Ushirombo
JF-Expert Member
- Jan 22, 2013
- 3,557
- 2,692
Kifupi Rev.Square bro
Revolution square
Revolution square
Huu mwaka sitausahau pale mlimani.
Washikaji zetu ,Christopher mbusule, Lusako ,Ndunguru na wengine wengi tu walipoteza chuo.
Mlimani city ilikuwa jumba la maficho . Tulikimbia tukajificha kwenye maduka. Wale jamaa walikuja na hasira kama za simba wakitutafuta.
Poleni sana washikaji wote mliopoteza chuo kipindi Hicho. Harakati zenu zilifanyika neema kwa wengine.
Mungu bado anatupigania . Siku zimepita na maisha yanaendelea.
Tulikuwanae pia kwenye literature.Alikuwa CASS.Nilichojifunza kwenye wengi poana mengi. Wewe unaweza ukawa unafikiri kua lengo lenu ni moja ila kumbe miongoni mwenu kuna watu wana maelngo tofauti kabisa na maovu. Kusema kweli mgomo wa 2011 ulikua wa mwisho na sidhani kama itakaa kutokea mgomo mwingine tena kwenye vyuo vikuu.
Vijana walifanikiwa kwa asilimia mia moja kwenye mgomo ule japo furaha iligeuka msiba baada ya kusherehekea ushindi kwa kutaka kwenda kutoa kipigo kwa viongozi wa serikali ya wanafunzi (DARUSO) ambapo ilikuja kutafsiriwa kama jaribio la kutaka kupindua serikali ya wanafunzi.
Wakati mwingine najiuliza kama wale wanaosomea uandishi wa habari (Mass communication) matukio kama yale hawawezi hata kuyaandalia habari kwa kina na kuja na kitabu au makala zinazoelezea kwa kina kiini cha tatizo na masimulizi mpaka ilivyoisha na hasara au faida zilizopatikana.
Ila yote kumi tisa yule jamaa aliyejiita alshabab alikua mtu wa tofauti sana (Charismatic leader) kwa waliokuwepo mitaa ya chuo na kufatilia kiundani jamaa alijaliwa uwezo wa kushawishi watu.
jina lake lilikua halifahamiki kwa hiyo hata utawala walipata shida sana kumdhibiti mana hawajui ni nani wala anasoma kozi gani, alisumbua sana.
Duuuuuuuuu.Kwa kifupi ni kuwa, hakuna tena harakati?Revolution Square siku hizi wametia senyenge pale huwezi hata kupanda juu
Ndio mkuu 🙏🙏Na wewe ni mhitimu toka UDSM ?
Yani ilifika hatua kwamba kama hautaki chuo ukipanda tu pale Revo Square hata kama hujasema kitu jina laki linapelekwa utawala unakua huna chuoDuuuuuuuuu.Kwa kifupi ni kuwa, hakuna tena harakati?
SawaKifupi Rev.Square bro
Nyoka walimwagwa wengi sana aiseeYani ilifika hatua kwamba kama hautaki chuo ukipanda tu pale Revo Square hata kama hujasema kitu jina laki linapelekwa utawala unakua huna chuo
Mwaka gani ?Ndio mkuu
mgomo wa 10000Aisee nadhani huu mgomo ndo ule hadi alikuja waziri kawambwa aisee watu walishuka mpaka kuke kwenye swimming pool jamaa yule Laizer akaanza kumuita "Kawambwaaa Kawambwaaa Kawambwaa" nimekuita mara tatu kama isingelikua Nyerere usingesoma bure, aisee baadae nakumbuka polisi wanaondoka wakaanza ku4ushiwa makopo na mawe na kuitwa form 4 failure aisee mbio zilitimuka siku ile sitasahau nimefika Hall 1 ikabidi njegere zote zikaharishwe hahahaha...ila ilisaidia boom likawa 7500 badala ya 5000 nilienjoy sana kwa kweli daaah...ila maumivu ya bodi nayasikilizia sasa hivi hatari tupu...
Duuu.Ni shidaaa.Hakika kwa sasa hatuna tena vyuo.Unakumbuka mabomu ya Mlimani City kwenye harakati ya kwenda ikulu?.Kwa kifupi,CASS ilipoteza wawili.Hao wote tulikuwa nao kwenye literature.Yani ilifika hatua kwamba kama hautaki chuo ukipanda tu pale Revo Square hata kama hujasema kitu jina laki linapelekwa utawala unakua huna chuo
Hakika mkuuDah...huo mgomo ulifanya watu kua wanariadha kwa lazima. Nakumbuka tukiwa gate maji tukaamriwa kurudi nyuma tukajidai tumekaza, zikapigwa tear gas watu walitafutana sana kukimbilia COET na wengine sehemu tofauti tofauti.. Hao wanaharakati walikua na uwezo wa juu mno ku-convice na kuteka akili za watu. Watu walikua wako radhi mvua iwanyeshee pale Rev square kusikiliza nondo za hao jamaa....missing you muuuuuch UDSM.
Sie darasani kwetu jamaa wawili waliwasimamisha masomo wakaja kurudi chuo sie tupo mwaka wa mwisho, yani mkuu baada ya mbio zile za kutoka kule kwenye swimming pool ukichungulia nje unaiona land cruiser ya polisi ilee inafanya doria..hao jamaa wawili walifariki au?Duuu.Ni shidaaa.Hakika kwa sasa hatuna tena vyuo.Unakumbuka mabomu ya Mlimani City kwenye harakati ya kwenda ikulu?.Kwa kifupi,CASS ilipoteza wawili.Hao wote tulikuwa nao kwenye literature.
Mbona bavicha wanasema kipindi cha jk maisha yalikuwa rahisi sana na pesa bwerere tu?Kipindi hicho shule nyingi zilikuwa zinakabiliwa na baa la njaa, kama kumbukumbu ziko sawa kipindi hicho wazabuni waligoma kwa sababu serikali ilikuwa haijawalipa kwa muda mrefu, baadhi ya shule zilifikia hatua ya kufungwa kwa ukosefu wa chakula
unajua kilichosababisha siku zile ffu wapige mabomuDah...huo mgomo ulifanya watu kua wanariadha kwa lazima. Nakumbuka tukiwa gate maji tukaamriwa kurudi nyuma tukajidai tumekaza, zikapigwa tear gas watu walitafutana sana kukimbilia COET na wengine sehemu tofauti tofauti.. Hao wanaharakati walikua na uwezo wa juu mno ku-convice na kuteka akili za watu. Watu walikua wako radhi mvua iwanyeshee pale Rev square kusikiliza nondo za hao jamaa....missing you muuuuuch UDSM.
Kinachoniuma ni kuwapoteza course mates wetu,akiwepo Alshabab.mgomo wa 10000
watu walirusha chupa kwenye msafara wa kawambwa ffu walitembeza mabomu
niliumia kidole hadi leo kicha aioti vizuri
wale wahuni walirusha hadi moto ukawaka maeneo ya COET
nilikuwa 100% ya huo mgomo ulipoanza hadi kuisha