2011 UDSM nilinusurika kukamatwa

2011 UDSM nilinusurika kukamatwa

nilipita hapo juzi kati kumeota kichaka kikubwa..hahahah unafikiri historia yenu itafutika pale??
ni kama historia ya kina ODWANG ambayo kila anaeingia pale anaikuta
tena kipindi hichi cha Magu hamna atakaedhubutu
Waendelee kula viepe vya kaseja tu sijui nae kama bado yupo pale
 
Huu mwaka sitausahau pale mlimani.

Washikaji zetu ,Christopher mbusule, Lusako ,Ndunguru na wengine wengi tu walipoteza chuo.

Mlimani city ilikuwa jumba la maficho . Tulikimbia tukajificha kwenye maduka. Wale jamaa walikuja na hasira kama za simba wakitutafuta.

Poleni sana washikaji wote mliopoteza chuo kipindi Hicho. Harakati zenu zilifanyika neema kwa wengine.

Mungu bado anatupigania . Siku zimepita na maisha yanaendelea.
Umemsahau Machibya na Odong...Odong walimweka Central halafu interpol wakamsepesha fasta mpaka uganda
 
Alikua shemela wangu, haha alikua anatoka na best friend wangu enzi hizo mapenzi motomoto bahati mbaya interpol wakawatenganisha
😂😂😂😂😂😂😂au ulikuwa unamtunuku tundaaaaaaaaaaa!.Maana si unajua tena kichuo chuo.😂😂😂😂
 
Huu mwaka sitausahau pale mlimani.

Washikaji zetu ,Christopher mbusule, Lusako ,Ndunguru na wengine wengi tu walipoteza chuo.

Mlimani city ilikuwa jumba la maficho . Tulikimbia tukajificha kwenye maduka. Wale jamaa walikuja na hasira kama za simba wakitutafuta.

Poleni sana washikaji wote mliopoteza chuo kipindi Hicho. Harakati zenu zilifanyika neema kwa wengine.

Mungu bado anatupigania . Siku zimepita na maisha yanaendelea.
Umenikumbusha James Mbatia alivyotimuliwa kwa mambo kama hayo enzi za Mwinyi!
 
sina kumbukumbu vizuri lakini mgomo wa 10000 ulikuwa mzito ndo pesa ikapanda mpaka leo 7500 imegota hapo sijui kama imeongezeka
Tulidai 10,000 tukaongezewa ila 7,500 ila sasa hivi naskia ni 8,500 yani hadi leo haijafika 10,000 kwa siku daah ila enzi zile maisha yalikua marahisi sana yani RB 600 Wali Kitenesi(Njegere) ilikua 800 daah na juice ilikua 300 yani 3000 unaishi vizuri kabisa daah
 
Dah...huo mgomo ulifanya watu kua wanariadha kwa lazima. Nakumbuka tukiwa gate maji tukaamriwa kurudi nyuma tukajidai tumekaza, zikapigwa tear gas watu walitafutana sana kukimbilia COET na wengine sehemu tofauti tofauti.. Hao wanaharakati walikua na uwezo wa juu mno ku-convice na kuteka akili za watu. Watu walikua wako radhi mvua iwanyeshee pale Rev square kusikiliza nondo za hao jamaa....missing you muuuuuch UDSM.
Mkuu mm nilkimbilia pale kwenye kaa zahanati kachuo huku mabomu yakirindima nje
 
Kulikua na jamaa ana jicho flani kama bovu tukimwita Baraka kijicho, ila yote kwa yote ni Alshababu alikuja pale Bibo tukakusanyika block G ilikua na amsha amsha mno. Sijui akili zilikuaje tu.
Siku hizi hapa block G wapendanao ndio hukaa kuliwazana kunako majira ya jioni
 
msomi wa chuo kikuu hata neno "lecture" tu linakushinda kuliandika kwa ufasaha badala yake unaandika "lekicha". sasa si bora tu ungeandika "mhadhara wa kitaaluma"
kumbe bora hata mimi niliyeishia darasa la nne B.
acha upoyoyo wewe yaani kwa akili yako unaamini kashindwa?
 
  • Thanks
Reactions: Pep
Back
Top Bottom