uchaguzi 2025

No Wikipedia entry exists for this tag
  1. C

    GE2025 Tanzania haiwezi kuvushwa na CCM ,HAIWEZEKANI ni lazima itafutwe namna ya kuikomboa hii nchi kwa mara nyingine

    Ndivyo ilivyo na msio ukweli , CCM haiwezi tena kuikomboa hii nchi na kuipeleka kwenye maendeleo ya kweli yanayo lingana na rasilimali zilizopo na sasa ndio kabisaa imesha jiingiza kwenye tope zito kabisa
  2. H

    GE2025 Babalevo: uwezo ule wa kuwasemea wananchi ndiyo sifa yangu pekee kubwa niliyonayo....

    Kazi kubwa ya diwani/mbunge ni kuwasemea wananchi wao matatizo yanayosibu ili kupata ufumbuzi kwa maendeleo ya watu wake hayo mengine i.e:kutunga sheria,kupangua hoja,kujadili miswada ni ziada tu na ujanjaujanja ili kuwaibia watu kwani hata madiwani wanatunga sheria ndogondogo bwana? Hili...
  3. W

    GE2025 Mpina: Wamenifukuza bungeni baada ya kuwakaba, nilikataa mipango yao ya kuuza bandari na rasirimali za nchi

    Mpeperusha bendera ya Urais kupitia chama cha ACT Wazalendo, Luhaga Mpina anasema kuwa sababu ya yeye kufukuzwa bungeni ni baada ya kuwakaba sana na kupinga baadhi ya mipango ikiwemo kuuza bandari na rasilimali za nchi. "Viongozi uliowapa dhamana wamefika mahali wanasema kwamba wanakula kwa...
  4. msuyaeric

    GE2025 Rais Samia atakavyopata Ushindi Kupitia Wagombea wa Ubunge wa CCM

    Uchaguzi Mkuu wa 2025 unakaribia. Rais Samia Suluhu Hassan anaonekana kuwa na nafasi kubwa ya kushinda na moja ya silaha zake kuu ni aina ya wagombea ubunge waliopitishwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM). Wagombea Wenye Ushawishi CCM imepitisha wagombea wanaopendwa na wananchi na wenye historia ya...
  5. Kichuguu

    GE2025 Inawezekana CCM haikuwa Makini katika kuteuwa Wagombea ubunge baada ya Kura za Awali

    Kumpitisha mshindi wa tatu kwenye primaries na kumwacha mshidni wa kwanza linaweza kuwa ni siyo tu kutokuheshimu demokrasia na maoni ya wananchi bali pia ni dalili ya udikiteta. Kuna majimbo ambao CCM inaweza kukosa kwa mfano Tarime Mjini, Tanga mjini na kwingineko...
  6. H

    GE2025 Babalevo ni Traore wa Kigoma mjini asipuuzwe, uongozi siyo elimu!!

    Walikuja wasomi kina Dkt Kaburu walifanya nini cha maana? Wabunge wasomi wangekuwa wa maana kungekuwa na ufisadi kila leo? Kujua kuongea kiingereza ndiyo kipimo cha elimu kwa waTanzania walio wengi na ingekuwa hivyo basi nchini uingereza wote wangekuwa wabunge
  7. McLaren

    GE2025 Tume Uhuru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC): Polepole hana uelewa na ufahamu kuhusu mfumo wa Uchaguzi

    Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imekanusha taarifa zinazodai kuwa mfumo wa uchaguzi unaotumika na Tume hiyo umeunganishwa na mfumo wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) na chama cha siasa, hususan Chama Cha Mapinduzi (CCM), pamoja na madai kwamba zoezi la upigaji kura tayari...
  8. McLaren

    GE2025 Mwenyekiti wa Asasi ya Wanafunzi ya Siasa UDSM: Hapa nchini unaambiwa ili utoboe unahitajika uwe na kadi ya chama fulani ili uwe karibu na mifumo

    Akiwa anazungumza kwenye kipindi cha Malumbano ya Hoja cha ITV Mwenyekiti wa Asasi ya Wanafunzi ya Siasa UDSM Antony Severine alisema: "Kama vyama vinaunganishwa na vijana kupitia ilani, ni dhahiri vijana ndio wanaoathirika na ilani za vyama hii imenikumba hata mimi, ambapo unaambiwa ili utoboe...
  9. Pascal Mayalla

    GE2025 Polepole, Asante kwa ukweli wako kuhusu kiini macho cha Uchaguzi. Hoja ya tusishiriki, haina tija tena na Uchaguzi Upo!

    Wanabodi Nimemsikiliza HP mwanzo mwisho, hoja zake ni za ukweli na za msingi sana kuhusu kiini macho cha uchauzi wa Tanzania. Ushauri wake watu wasijitokeze kupiga kura mpaka kwanza upatikane muafaka wa kitaifa, ni ushauri tenge kama ulivyo uwanja tenge wa uchaguzi, it's a bit too little too...
  10. W

    GE2025 Prof Kabudi: Wananchi wanahitaji habari zenye uzito wa hoja na si uzito wa posho, waandishi jiepusheni na bahasha za kahawia

    Wakati akizungumza kwenye Mkutano wa Wadau wa Sekta ya Habari Kanda ya Mashariki Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025, Waziri wa habari Prof Kabudi amewahimiza waandishi wa habari kuacha kupokea rushwa na bahasha za kahawia kwani wananchi wanahitaji habari zenye uzito wa hoja na si uzito wa posho...
  11. McLaren

    GE2025 Mtendaji Bodi ya Ithibati: Ni kosa la Jinai kufanya uandishi wa habari bila Ithibati, adhabu ni kifungo miaka mitatu

    Akizungumza leo kwenye Mkutano wa Wadau wa Sekta ya Habari Kanda ya Mashariki Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 Wakili Msomi Patrick Kipangula Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari amesema kwamba kwa waandishi wa habari ambao hawana Ithibati na wakaendelea kufanya uandishi wa habari...
  12. Tlaatlaah

    Polepole hana athari zozote kisiasa na kijamii. Asanteni Watanzania kwa kumpuuza

    Tabia za mpambanaji manafiki daima huwa ni pamoja na kua mwoga, mfitini, muongo na mzandiki. Na mara zote nia yake hua ni uchochezi na dhamira yake ovu hua ni migawanyiko. Ni jambo la maana sana waTanzania wamempuuza katika umoja wao na wamebaki wamoja. Maoni, mtazamo na mawazo yake kwa jamii...
  13. McLaren

    GE2025 Kamanda Muliro: Hakuna chama kinachotaka kichafuke kwenye shughuli ya mchakato wa Uchaguzi

    Wakuu, Akizungumza kwenye Mdahalo wa Wadau wa Amani Kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Wabunge na Madiwani 2025 Kamanda Muliro amesema kwamba watahakikisha Uchaguzi utafanyika kwa amani na vifaa vya Uchaguzi vitalindwa
  14. M

    GE2025 Polepole acha maneno fanya vitendo. Kama mchakato wa mgombea Urais wa CCM umekosewa, peleka barua ya malalamiko kwa Msajili wa Vyama

    Bwana Polepole ulichoongea tumekusikia, Ila sisi Watanzania huwa tunasema kuwa maneno matupu hayavunji mfupa!. Tumeshaona precedent ya watu wasiokubaliana na mwenenendo wa mambo katika vyama vyao ambavyo wao wanaamini katiba za vyama vyao zikivunjwa wakiandika barua rasmi kwa msajili wa vyama...
  15. W

    GE2025 Omary Mjengwa: Vyama vingi vya Tanzania havina siri. Unamueleza Mmarekani Tanzania ipo hivi na hivi ili iweje?

    Wakati akizungumza katika mkutano wa vya viongozi wakuu wa vyama vya siasa wakipatiwa mafunzo ya sheria ya gharama za uchaguzi. MWanadiplomasia na mbobezi wa Itifaki Omary Mjengwa amegusia suala la usiri ambapo ameeleza kuna vyama vya siasa havina siri. === "Vyama vingi Tanzania havina siri...
  16. Mindyou

    GE2025 Aliyejitokeza kupinga Mpina kuteuliwa kugombea Urais ACT Wazalendo afunguka. Kasema hajatumwa na mtu yeyote

    Wakuu. Mambo yanaendelea kuwa mazuri. Huyu hapa ni yule mdada aliyepinga Mpina kugombea Urais ACT Wazlendo. Anaitwa Ndala Monalisa. Leo akiwa kwenye interview Wasafi amejitokeza akisema kuwa hajatumwa na yeyote kupinga Mpina kugombea Urais ACT Wazalendo
  17. W

    GE2025 DC Kissa: Kipindi hiki cha Uchaguzi tutawatumia Mgambo kutazama Usalama

    Mkuu wa Wilaya ya Makete mkoani Njombe Kissa Kasongwa amewataka vijana waliohitimu mafunzo ya Jeshi la Akiba (Mgambo) kwenda kuwa wazalendo na nchi yao na kuilinda kwa wivu mkubwa ambapo pia ametoa ahadi ya serikali kuwatumia kwa ajili ya kutazama usalama katika kipindi cha uchaguzi. DC Kissa...
  18. K

    GE2025 Ninaiomba halmashauri kuu ya taifa kuchunguza ushindi wa mgombea aliyeongoza kura za maoni jimbo la Rorya

    Ratiba ya uteuzi wa watia nia kwa nafasi ya Ubunge inaanza tarehe 22 Agosti, 2025. Tayari kura za maoni zilikwishapigwa katika Majimbo yote. Kuna habari kuwa Katika Jimbo la Rorya wapiga kura wengi walinunuliwa kwa Rushwa na hivyo mshindi aliyeshika namba moja hakushinda kwa halali. Ninaiomba...
  19. U

    Askofu Gwajima, ulitafakari kwa kina Madhara, Matokeo na Maana halisi ya kauli yako ya kutoa siku 10 kwa Mamlaka kutekeleza madai yako?

    Unajua kuwa kauli yako ni sawa na kuitisha Serikali iliyopo madarakani na yaweza hesabiwa kuwa ni Uhaini? Ukweli Nchi yetu imejaaliwa viongozi wenye hekima na huruma hilo ndilo jambo la kumshukuru Mungu. Kwa upendo mkubwa nakushauri utazame vizuri mahali uliposimama na uombe radhi mapema kwa...
  20. JanguKamaJangu

    GE2025 Luhaga Mpina na Ferej Jumanne wachukua Fomu ya kuwania Urais Ofisi za INEC, Agosti 15, 2025

    Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele, leo tarehe 15 Agosti 2025 amekabidhi fomu za uteuzi kwa mgombea wa kiti cha Rais, Luhaga Mpina, na mgombea wa kiti cha Makamu wa Rais, Ferej Jumanne, kupitia Chama cha ACT Wazalendo. Hafla hiyo...
Back
Top Bottom