Wakati chama chetu kikiendelea kujipanga sawasawa katika mtanange Wa Ubunge na Udiwani katika majimbo yote 264 na kata zote 3,956 Mkt. wa Chama ameongea na watia nia wa Ubunge/Udiwani jimbo la Arusha Mjini (Jana) leo ni Jimbo la Moshi Mjini.
Wale wote wanaodhani wameitiwa kuwatumikia Watanzania...
Afisa Mwandamizi Usimamizi wa Fedha kutoka Management ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ndugu Geofrey Timoth leo asubuhi katika Ofisi za Chama Cha Mpinduzi (CCM) Wilaya ya Kinondoni amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea Ubunge wa Jimbo la Kawe kwa kupitia chama hicho.
Rais Magufuli anamaliza ungwe yake ya kwanza ya miaka 5 na sasa anakwenda ungwe ya pili 2020-25. Bila shaka atashinda kwa maana wapinzani wake wana hoja dhaifu na maandalizi yao ni muda mfupi kiasi ambacho wanakosa muda na agenda ya kupindua meza ya kifikra ili kuchukua Urais. Ila hoja yangu...
Mimi si mtu mzima sana ingawa nami najongea miaka ya kuweza kugombea Urais wa Tanzania kwa mujibu wa Katiba yetu ya sasa(miaka 40). Hatahivyo, nimekuwa mfuatiliaji mkubwa wa siasa na mambo ya kinchi tangu nikiwa mdogo. Leo, nitalizungumzia Bunge kama Mhimili mmojawapo wa dola. Mingine, wengi...
Mgombea Jacob Tesha akipokea fomu za kugombea ubunge kutoka kwa Kaimu Katibu wa CCM, Wilaya ya Moshi Ndugu Nada Orry.
Mtangazaji na Mwandishi wa Habari nguli nchini Ndugu Jacob Tesha leo ametinga Ofisi za CCM Wilaya ya Moshi kuchukua fomu za kuwania ubunge Jimbo la Moshi mjini. Mgombea...
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI), Mwita Waitara amechukua fomu kuomba Chama Cha Mapinduzi- CCM kimpitishe kuwania Ubunge Tarime Vijijini Mkoa wa Mara. Mwita Waitara 2015 alikuwa Mbunge wa Ukonga kupitia CHADEMA kabla ya kuhamia CCM na kutetea kiti chake...
Ndugu EMMANUEL KWAYU, mkurugenzi mkuu wa kampuni ya dolphin sea and air amejitosa kugombea ubunge jimbo la Hai kupitia chama cha mapinduzi. Jimbo hilo lilikuwa likishikiliwa na mwenyekiti wa chadema Freeman Mbowe.
Kwa mara ya mwisho alionekana Dodoma kwenye Mkutano Mkuu wa CCM akilalamika kuibiwa kura 2015 , naona sasa amekuja na mkakati mpya .
Mytake : Wassira bado yupo
Hatimaye mkongwe Kangi Lugola amechukua fomu za kugombea ubunge jimbo la Mwibara kwa tiketi ya CCM.
=======
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amejitokeza mapema leo katika ofisi za Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Bunda kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea ubunge katika...
Msando amewashukuru wote ambao wamempa moyo na kumtakia kheri, ''safari hii inapaswa kuwa ya pamoja”
Pia soma
- Je, Wakili Albert Msando anafaa ubunge wa Arusha Mjini?
- Celebrity Lawyer Albert Msando: Utajiri wa ghafla wamchanganya, afanya kufuru
Producer Mkongwe wa Muziki Joachim Marunda Kimaryo maarufu kama ‘Master Jay’ tayari amechukua fomu ya kugombea Ubunge katika Jimbo la Rombo kupitia CCM
Kumekucha CHADEMA.
Aliyekuwa mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea amesema hajachukua fomu za kugombea ubunge jimbo la Ubungo kupitia CHADEMA lakini hiyo haimzuii kugombea ubunge jimbo hilo hilo kupitia chama kingine
Maendeleo hayana vyama
======
Aliyekuwa mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea ameiambia...
Meneja wa Diamond na WCB, Babu Tale mapema leo amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea Ubunge Morogoro Vijijini kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM.
Tumaini Limbe mkazi wa wilaya ya Sengerema ametumia baiskeli kwenda ofisi za CCM kuchukua fomu kuwania ubunge jimbo la Sengerema huku akieleza kuwa kipato kidogo ndio sababu ya kutumia usafiri huo
Mgombea Ubunge jimbo la Handeni vijijini Hussein Msopa maarufu kama Sheikh Sharif Majini ni mmoja wa wagombea walionitokeza leo na amefika ofisi za CCM wilaya ya Handeni kwa ajili ya kusalimia na baadae kuelekea ofisi ndogo ya CCM Mkata kuchukua fomu ya kugombea Ubunge.
Bungeni patanoga huku...
Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Profesa Kitila Mkumbo, amejitokeza kuchukua fomu ya kuomba ridhaa ya chama chake kimteue ili aweze kugombea Ubunge katika Jimbo la Ubungo kupitia CCM.
M'kiti wa CHADEMA Jimbo la Ubungo na Diwani wa Sinza aliyemaliza muda wake, Renatus Pamba amejiuzulu na kutangaza kuhamia ACT Wazalendo kwa alichodai ni ubakaji wa demokrasia ndani ya CHADEMA hususan mchakato wa kumpata mgombea ubunge jimbo hilo na kudai uongozi wa juu kuwakandamiza wagombea...
Habari kutoka ndani ya chama jimbo la Kibamba zinasema mbunge wa sasa wa Kibamba Mheshimiwa John John Mnyika ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CHADEMA mpaka muda wa kuchukua fomu unaisha alikuwa hajachukua fomu ya kutetea kiti hicho.
Kama hizi habari ni za kweli je ni nini sababu? Ametosheka au...
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kwa siku ya leo, ikiwa ndio siku ya kwanza ya kuchukua fomu, watu 31 wamechukua fomu kwa Jimbo la Kinondoni huku 80 wakichukua kwa Jimbo la Kawe
Kwa upande wa Kinondoni, mtu mmoja tayari amerudisha fomu na kwa Jimbo la Kawe, watu wanne wamerudisha fomu hizo za...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.