Watia nia ubunge kigoma mjini mpaka sasa kupitia ACT-WAZALENDO ni Abdul Nondo, Baba Levo. Bado najiuliza Zitto Kabwe atahama jimbo tena au atagombea nao kura za maoni, au hatagombea mwaka huu?
Waziri wa Mambo ya Nje wa zamani wa Tanzania na kada wa chama tawala cha Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa miongo mingi Bernard Membe anasema ikiwa Vyama vya Upinzani vitaungana na kumpa ridhaa ya kugombea nafasi ya Urais, basi atakuwa tayari kupambana na Rais John Magufuli katika uchaguzi mkuu ujao...
Mchakato wa kuchukua fomu utawajumuisha hata wale ambao hawakutia nia. Kila mwanachama anaruhusiwa kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa kuwania nafasi ya Urais, Ubunge na Udiwani- Katibu Mkuu wa Chadema, Mheshimiwa Mnyika.
Team salaam!
Safari ya TLP kuelekea Oktoba 2020 imepamba moto kwelikweli,
Leo chama chetu kimepokea tena Mgombea Wa Ubunge toka Same Magh Mhe. Mch Michael Msigati,
Kuna video inatembea ikomuonesha Steve Nyerere akijinadi kufika ofisi ile kuchukua fomu ya Ubunge.
Hivi hakumuelewa Dkt. Bashiru aliposema ni kuulizia tu utaratibu wa kugombea na kutangaza nia? Fomu zitatolewa kuanzia tarehe 14 hadi 17 July kupitia CCM.
Katika hali isiyoeleweka kama ni figisu za mchungaji Msigwa ama la, Mwalimu Andrew Palagio aliyetia nia kugombea ubunge Iringa mjini kwa tiketi ya Chadema amesimamishwa kazi.
Andrew ni mwalimu katika shule ya St Dominic Savio katika manispaa ya Iringa.
Ngoja tuone.
Maendeleo hayana vyama!
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Profesa Kitila Mkumbo ametangaza nia ya kugombea ubunge jimbo la Ubungo katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu kupitia Chama Cha Mapinduzi.
====
Kitila Mkumbo ni muhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ana phd ya Saikolojia, Maters ya Elimu...
Dkt. Magufuli ambaye ndiye Rais wa Tanzania leo atarudisha fomu ya maombi ya kugombea urais kupitia CCM kwenye makao makuu ya chama jijini Dodoma.
===
Updates:
Rais Magufuli anarudisha fomu ya maombi ya kugombea Urais wa Tanzania kupitia CCM kwenye Makao Makuu ya chama, Dodoma. Hadi sasa ni...
Mheshimiwa Membe nashindwa kuamini kuwa wewe ni mwanaintelejensia makini.
Intelligence maana yake ni uwezo wa kuona mbali zaidi ya wengine that's why hata hapa Tanzania ndege anayeona mbali hufanywa kama alama ya intelligency.
Ulipaswa ukae kimya miaka yote mpaka wiki ya kuchukua fomu...
Muandaji muziki maarufu Joachim Marunda Kimaryo (Master J) ametangaza nia ya kugombea ubunge jimbo la Rombo akiwa kwenye mahojiano katika redio ya Clouds FM kwenye kipindi cha XXL.
Master J amenukuliwa akisema "Mimi nipo CCM tangu zamani, natangaza nia, uchaguzi wa mwaka huu, Chama kikinipa...
Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Fatma Kombo Masoud amekuwa mwanamke wa tatu kujitokeza kuomba ridhaa ya chama hicho kugombea urais wa #Zanzibar
Fatma anafanya idadi ya watia nia kupitia Chama cha Mapinduzi hadi sasa kufikia 26 visiwani humo
------
Tunaweze kusema historia imevunjwa. Hadi...
Bi Hussina Amekamatwa na watu wanaosadikika kuwa ni Police, na yuko kituo cha Polisi Geita.
NYUMBANI kwake kumejaa Polisi nje na ndani. Kosa la yeye kushikiliwa halijulikani.
Zaidi soma:
Chato: Bendera za CHADEMA zashushwa na wanaodaiwa kuwa makada wa CCM. Mwanamama Husna Amri Said acharuka...
Hapo juzi aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani wa Tanzania shushu mbobezi, bwana Benard Camilius Membe alijitokeza kupitia mitandao ya kijamii akihoji juu ya uwepo wa tume huru ya uchaguzi. kauli ya Membe juu ya jambo hilo ilizua kelele nyingi miongoni mwa wahafidhina wa chama tawala ccm. kwao wao...
Wanawake wenye uthubutu wako wengi Sana! Ni Jambo jema; Na yote hayo yamepelekewa na sisi wanaume kutowatimizia mahitaji yao ipasavyo!
Huyo mama anaonekana Ni miongoni mwa wapambanaji
Biashara Ni VITA ya kiuchumi! Hupaswi kuingia mzimamzima kizembe Utapigwa KNO moja (noki Auti) na usirudi tena...
Huyu Mwamba, Benard Camilius Membe, huyu jamaa akiwa foreign Minister, kijana aliyekulia ndani ya kitengo, akiwa na mabilioni ya Gaddafi na maconnection kibao ndani hadi kwa Mabeberu, alitumia almost miaka mitano ya mwisho ya utawala wa J.K kujiandaa kuukwa Urais wa Jamhuri lakini hata kwenye...
Mwigizaji mkongwe wa vichekesho hapa nchini, Rashid Mwinshehe maarufu kama "Kingwendu" amesema kwa mara nyingine atagombea ubunge wa Kisarawe kupitia chama chake cha CUF na safari hii ameapa kumng'oa mshindani wake mkuu Suleiman Jaffo
Maendeleo hayana vyama!
Kingwendu amesema anagombania...
Wadau,
Mpaka leo 19/06/2020 wanachama 13 wa CCM wamechukua fomu kuwania kuteuliwa ili kugombea nafasi ya Urais katika visiwa vya Zanzibar.
Idadi hii sio haba, je ni kukua kwa demokrasia au kudhoofika? Je, hatma yake ni shwari au sharii? Yajayo yanfurahisha.
CCM oyee
===
---
Watia nia Mpaka sasa
1. Tundu Lissu
2. Freeman Mbowe
3. Lazaro Nyalandu
4. Peter Msigwa,
Hawa ni watia nia ambao ninawatenga katika makundi matatu
KUNDI A
Wanaoonekana kuimiliki chadema kimtizamo na mawazo ya waliowengi japo wana maono na ni wachapakazi
KUNDI B
Wanaoonekana Kuwa wapya na wana...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.