K
Kweli mkuu,Kuna siku tuko na Boss wangu, yeye alikuwa mtu wa kujisikia sana na kujiona MSOMI sana na kudharau watu!Siku Moja tumeeenda Singida njia ya Kwamtoro,Ambaye kapita njia hiyo ,anapajua ni mapori kwa kweli.
Tukiwa njiani gari ikapata pancha na rimu likawa limepinda na spare tyre halina upepo na hakuna magari yanayopita mara kwa mara!Kipindi hicho Hamna Hawa bodaboda,hivyo pikipiki ni za shida pia.Mimi nimekulia vijijini na nayaelewa maisha ya vijijini.Nikatafuta wanakijiji Rika langu,nikawaeleza shida yetu ya gari nk.Hali ikabadilika msaada Hakuna Basi linalopita hapo,ni Moja tuu na linaenda asubuhi na kurudi jioni.Bosi mazingira kwake haya ni mapya!Yule kijana niliyemfanya Rafiki,ndie Tukawa tunamtumia kwa dharula pale,Boss hana hata Moja hajui tunatokaje hapo ,Njaa,Njaa,Dogo akatutafutia kuku ,akasonga na ugali.Kumbuka tuna hela na tuko na Boss ila hapo hakuna Bar,Mgahawa Wala duka! Wanategemea minada ya kila mwezi kununua mahitaji Yao .Baada ya hapo asubuhi tukampa kijana ya kwenda mjini Singida na kuziba pancha na kurudi jioni na tyre!Kwa ufupi boss wangu alijifunza vitu vingi na Heshima debe!.Sure pesa si kila kitu kuna mahali haiitajiki pesa hata uwe nazo!.Mungu mwema humpa ampendaye na Humnyima ampendaye vilevile!