2011 UDSM nilinusurika kukamatwa

Mkuu ukifuatilia maisha ya JF na kutaka mtu afanye unavyotaka utapata tabu sana mkuu, kuna mtu id siiweki hapa mada zake za humu anazoandika pale MMU na status yake ni tofauti.

Fuata kilichokuleta lasivyo utaonekana umetoroka Milembe
Unajua kusoma?
 
salumu nashangaa hili jina la hapy limetokea wapi nakosa majibu
jamaa alijifanya mwanaharakati picha yake ikaonekana gazetini akiwa dodoma kavaa sare ya chama...
gazeti likabandikwa pale cafteria ya pili baada ya manzese pale walikua wanaekaga matangazo mengi
ndo raia wakajua jamaa ni CCM
Huyu alikua anajifanya mwanaharakati sana ila hamna kitu, afu alikua anapenda mademu weupe wembamba warefu sema alikua hana swaga la kutongozea...swaga lake la kutongozea ni kujifanya anasoma sheria
 
Dah...huo mgomo ulifanya watu kua wanariadha kwa lazima. Nakumbuka tukiwa gate maji tukaamriwa kurudi nyuma tukajidai tumekaza, zikapigwa tear gas watu walitafutana sana kukimbilia COET na wengine sehemu tofauti tofauti.. Hao wanaharakati walikua na uwezo wa juu mno ku-convice na kuteka akili za watu. Watu walikua wako radhi mvua iwanyeshee pale Rev square kusikiliza nondo za hao jamaa....missing you muuuuuch UDSM.
Sisi tuliosoma vyuo vya kanisa hatuna pa kuchangia maana utii ulitamalaki
 
Mimi sijasema.
Ila UD nilijiunga 2010 na nilikutana na masekeseke sana.
Na masekeseke nilianza nayo secondary, kama unakumbuka 2008-2010 shule nyingi zilikuwa na fujo sana.
Shule nyingi za advance wanafunzi tuligoma kwa sababu kwa sababu ya wazabuni kugoma kusaplay chakula na wanafunzi tukaanza kupewa vyakula vya ovyo. Ndipo wanafunzi tukanza kugomq hqli iliyopelekewa shule kuwa zinafungwa kwa muda usiojulikana. Hadi usikie Tangazo kwenye redio na Tv.
Kimbembe cha Udsm kwenye maandamano ya kudai bumu la sh. 10,000/=. Mwita ndie alianza kuandamana pekee yake.
Baadae akamobulize na kuandaa kunji la kwenda White House ambalo lilikomea suvey na kupata Mabomu ya machozi ya kutosha.
 
Mimi nilikua kiongozi kwenye moja ya kitivo na nilifukuzwa kutokana na huu mgomo ila badae nilirudishwa baada ya kuonekana sina hatia.
 
Aiseee Ndunguru alikua mbishi kwelikweli alianza kuandamana peke yake akiwa peku,, daaah Tanzania kuna watu walikua na mioyo ya kipekee sana,, imagine alikua na mkopo na alikua mwaka wa tatu anamaliza lakini alishindwa kukaa kimya mwanafunzi wa mwaka wa kwanza alipokosa mkopo. Halafu akaja funga kazi aliejiita alshabab,,
Hahahaha ndunguru nilisoma nae milambo high school, nikaja nae pale ud ,jamaa ni noma alikua anafoka pale utawala , huyu alshababu alianzia mabibo hostel alifunga kazi akiwa na demu flani ivi
 
Daah mabibo nilikaaga kuanzia 2nd year hadi mwaka wa mwisho kulikuaga fresh sana misosi pale kwa wale wapemba ilikua si mchezo, victoria hata siikumbuki ilikuaga ipo sehemu gani? Au ule mtaa wa nyuma ulioongozana masteshenari kama ukiwa unakula shato pori?

Victoria ni mgahawa ambapo kuna ATM
 
Duuu.Ni shidaaa.Hakika kwa sasa hatuna tena vyuo.Unakumbuka mabomu ya Mlimani City kwenye harakati ya kwenda ikulu?.Kwa kifupi,CASS ilipoteza wawili.Hao wote tulikuwa nao kwenye literature.
hapana usiseme hakuna vyuo. but in short ni kwamba vyuo vingi vya serikali kero hakuna. na kumbuka kero kubwa ilikuwa bumu ila sasa hivi bumu halichelewi hata wiki moja sasa migomo itatokea wapi?
 
du umenikumbusha mbali vijana wa main cumpos walikuwa waomga mipango yote ilikuwa inaanzia mabibo chini ya alshababu jamaamoja alikuwa anajiita sokwe na manzii moja ya arusha jina nimelisahau
mi nikijikuta nipo mwenge dani ya dakika kumi au kumi na tano
 
hapana usiseme hakuna vyuo. but in short ni kwamba vyuo vingi vya serikali kero hakuna. na kumbuka kero kubwa ilikuwa bumu ila sasa hivi bumu halichelewi hata wiki moja sasa migomo itatokea wapi?
Hiyo sio sababu ya msingi kabisa.Kumbuka kipindi hiki ni wanafunzi wachache sana wanapata mikopo,kitu ambacho kilichangia migomo kwa wakati wetu.Kwa sasa wanafunzi wanahofu sana kutokana na utawala wenyewe ulivyo.
 
Shule nyingi za advance wanafunzi tuligoma kwa sababu kwa sababu ya wazabuni kugoma kusaplay chakula na wanafunzi tukaanza kupewa vyakula vya ovyo. Ndipo wanafunzi tukanza kugomq hqli iliyopelekewa shule kuwa zinafungwa kwa muda usiojulikana. Hadi usikie Tangazo kwenye redio na Tv.
Kimbembe cha Udsm kwenye maandamano ya kudai bumu la sh. 10,000/=. Mwita ndie alianza kuandamana pekee yake.
Baadae akamobulize na kuandaa kunji la kwenda White House ambalo lilikomea suvey na kupata Mabomu ya machozi ya kutosha.


Nimemkumbuka Mwita alikuwa na kengeza.

Alianza kwa kuandika bango kwa Maker pen nyekundu maandishi makubwa yanasomeka "BOOM 10,000/=" halafu akaenda kusimama katikati ya Barbara ya Sam Nujoma maeneo inakoanzia University Road.

Alishika bango uelekeo wa Ubungo Mataa.

Ninakumbuka alivaa nguo za kaki enzi hizo CHADEMA iliwika sana.
 
Wenzio wanapambana ww unakimbia hufai kwa mabadiliko

Nilimaliza kwa amani.

Na baada ya masomo nimefanya mabadiliko.

Nimejituma kufanya kazi na siasa pia ninafanya kwa kufuata sheria za nchi.

Mabadiliko siyo kuandamana bila sababu ya msingi.
 
kipindi hiki ndo usnich , ulafi na undumilakuwili wa ALLI HAPI huyu gavana wa Iringa ulivyoanza kuonekana kuna jamaa yangu anasema angejua angemchoma hata bisibisi ili aonekane amekufa kwenye vurugu za maandamano maana Iringa ingekuwa na kiongozi bora sasa hivi.
 
Back
Top Bottom