo chuki dhidi ya Vodacom waache kwa sababu madhara yake yanweza kuwa makubwa na pia serikali ipokee msaada wa Vodacom kwa maana hauwapunguzii chochote wafiwa ila utawafariji kwa namna moja uau nyingine na pia isijiingize katika malumbano au ugomvi usio na maana.

Huo ni mtizamo wangu, kila mtu anao mtizamo wake.
 
Nashauri SMZ waende mbali zaidi ya hapo kwa kuipiga BAN Vtl isioperate Zanzibar .


Barubaru,
Nini maoni yako kuhusu miss Tanzania, Tbc kuonesha wakata viuno wa kongo, CCM na Serikali yake waliozembea na waziri wa wizara husika? Wote wote wana makosa, Nani anapaswa adhabu kubwa kati ya hao na vodacom?
 

Barubaru.

Vodacom ikipigwa ban Zanzibar haitaathiri mapato yao hata kidogo soko la Zanzibar ni sawa na wilaya ya Muheza Tanga.Nakushangaa sana unaacha kuwakomalia waliosababisha ajali unakimbilia Vodacom.Kwani nani kakwambia Vadacom ni suala la muungano acheni uchuro.

Kwa mfanya biashara mahiri tunasema Ndo ndo ndo si chululu. Na Vodacom wanalijua hilo ndio maana wameweka coverage nzuri huko.

Ni Bora kabisa kuwa BAN wasioperate na kuondoa kila kilicho chao kwani wao wana kibri na dharau dhidi ya maisha ya watu. Hili litakuwa fundisho kwao na wengine wanadharau mamlaka za SMZ.
 
Barubaru,
Nini maoni yako kuhusu miss Tanzania, Tbc kuonesha wakata viuno wa kongo, CCM na Serikali yake waliozembea na waziri wa wizara husika? Wote wote wana makosa, Nani anapaswa adhabu kubwa kati ya hao na vodacom?

Suala la TBC litachukuliwa na Serikali ya JMT kwani pasi na shaka Rais wa JMT alitangaza pia maombolezo hayo na hata kukatisha safari yake ya ughaibuni. Hao watakuwa wamedharau mamlaka sio tu za SMZ bali pia hata za JMT na hivyo wanastahikhi kuchukuliwa hatua na JMT.

Vodacom kama taasisi binafsi lazima ichukuliwe hatua na JMT ambako imesajiliwa lakini vile vile SMZ lazima wawa adhibu sio tu kwa kukataa misaada yao lakini pia kuwazuilia wasifanye shughuli zao ndani ya mamlaka ya SMZ kama fundisho kwao kwa kudharau maisha ya watu na kundekeza starehe.
 
Back
Top Bottom