2011 UDSM nilinusurika kukamatwa

Sisi tulikuwa na test kule yombo asubuhi tulivyogawiwa tu mitihani tukavamiwa na ilikuwa si mchezo kukiwa na mgomo nyie mkasaliti mnachalazwa hatari tulivyosikia tu wanakuja wanaimba kila mtu haijulikani alitokaje mlangoni si kwa mbio zile kulikuwa na malecturer wawili wakisimamia mtihani walitimua km vichaa test ikawa imavurugwa baada wa mgomo kuisha tulitungiwa test nyingine ilikuwa ngumu km mpingo tulikoma
Kweli wewe ngishi, kikulya ni boya sana!!
 
Huyo huyo Ndunguru akafika revolution square pale, akaanza kutema hoja baada ya muda watu wakajaa, jamaa yuko peku peku anaongea balaa. Kilichokua kinasisimua zaidi ni hoja zilivyokua zinatolewa. Baada ya Ndunguru na wengine kukamatwa sasa ndio chuma Alshabab kilipoamka sasa,, akaanza peke yake ku mobilize watu na kuhubiri. The guy will make a very good politician sijui yuko wapi siku hizi.
Mkuu endelea kufafanua kidg maana wengine tulisikia tu redioni
 
Daah udsm ilikuwa raha enzi zile, nakumbuka tukiwa lekicha na msaidizi wa mkandala Dr kessi,siku hiyo Prof hakuja pale Theatre one wakamvamia Kessi,daah akaanza kuomba kwa kuwaambia mimi siyo Mkandala.Ndo Lekicha ikaishia hapo

msomi wa chuo kikuu hata neno "lecture" tu linakushinda kuliandika kwa ufasaha badala yake unaandika "lekicha". sasa si bora tu ungeandika "mhadhara wa kitaaluma"

kumbe bora hata mimi niliyeishia darasa la nne B.
 
Kipindi hicho shule nyingi zilikuwa zinakabiliwa na baa la njaa, kama kumbukumbu ziko sawa kipindi hicho wazabuni waligoma kwa sababu serikali ilikuwa haijawalipa kwa muda mrefu, baadhi ya shule zilifikia hatua ya kufungwa kwa ukosefu wa chakula


Sawa kabisa.

Umenikumbusha kitu.

Kuna wakati tuligoma na kufanya fujo baada ya kupikiwa kande badala ya WALI maana mzabuni hakuleta MCHELE.

A level nilirudi nyumbani Mara mbili baada ya vurugu.

Nimemaliza tu, kufika chuo nako nikakutana na virungu.

Fujo ikianzia Mabibo, mimi nawahi Main Campus, wakija main campus naenda Mbezi
 
Sawa kabisa.

Umenikumbusha kitu.

Kuna wakati tuligoma na kufanya fujo baada ya kupikiwa kande badala ya WALI maana mzabuni hakuleta MCHELE.

A level nilirudi nyumbani Mara mbili baada ya vurugu.

Nimemaliza tu, kufika chuo nako nikakutana na virungu.

Fujo ikianzia Mabibo, mimi nawahi Main Campus, wakija main campus naenda Mbezi
Hahaha mwanaume wa Dar
 
Ilikua hivi, mwaka wa kwanza 2011, walipangiwa chuo wengi wao wakikosa mikopo. Kwa hiyo baada ya muda wengine wakaanza kuacha masomo kwa ugumu wa maisha na kushindwa kulipa ada.
Wakati huo wote kulikua kikundi cha watu wachache waliokua wanajiita ama kuitwa wanaharakati, muda wote walikua wakifanya jitihada na kuwasiliana na uongozi wa chuo (DARUSO) ili vijana wa mwaka wa kwanza wapewe mikopo wote.

Juhudi hizi zilipogonga mwamba sasa ndio inakuja option ya mwisho ya kuandaa mgomo ambapo vijana wanaanza kuandamana sasa.
Mkuu endelea kufafanua kidg maana wengine tulisikia tu redioni
 
Ilikua hivi, mwaka wa kwanza 2011, walipangiwa chuo wengi wao wakikosa mikopo. Kwa hiyo baada ya muda wengine wakaanza kuacha masomo kwa ugumu wa maisha na kushindwa kulipa ada.
Wakati huo wote kulikua kikundi cha watu wachache waliokua wanajiita ama kuitwa wanaharakati, muda wote walikua wakifanya jitihada na kuwasiliana na uongozi wa chuo (DARUSO) ili vijana wa mwaka wa kwanza wapewe mikopo wote.

Juhudi hizi zilipogonga mwamba sasa ndio inakuja option ya mwisho ya kuandaa mgomo ambapo vijana wanaanza kuandamana sasa.
Huyu alishabab vipi nimekua interested Na huyu kiumbe
 
Back
Top Bottom