RC Chalamila atengua nia yake ya kugombea ubunge Iringa mjini

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,616
141,450
Mkuu wa mkoa wa Mbeya Albert Chalamila amesema anatengua nia yake ya kugombea ubunge katika jimbo la Iringa mjini na kwamba ataendelea kuwatumikia wana Mbeya.

Chalamila amesema baada ya kumsikiliza Rais Magufuli jana kwa tahadhari aliyotoa kwa wateule wanaoomba ruhusa, alimwelewa vizuri na ameamua kubadili gia angani.

Source: Azam tv

Maendeleo hayana vyama!

====

RC Mbeya, Albert Chalamila Atengua Uamuzi wake Wa Kugombea Ubunge

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila, amesema kuwa hawezi kukiuka maagizo ya Rais Magufuli aliyowataka wateule wake kuridhika na nafasi walizonazo, hivyo ameamua kuendelea kuwatumikia wananchi wake na hivyo hawezi tena kukimbilia kugombea Ubunge.
“Nilikuwa miongoni mwa watia nia ya kugombea ubunge Iringa mjini, kwa sasa sintofanya hivyo zaidi ya kuendelea kuwatumikia wananchi wa Mbeya na kutii maelekezo ya Rais Magufuli,” amesema Chalamila na kuongeza;

“Ni hekima na busara na itakuwa ni utoto wa kupindukia kama leo hii nitakwenda kuchukua fomu kugombea nikashinda kwenye kura za maoni, halafu huku Mwenyekiti wangu wa Chama cha Mapinduzi nimekwishamkwaza kwa kuwaacha Watanzania wake wakilia na kuhangaika”.

Kauli hiyo ameitoa leo Jumanne tarehe 7 Julai 2020 jijini Mbeya wakati akizungumza na Waandishi wa Habari na kuongeza kuwa kuna miradi mingi amepewa kuisimamia, hivyo itakuwa ni utovu wa nidhamu kuukimbia Ukuu wa Mkoa na kukimbilia Ubunge, huku akiacha miradi hiyo bado haijakamilika.

Wakati akiwaapisha viongozi aliowateua hivi karibuni, Ikulu Chamwino, jijini Dodoma Rais Magufuli alisema ili kazi ziendelee, taifa lazima liendelee kutatua matatizo ya kila siku ya wananchi, hivyo alisema hawezi kusubiri mtu anayeomba ruksa ya kusaka ubunge, akakose ndo arudi tena.
 
Kaogopa kutuma barua ya kuomba ruhusa, ili apate nafasi kuwania. Hajiamini yupo kwa cheo na kiki.
 
johnthebaptist,

Kwahiyo baada ya Rais kutoa rukhsa, then akajitathmini na akaona bora akimbilie kwenye media ili autetee ugali wake na familia yake.
Unamaanisha, alienda Azam TV kuomba kipindi ili ahojiwe alafu atengue kauli...
 
Msigwa atapumuwa sasa!

Mtakimbia wote na mwisho wa siku Mchungaji Msigwa atashinda uchaguzi saa mbili tu asubuhi. Uzuri mnaitambua nguvu yake.

Nasikia na kada wenu mwingine yule bongo muvi na mpigaji wa michango ya misiba, Steve Nyerere alishakimbia kitambo na kujutia kauli yake ya kutaka kugombea hapo Iringa Mjini.
 
Mtakimbia wote na mwisho wa siku Mchungaji Msigwa atashinda uchaguzi saa mbili tu asubuhi. Uzuri mnaitambua nguvu yake.

Nasikia na kada wenu mwingine yule bongo muvi na mpigaji wa michango ya misiba, Steve Nyerere alishakimbia kitambo na kujutia kauli yake ya kutaka kugombea hapo Iringa Mjini.
Yupo Pierre Liquid!
 
7 July 2020
Mbeya, Tanzania

Chalamila Aeleza Hoja Nzito za Kubaki Mbeya



Albert Chalamila mkuu wa mkoa wa Mbeya akiri kuwa alikuwa na mawazo ya kugombea ubunge siku za nyuma.

Ila kutokana na methali asiyesikia la mkuu huvunjika guu mwisho wa nukuu. Hivyo kwa kuwa kuna mambo mengi ya kuyafanya mkoani Mbeya anadhani aendelee kuchapa kazi badala ya kukimbilia kugombea nafasi ya kisiasa ya ubunge.

Mfano kuna kazi kubwa kusimamia ujenzi ktk sekta ya afya kama hospitali ya Rufaa mkoani Mbeya na vituo vya afya 19, sekta ya elimu pia inatakiwa kufanyiwa kazi mfano Rungwe sekondari, barabara kuelekea Busekelo , Airport ya Songwe kuendelezwa kuweka miundombinu ili ndege ziweze kuruka usiku... mradi wa REA unaofanywa na mkandarasi toka Tunisia kusambaza umeme vijijini...

Hivyo kila mtu ktk utumishi wa serikali akitimka kwenda kugombea nafasi za kisiasa kupitia chaguzi mambo yatakwama ya maendeleo......

Source : millard ayo
 
01 Julai 2020
Busokelo Mbeya,
Tanzania

HUU NI UPUUZI, HATUWEZI KUVUMILIA, NAVUNJA MKATABA, HATUWEZI KUBEMBELEZANA" - RC MBEYA MKUU



Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila, amevunja mkataba wa ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Busokelo lenye kugharimu Bilion 5.2 baada ya kampuni ya Mzinga Holding Company kushindwa kukamilisha ujenzi huo kwa wakati.

Source : Global TV online
16 Jun 2015 · Mzinga Corporation is a Government Institution under the Ministry of Defence. The Corporation's Head Office is in Mzinga, Pwani.
 
Songwe International Airport
Mbeya Songwe
Tanzania

Jengo la abiria toka 2018 mpaka sasa tarehe 7 Julai 2020 linaendea kufanyiwa matengenezo



Source: MbeyaYetuOnlineTV
 
7 July 2020
Mbeya, Tanzania

Chalamila Aeleza Hoja Nzito za Kubaki Mbeya



Albert Chalamila mkuu wa mkoa wa Mbeya akiri kuwa alikuwa na mawazo ya kugombea ubunge siku za nyuma.

Ila kutokana na methali asiyesikia la mkuu huvunjika guu mwisho wa nukuu. Hivyo kwa kuwa kuna mambo mengi ya kuyafanya mkoani Mbeya anadhani aendelee kuchapa kazi badala ya kukimbilia kugombea nafasi ya kisiasa ya ubunge.

Mfano kuna kazi kubwa kusimamia ujenzi ktk sekta ya afya kama hospitali ya Rufaa mkoani Mbeya na vituo vya afya 19, sekta ya elimu pia inatakiwa kufanyiwa kazi mfano Rungwe sekondari, barabara kuelekea Busekelo , Airport ya Songwe kuendelezwa kuweka miundombinu ili ndege ziweze kuruka usiku... mradi wa REA unaofanywa na mkandarasi toka Tunisia kusambaza umeme vijijini...

Hivyo kila mtu ktk utumishi wa serikali akitimka kwenda kugombea nafasi za kisiasa kupitia chaguzi mambo yatakwama ya maendeleo......

Source : millard ayo

Sababu kubwa ni udikteta wa jiwe basi.
 
7 July 2020
Mbeya, Tanzania

Chalamila Aeleza Hoja Nzito za Kubaki Mbeya



Albert Chalamila mkuu wa mkoa wa Mbeya akiri kuwa alikuwa na mawazo ya kugombea ubunge siku za nyuma.

Ila kutokana na methali asiyesikia la mkuu huvunjika guu mwisho wa nukuu. Hivyo kwa kuwa kuna mambo mengi ya kuyafanya mkoani Mbeya anadhani aendelee kuchapa kazi badala ya kukimbilia kugombea nafasi ya kisiasa ya ubunge.

Mfano kuna kazi kubwa kusimamia ujenzi ktk sekta ya afya kama hospitali ya Rufaa mkoani Mbeya na vituo vya afya 19, sekta ya elimu pia inatakiwa kufanyiwa kazi mfano Rungwe sekondari, barabara kuelekea Busekelo , Airport ya Songwe kuendelezwa kuweka miundombinu ili ndege ziweze kuruka usiku... mradi wa REA unaofanywa na mkandarasi toka Tunisia kusambaza umeme vijijini...

Hivyo kila mtu ktk utumishi wa serikali akitimka kwenda kugombea nafasi za kisiasa kupitia chaguzi mambo yatakwama ya maendeleo......

Source : millard ayo

Kubabeki...

Biti noma.
 
Back
Top Bottom