Afadhali daladala kuliko UDART

Afadhali daladala kuliko UDART

Tatizo madereva wana mgomo baridi. Apakie asipakie kwake sawa tu, kwani mshahara atalipwa tu.

Hii hali ilikuwepo pia wakati wa DMT na UDA.

Mali ya umma ndo matatizo yake.
 
Changamoto zipo kila siku, hata kwenye maisha binafsi changamoto haziishi. Leo ukitatua hili, kesho utakumbana na lingine. Hayo mabasi, wamiliki wa mradi pamoja na wafanyakazi ni lazima wapitie changamoto hizi ili kupata kitu kizuri.

Wenzetu huko ulaya, marekani na nchi zilizoendelea walipitia changamoto nyingi zaidi ya hizo katika kuleta maisha tofauti kwa watu wao.

Niliangalia documentary moja ya "when we left earth", vitu kama hivi ndio vimeleta dunia ya tofauti na iliyokuwa mwanzo. Wengine walipoteza maisha yao ili tu kubadilisha maisha ya wengine.

Natamani sana DART ingekuwa implemented throughout the city, hakuna usafiri mzuri kama huu. Watu wangeacha usafiri binafsi nyumbani asee.
mkuu kunatofauti kati ya changamoto za kielemu na taaluma, wanachokosa hawa jamaa ni taaluma, na siku wakiligundua hlo changamoto hzo unazozisema zitabadilika na kuwa suluhisho..

wangekuwa na watu wanaojua kufuatilia mambo hasa wenye taalum ya usafirishaji, m naamini tusingekuwa na malalamiko haya, ila ingekuwa ni namna ya kujiendesha....

huu mradi kama si ufisadi wa namna ya kuuendesha leo hii naul ingekuwa tsh 200, na ingetolewa kama huduma, ila kwa kuwa ni biashara, ndiyo maana tunasema waajiri watu wenye taaluma,
 
Wabongo bwana kwa kulalamika, naona hii hali itaisha tuwape muda kutatua changamoto, mbona mradi UDART mzuri tena sana ana save time, ila hizo changamoto naamini zitatatuliwa, ila si washangai wa bongo wanazani maendeleo ni SAWA NA KUCHUKUA SUKARI KTK KIJIKO, UWEKE KWENYE CHAI, UKOROGE ALAFU UNYWE kila kitu kinaugum wake tuwape mda.
 
Wabongo bwana kwa kulalamika, naona hii hali itaisha tuwape muda kutatua changamoto, mbona mradi UDART mzuri tena sana ana save time, ila hizo changamoto naamini zitatatuliwa, ila si washangai wa bongo wanazani maendeleo ni SAWA NA KUCHUKUA SUKARI KTK KIJIKO, UWEKE KWENYE CHAI, UKOROGE ALAFU UNYWE kila kitu kinaugum wake tuwape mda.
mkuu uwape muda wa nini wakati mambo yanayo lalamikiwa hayahitaji muda wa fedha. ni mambo ya kuamua tuu.
 
nyie watu wa mikoani mna tabu sana.... umetoka kwenu huko Namanyere kuja kushangaa magari ya mwendokasi sasa unajifanya unajua taratibu zoote za hayo magari.. kwa taarifa yako ni kwamba, sio magari yote yanasimama kila kituo.... mengine ni éxpress', k.m likianzia ferry, linatangaza kabisa kituo cha kwanza ni Ubungo linamalizia Kimara... so vituo vya hapo kati halitashusha wala kupakia... uwe unatuuliza kwanza wanaume wa Dar!!
 
Wabongo bwana kwa kulalamika, naona hii hali itaisha tuwape muda kutatua changamoto, mbona mradi UDART mzuri tena sana ana save time, ila hizo changamoto naamini zitatatuliwa, ila si washangai wa bongo wanazani maendeleo ni SAWA NA KUCHUKUA SUKARI KTK KIJIKO, UWEKE KWENYE CHAI, UKOROGE ALAFU UNYWE kila kitu kinaugum wake tuwape mda.
Ni vizur zikaongelewa kuliko kukaa kimya, hata management ya DART inakiri kuna changamoto na inafatilia hata operation yenyewe,why watumiaji wasikosoe?
 
Yapo yasiyotangaza wakati wa kushusha kituo husika,hili walifanyie kazi,vingine naona vinaenda sawa tu
ndo maana kuna álarm''horn'kwenye kila nguzo ndani ya gari.. kama wewe umekaribia kufika kituoni kwako unabonyeza, driver atasimama.... muda mwingine wanapitiwa na ww abiria lazima ujiongeze...
 
Je kuna yanayotangaza na yasiyotangaza vituo vya kushuka?
Nacho sema huyo mkuu kuhusu ratiba ya mabasi yasiyo simama baadhi ya vituo sio matatizo yanayo lalamikiwa.

matatizo makubwa yanayo lalamikiwa ninkama yafuatayo.

1. abiria kukaa muda mrefu bila kupata mabasi.

2. Abiria kukaa muda mrefu kwenye foleni bila kupata tiketi.

3. Madereva kuto simama kwenye vituo kwa kisisngizomio eti anawahi kuchukua wengine mfano, abiria asubuhi yupo mapipa anaelekea morocco, dereva wa kivukoni morocco anapita mapipa bila kusimama eti anawahi abaria morocco, huo ni uzuzu.

4. Mabasi kuto kuwa na tariba maalumu wala muda maalum, utakuta abiria wamekaa hata saa moja wanasubiri baadae mabasi yanakuja yameongozana.

5. Madereva kudanganya abairia eti gari haligeuzi ili kukwepa abiria ambao baada ya kuona hawapati usafiri wanaamua kupanda basi ili wakageuze nalo kwani yanauo pita yanapita yameshina sana.
 
ndo maana kuna álarm''horn'kwenye kila nguzo ndani ya gari.. kama wewe umekaribia kufika kituoni kwako unabonyeza, driver atasimama.... muda mwingine wanapitiwa na ww abiria lazima ujiongeze...
Na madereva wengine hawatoi maelekezo hayo kwa abiria.Shida inakuja haya mabasi kila siku watumiaji wapya wanapanda,ile orientation inapaswa kufanyika kwa muda mrefu.
Kuna siku nilipanda,Dereva akawa anatangaza kila kituo.Na akasisitiza kuwa abiria msibonyeze kitufe chekundu kwakua ntasimama kila kituo na alikuwa akiwatangazia abiria.Kuna basi lngine dereva hakuwa akitangaza kituo ila anasimama, hapo pia kuna changamoto,kuna dereva alikuwa hasimami kila kituo kisha baadae akasema ukitaka kushuka bonyeza kitufe chekundu kabla sijafika kituoni.
Sasa kwa sampuli hizi nadhan kuwe na formality moja tu hasa kwa yale ya kila kituo
 
Nacho sema huyo mkuu kuhusu ratiba ya mabasi yasiyo simama baadhi ya vituo sio matatizo yanayo lalamikiwa.

matatizo makubwa yanayo lalamikiwa ninkama yafuatayo.

1. abiria kukaa muda mrefu bila kupata mabasi.

2. Abiria kukaa muda mrefu kwenye foleni bila kupata tiketi.

3. Madereva kuto simama kwenye vituo kwa kisisngizomio eti anawahi kuchukua wengine mfano, abiria asubuhi yupo mapipa anaelekea morocco, dereva wa kivukoni morocco anapita mapipa bila kusimama eti anawahi abaria morocco, huo ni uzuzu.

4. Mabasi kuto kuwa na tariba maalumu wala muda maalum, utakuta abiria wamekaa hata saa moja wanasubiri baadae mabasi yanakuja yameongozana.

5. Madereva kudanganya abairia eti gari haligeuzi ili kukwepa abiria ambao baada ya kuona hawapati usafiri wanaamua kupanda basi ili wakageuze nalo kwani yanauo pita yanapita yameshina sana.
Hizi hoja ni za kweli kabisa mdau,me nimeona hizi mambo zinasababishwa na sababu zifuatazo
1.System zao DART BADO HAZIKO SAWA
2.Madereva hawana stress ya kudaiwa kipande na boss,mwisho wa siku mshahara wake upo tu,na leo wamesema wanataka laki 8
3.Matrafki wetu ni chanzo pia,kuna wakat wanayaweka sana haya mabasi kwenye junctions hasa Magomeni na Ubungo (Hili huwa nalishuhudia) sijui kwa huko kwingine
4.Hayana muda maalum haya mabasi,muda wa kufika kituo flan sababu ya uongozaj wa magar ya kawaida ufanywao na matrafki.
5.Hakuna utaratibu wa kukata tiketi za mwezi ambapo abiria hatakaa foleni kwenye kukata tiket
 
Kinachonikera rti uende na pesa kamili basi wakatisha tiketi wanakula hamsini su 350 zetu
 
BRT ndio habari ya mujini
Vidaladala kapande Mwanza
 
1. Kwenye daladala abiria ndio mfalme , hata uwe mbali utasubiriwa, hata kama basi limejaa utaambiwa kuna nafasi etc

Sasa UDART ni kinyume chake kabisa, dereva ndio mfalme, anaamua apakie au asipakie, anaweza pita na gari tupu na asipakie, anaweza hata akadanganya eti gari bovu anaenda kupaki kumbe hataki apakie njiani, usumbufu kibao utadhani abiria wanapanda bure.

tofauti nyingine ongezeni..

Kwa hiyo unafurahia vurugu za daladala? Kusimama ovyo kila sehemu bila kufuata vituo rasmi. Kwenda bila kuzingatia muda wa safari? Ama kweli wewe ni Tabutupu
 
Back
Top Bottom