Suala la TBC litachukuliwa na Serikali ya JMT kwani pasi na shaka Rais wa JMT alitangaza pia maombolezo hayo na hata kukatisha safari yake ya ughaibuni. Hao watakuwa wamedharau mamlaka sio tu za SMZ bali pia hata za JMT na hivyo wanastahikhi kuchukuliwa hatua na JMT.
Vodacom kama taasisi binafsi lazima ichukuliwe hatua na JMT ambako imesajiliwa lakini vile vile SMZ lazima wawa adhibu sio tu kwa kukataa misaada yao lakini pia kuwazuilia wasifanye shughuli zao ndani ya mamlaka ya SMZ kama fundisho kwao kwa kudharau maisha ya watu na kundekeza starehe.
Suala la TBC litachukuliwa na Serikali ya JMT kwani pasi na shaka Rais wa JMT alitangaza pia maombolezo hayo na hata kukatisha safari yake ya ughaibuni. Hao watakuwa wamedharau mamlaka sio tu za SMZ bali pia hata za JMT na hivyo wanastahikhi kuchukuliwa hatua na JMT.
Vodacom kama taasisi binafsi lazima ichukuliwe hatua na JMT ambako imesajiliwa lakini vile vile SMZ lazima wawa adhibu sio tu kwa kukataa misaada yao lakini pia kuwazuilia wasifanye shughuli zao ndani ya mamlaka ya SMZ kama fundisho kwao kwa kudharau maisha ya watu na kundekeza starehe.
Inasikitisha sana katika hili suala jinsi ambavyo VTL walivyochemsha katika suala hili. Watendaji wao hasa wa masoko wamesaahu suala la 'corporate social responsibility' na hasa katika janga hili la kitaifa. Naona picha za mama masoko akijirusha kuelekea MC zimeondolewa kule 'kata kona'
KANI VODAKOM NDIO WAANDAAJI?? WAO NI WADHAMINI TU NA HAWAKUA WADHAMINI PEKEE IWEJE LAWAMA WAPEWE WAO?? na vipi kuhusu CCM KUZINDUA KAMPENI IGUNGA NAO WAMESUSIWA AU??
Kumbuka miongoni mwa waliofariki ni wateja zao?
Sioni logic ya kukataa 'ubani' wa Vodacom na kuwalaumu kiasi hicho kwa sababu;
Vodacom hawakuwa wadhamini pekee katika shindano hilo. Kulikua na wadhamini wengine kama Ngorongoro, TANAPA, Star TV, Giraffe Ocean View Hotel na wengineo. Kwa nini lawama ziende kwa Vodacom pekee? Hata kama Vodacom ndio mdhamini mkuu lakini bado sio haki kupewa lawama zote wakati yeye ni mdhamini kama wengine na sio muandaaji???
Vodacom hajachangia lolote katika kutokea kwa maafa yale, uzembe ulianzia serikalini ambako waliruhusu ile boti/meli kutoka bandarini wakati wakijua ilibeba mzigo mkubwa zaidi ya mara 2 ya uwezo wake wa kawaida. Wao hawajaomba msamaha, hawajafukuzwa walipoenda kuangalia wahanga, misaada yao imepokelewa na pia wengine wameenda kujinufaisha kisiasa kwa makosa waliyoyafanya wenyewe.
Lawama nyingine kubwa inabidi ziende serikalini pia kwa sababu walitaarifiwa mapema kabisa meli ilipokua inaanza kuzama, laiti kama wangekua na utaratibu mzuri wa kukabiliana na majanga watu wengi wangeokolewa na vifo vichache sana vingeripotiwa. Kuchelewa kwao kupeleka kikosi cha uokoaji ndio sababu kubwa ya kutokea vifo vingi kiasi kile. Ingekua imetokea maandamano ya kuwalaumu wao huko Z'bar wangeenda muda ule ule tena kwa boti ya kasi ili kwenda kuwalipua kwa mabomu ya machozi na kuwapiga risasi ila kwa sababu ilikua haiwahusu hawakuona umuhimu, kwa kosa hilo ilibidi walaumiwe vikali na kuwajibishwa. Kwa maana hiyo, sioni sababu ya kulaumiwa kwa Vodacom ili hali wasababishaji na waliofanya uzembe wa wazi hawajalaumiwa.
Taarifa zaidi zilisambaa mida ya mchana, ingawa mpaka mida ya jioni wengi walikua hawajajua kilichotokea. Hakukuwa na uwezekano wa kutangaza kuhairishwa kwa tukio lile mida ya jioni wakati watu wengi kutoka sehemu mbalimbali nchini walikua wamefika kwa ajili ya tukio lile. lakini pia hata maombolezo yalikua bado hayajatangazwa siku ile, hata wewe msomaji hapa nina uhakika 'ulispend' wik end yako kwa furaha as if hakuna kilichotokea.
Hakuna haja ya kuwalaumu Vodacom kwa tukio lile ambalo lilizingatia na kutambua vifo vilivyotokea na walianza tukio lile kwa maombolezo kwa namna ambayo imeelezwa kwenye 'press release' yao. Hata hivyo, tukio lilisheheni watu wengi ambao pia kama ndio hivyo walistahili kulaumiwa kwa kuhudhuria huku wakijua kulikua na maombolezo.
Ninaomba kumalizia kwa kuwatahadharisha; inawezekana kuna watu ambao wanaitumia nafasi hii ya udhamini wa Vodacom kujinufaisha kibiashara. Wanadhamini wanafiki na wazushi ili kupunguza soko la Vodacom kibiashara, wanatumia njia nzuri ila wakati huu sio muafaka kuwafanyia hivyo Wazanzibar na WaTz kwa ujumla katika kipindi hiki cha majonzi. Mshikamano kati yetu sote bila kujali tuliitumia vipi siku ya jumamosi ndo utakaotupitisha salama ila tukianza kulaumiana kwa mtindo huo mwishoni watu wa Zanzibar watatuzuia wabara kwenda kule kisa tuliendelea na kazi siku ambazo wao walikua wanaomboleza. Hivyo, ninawashauri wale wote wanaopandikiza hizo chuki dhidi ya Vodacom waache kwa sababu madhara yake yanweza kuwa makubwa na pia serikali ipokee msaada wa Vodacom kwa maana hauwapunguzii chochote wafiwa ila utawafariji kwa namna moja uau nyingine na pia isijiingize katika malumbano au ugomvi usio na maana.
Huo ni mtizamo wangu, kila mtu anao mtizamo wake.
kwa hiyo wangefuta mashindano hao wateja wao wangepona kifo?
V
Vodacom wameonesha corporate social responsibility kwa kutaka kutoa ubani na serikali mbumbumbu imekataa kupokea. Ulitaka wafanye nini zaidi ya hapo? Yale mashindano wao ni wadhamini tu na sio waandaaji ambao nao hawakuwa na makosa yoyote, sio kiutamaduni wala kisheria. Msitake kukuza saaaaana hii issue ati kwa sababu kuna watu wamekufa basi wengine waache mambo yao. Kama mnaona wamekosea, muwafutie leseni na sio kujaza upuuzi wa maneno maneno. (mimi sio mdau wa voda)
watanzania kama wewe ndio wanasababisha tuendelee kuwa maskini wa kifikra .umepanga maneno vyema ila sidhani kama unachangia kitu ulichokielewa .hoja ya msingi ilikuwa vodacom kama wadahamini wakuu ndio wenye sauti ya mwisho kwenye mashindano yale .kamati ingesema tuahirishe yale mashindano wasingeweza kwa sababu sorce yote ya fedha inatoka kwa vodacom kwa asilimia zaidi ya 85.wanatoa msaada kwenye maafa ili hali waliyapuuza maafa! Msaada mkubwa ungekuwa wao kubeba gharama za tamasha na kuliahirisha ,hilo lingeonyesha utu zaidi ya fedha wanazopeleka sasa.waafrika tumefika mahali tuwe tunajithamini ,kitendo kile kimeonyesha baadhi ya watanzania wachache wanatumiwa vibaya na haya makampuni ya kigeni kwa manufaa yao yao binafsi.mbaya tamasha lile limekaa kitaifa zaidi na hufanyika mara moja kwa mwaka na limekaa kiburudani zaidi,ndio maana watu wamelishupalia kwa hoja nzito.nawasilisha
suala la tbc litachukuliwa na serikali ya jmt kwani pasi na shaka rais wa jmt alitangaza pia maombolezo hayo na hata kukatisha safari yake ya ughaibuni. Hao watakuwa wamedharau mamlaka sio tu za smz bali pia hata za jmt na hivyo wanastahikhi kuchukuliwa hatua na jmt.
Vodacom kama taasisi binafsi lazima ichukuliwe hatua na jmt ambako imesajiliwa lakini vile vile smz lazima wawa adhibu sio tu kwa kukataa misaada yao lakini pia kuwazuilia wasifanye shughuli zao ndani ya mamlaka ya smz kama fundisho kwao kwa kudharau maisha ya watu na kundekeza starehe.
Mbona ujiulizi Rais Kikwete alihairisha Safari yake ya Ughaibuni kwa nini?
Je Vodacom au hata hao waandaaji wana mamlaka ya juu kuliko Rais kisheria?
Jiulize . Je maafa hayo yangetokea mafia au Ukerewe, je wangefanya shindano hilo?
Fikiria kabla kunena.
<br />Wazanzibar wenyewe hawajitambui. Hawautambui muungano na bado wanakomalia ya bara. Hawa watu zimo kweli?
Watanzania kama wewe ndio wanasababisha tuendelee kuwa maskini wa kifikra .Umepanga maneno vyema ila sidhani kama unachangia kitu ulichokielewa .Hoja ya msingi ilikuwa Vodacom kama wadahamini wakuu ndio wenye sauti ya mwisho kwenye mashindano yale .Kamati ingesema tuahirishe yale mashindano wasingeweza kwa sababu sorce yote ya Fedha inatoka kwa Vodacom kwa asilimia zaidi ya 85.Wanatoa msaada kwenye maafa ili hali waliyapuuza maafa! Msaada mkubwa ungekuwa wao kubeba gharama za tamasha na kuliahirisha ,hilo lingeonyesha utu zaidi ya fedha wanazopeleka sasa.Waafrika tumefika mahali tuwe tunajithamini ,kitendo kile kimeonyesha baadhi ya watanzania wachache wanatumiwa vibaya na haya makampuni ya kigeni kwa manufaa yao yao binafsi.Mbaya Tamasha lile limekaa kitaifa zaidi na hufanyika mara moja kwa mwaka na limekaa kiburudani zaidi,ndio maana watu wamelishupalia kwa hoja nzito.Nawasilisha