Mgombea urais wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu, amesema kuwa licha ya pikipiki za biashara maarufu kama bodaboda kuwa mkombozi wa ajira kwa vijana wengi nchini, ipo hatari kubwa sekta hiyo kupoteza maana kama suluhisho la ajira endapo serikali haitatafuta mbadala wa kudumu...
Maafisa wa usafirishaji wa Stendi ya Zamani, Singida wametakiwa kuendelea kuwa mfano wa kuigwa katika kulinda amani na utulivu, hususan kipindi hiki kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025 kwa kuwa amani ni msingi wa maendeleo na si jukumu la vyombo vya dola pekee, bali la kila mwananchi
Wito huo...
Mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM, Dkt. Samia Suluhu amesema alikasirishwa kuona makundi ya watu wakisubiri usafiri usiku kwenye vituo vya daladala, ambapo ameeleza kuwa changamoto hiyo itamalizwa karibuni.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima, ametoa onyo kali kwa makundi au watu wenye nia ya kuanzisha fujo ama vurugu wakati wa kipindi cha uchaguzi Mkuu wa Tanzania, akisisitiza kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vipo imara na makini kuhakikisha amani na utulivu vinaendelea kudumishwa nchini...
Mkurugenzi wa Everlasting Legal Aid Foundation, Dokta Khamis Masoud, amezungumzia umuhimu wananchi kupiga kura pamoja na madhara ya vurugu na maandamano wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani Jumatano ya Oktoba 29 mwaka huu.
Said Miraj, Mtaalamu wa masuala ya Siasa ameeleza umuhimu wa Mtanzania kushiriki uchaguzi mkuu Oktoba 29, faida zinazoweza kuletwa na mabadiliko yanayoweza kutekelezwa na kura yake.
Said ameeleza umuhimu na utekelezwaji wa sera ya vyama vingi, namna inavyofanya kazi nchini kulinganisha na...
Mgombea wa uraisi kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Samia Suluhu Hassan amesema awali katika Mkoa wa Dar es Salaam kulikuwa kunachangamoto ya umeme lakini kutokana na kazi kubwa iliyofanyika, hadi kufikia sasa katika mkoa huo nishati ya umeme inapatikana kwa saa 24
“Si muda mrefu uliopita...
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Arusha Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Paul Makonda, ametoa wito kwa wavuvi wa samaki katika kata ya Kivukoni, jijini Dar es Salaam, kuendelea kulinda amani ya nchi na kutokubali kushawishiwa kuvuruga hali hiyo ya utulivu iliyopo Nchini.
Akizungumza na wavuvi...
Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Gombo Samandito Gombo alipokutana ana kwa ana na mgombea urais kupitia chama cha Kijamii CCK David Daud Mwaijojele, walipokutana ana kwa ana na kujibu nai kati yao atashinda urais?
Vyombo vya ulinzi na usalama mkoani Geita vimeendelea kuimarisha ulinzi na usalama ili kuhakikisha amani, usalama na utulivu kabla, wakati na baada ya kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Oktoba 29, 2025.
Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya...
Mgombea urais wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu, amesema akiingia Ikulu atarejesha hadhi ya Bunge madhubuti lenye hoja, usimamizi na uwajibishaji wa serikali, badala ya kuwa la kusifia.
Amesema hataki kuona bunge la “machawa” wanaomsifia rais muda wote badala ya kuikosoa...
Mgombea Udiwani kupitia Chama cha National League for Democracy (NLD) katika Kata ya Kinyerezi, Halmashauri ya Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam, Seleman Shimbi, anadaiwa kutoweka na hajulikani alipo kwa zaidi ya siku sita sasa.
Katibu Mkuu wa chama hicho, ambaye pia ni Mgombea Urais, Doyo...
Mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF), Gombo Samandito, amesema kuwa tatizo la rushwa limekikumba chama chake baada ya baadhi ya wagombea na mawakala kujitoa dakika za mwisho, hali inayotishia uhalali wa ushindani wa kisiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29 mwaka huu...
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Kanda ya Kusini na Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Aden Mayala Oktoba 22, 2025 alijiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM), akisema amechoshwa na manyanyaso ndani ya kilichokuwa chama chake
Akizungumza Oktoba 22, 2025 katika...
Zikiwa zimebaki siku sita kufanyika uchaguzi mkuu, zaidi ya viongozi 200 wa dini wa mikoa ya kanda ya kaskazini wameonyana, asitokee wa kuvuruga amani ya nchi.
Akizungumza Oktoba 22, 2025 katika semina ya amani iliyofanyika Moshi Mjini, ikiwahusisha viongozi wa dini mbalimbali wa mikoa ya...
Mratibu wa Polisi Jamii Wilaya ya Ukerewe, Mkoani Mwanza, SP Raphael Ganchira, ametoa elimu kwa wananchi wa Kata ya Bwilo kuhusu umuhimu wa kutunza amani.
Akizungumza katika mkutano huo uliofanyika Oktoba 21, 2025, katika kisiwa cha Bwilo, SP Ganchira alisema lengo la elimu hiyo ni kuhamasisha...
Mkoa wa Kipolisi Kinondoni kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama vilivyopo ndani ya Mkoa huo umefanya mazoezi ya pamoja Oktoba 3, 2025.
Mazoezi hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Jeshi la Wananchi Mwenge – Kikosi cha Bendi, yalihusisha matembezi mafupi (route match) pamoja na...
Madereva wa bodaboda na bajaji wa Wilaya na Mkoa wa Singida wametakiwa kuwa mstari wa mbele kuhubiri amani na utulivu, hasa kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025, kwa kutambua kuwa shughuli zao hutegemea uwepo wa usalama na utulivu nchini.
Wito huo umetolewa Oktoba 17, 2025 na Mkuu wa...
Akizungumza na wavuvi wa Bwawa la Tambuko katika Kijiji cha Mwahango, Kata ya Ilongero, Oktoba 17, 2025, INSP Asajile Mwatujobe aliwahimiza kudumisha utulivu na amani katika maeneo yao.
Amesisitiza umuhimu wa kuepuka kushiriki au kuunga mkono vikundi vyenye malengo ya uchochezi, hasa katika...
Mkoa wa Kipolisi Kinondoni kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama vilivyopo ndani ya Mkoa huo wamefanya mazoezi ya pamoja Oktoba 04, 2025 Ikiwa ni pamoja na matembezi mafupi (Route match) na mazoezi mbalimbali ya mwili, katika viwanja vya Jeshi la Qananchi Mwenge Kikosi cha Bendi.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.