Mwanasheria Mwandamizi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzaniania (TCRA) ambaye ni Katibu wa Kamati ya Maudhui inayofungia Vyombo vya Habari kwa kukiuka Kanuni za Maudhui mitandaoni, Dkt. Philip Filikunjombe amechukua fomu kuomba kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Ludewa
Mtoto wa Hayati Mwalimu Nyerere amechukua fomu ya kuwania ubunge wa Butiama mkoani Mara. Ikumbukwe hivi karibuni Madaraka Nyerere ambaye ni ndugu yake naye aliita waandishi na kutangaza nia ya ubunge jimbo hilo.
Pia soma > Uchaguzi 2020 - Madaraka Nyerere, mtoto wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius...
Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea ubunge Jimbo la Kawe kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi. ( aboodmediatz )
Mwijaku achukua fomu kuwania kuteuliwa na CCM kugombea ubunge katika Jimbo la Kawe. ( globalpublishers )
Aliyekuwa...
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea ubunge Jimbo la Arusha Mjini kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Mwenyekiti wa bendi ya African Stars (Twanga Pepeta), Asha Baraka akipokea fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea ubunge katika Jimbo la Kinondoni kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
=====
Asha Baraka alikua Mkurugenzi wa bendi ya Twanga Pepeta. Ameiongoza bendi hiyo kwa zaidi ya miaka 20.
Mbunge wa zamani wa Urambo Magharibi na waziri wa wizara mbili tofauti nchini, Profesa Juma Kapuya amechukua fomu ya kuwania ubunge jimbo la Kaliua, Tabora.
===
Prof. Juma Kapuya kama utakuwa unakumbuka alikuwa waziri wa ulinzi na mbunge wa Urambo Tabora wakati wa utawala wa Rais Mstaafu wa...
Aliyekuwa Meya wa jiji la Arusha Kalist Lazaro, leo Julai 14, 2020 amejitokeza katika ofisi za CCM wilaya ya Arusha kuchukua fomu za kuwania ubunge jimbo la Arusha mjini.
Msanii wa Bongo Movie, Steve Nyerere amefika katika Ofisi ya CCM Iringa Mjini kuchukua fomu za kuwani kugombea ubunge katika Jimbo la Iringa Mjini.
---
Muigizaji wa filamu nchini Steven Mengele, maarufu kama Steve Nyerere, amesema kuwa anawashukuru wale wote wanaomtishia
Msanii wa Bongo...
Dkt. Godfrey Simbeye amechukua fomu ya kuwania Ubunge Jimbo la Mbozi katika ofisi za CCM Mbozi na amekabidhiwa fomu hiyo na katibu wa CCM Wilaya Julius Mbwiga.
Siasa siasani.
Siri sirini.
Siasa ni sayansi ..siasa ni sanaa.
Kuna baadhi ya mawaziri huko nyuma hatukuwaza hata siku moja kuwa watakuwa wanasiasa ...wengi katika baraza la Magufuli hawakuwahi kuwa wanasiasa hata kwa Bahati mbaya..
Mfano
1. Mama Joyce Ndalichako hajawahi kuwa mwanasiasa...
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mh. Agrey Mwanri amechukua fomu ya kugombea Ubunge katika jimbo la Siha mkoani Kilimanjaro.
===
Aggrey Deaisile Joshua Mwanri amezaliwa Julai 17, 1955 alikuwa mbunge wa Siha tangu mwaka 2000, mwaka 2015 aliteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora na amestaafu...
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Joyce Ndalichako, leo Julai 14, 2020, amechukua fomu ya kuomba ridhaa chama chake ili kiweze kumteua, aweze kugombea Ubunge katika jimbo la Kasulu Mjini kupitia CCM.
====
Joyce Ndalichako alikuwa mhadiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuanzia 2000...
James Mbowe, mtoto wa kaka wa mwenyekiti wa CHADEMA Mh Freeman Mbowe amechukua fomu kugombea ubunge jimbo la Moshi Mjini kwa tiketi ya CHADEMA.
Freeman yeye alishatangaza kutetea kiti chake jimboni Hai mkoa huo huo wa Kilimanjaro.
Source: Ayo tv
Maendeleo hayana vyama!
Mong'oo wa Arusha ambaye ni mtoto wa Askofu Mkuu wa kanisa la Baptisti Tanzania, Arnold Manase amechukua fomu ya kuweka nia kuwania Ubunge Jimbo la Arusha mjini kwa tiketi ya CCM.
Fred Lowassa ambaye ni mtoto wa Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa achukua fomu ya kuwania ubunge jimbo la Monduli jijini Arusha.
======
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Monduli, Langael Akyoo, leo Jumanne July 14,2020 amemkabidhi Fredrick Lowassa fomu ya kuomba ridhaa ya Chama...
=======
Abbas Tarimba ambaye alikuwa Diwani wa Kata ya Ananasif, amechukua fomu za kuomba kuteuliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) kugombea Ubunge katika Jimbo la Kinondoni.
Waziri wa Uwekezaji, Angellah Jasmine Kairuki akichukua Fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Same Magharibi kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi leo Julai 14 , 2020. Anayemkabidhi fomu hiyo ni Katibu wa CCM Wilaya ya Same Victoria Mahembe.
=====
Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki (Alizaliwa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.