katiba

  1. S

    JamiiForums Tanzania Hivi ile peremende ya maridhiano na upatikanaji wa katiba mpya bado ipo vinywani mwa wapinzani ama imeyuyuka??

    Huyu rais Samia anapaswa kuangaliwa kwa jicho la tatu. Anajua kucheza na akili za watanzania kweli kweli. Kabla ya kumleta mwarabu alianza kwa kuwaweka sawa wabunge (kama alivyotujuza mbunge wa CDM Aida Kenan). Aliwapeleka Dubai kwa ziara ya "mafunzo". Wakala bata na kupewa cha mfukoni. Suala...
  2. GoldDhahabu

    JamiiForums Tanzania Naitamani "katiba dikteta" kiasi kwamba hata Amiri Jeshi Mkuu hawezi wala kuthubutu kuikanyaga

    Udikteta si mzuri. Lakini demokrasia inayotokana na katiba lege lege nayo ni hatari. Kwa kawaida, dikteta hapingwi kirahisi nchini mwake. Ni ama watu wake wampende, hata kama ni kwa unafiki, au kumwogopa kwa ajili ya usalama wao. Madikteta hawakubali kudharauliwa. Imeshatokea mara nyingi, hasa...
  3. H

    JamiiForums Tanzania Possi: Dubai ina uwezo wa kuingia mikataba imekasimiwa kwa mujibu wa Article 120 – 123, ya katiba ya Umoja wa Jumuia za Falme za Kiarabu

    Utangulizi: Ni ukweli usiopingika kuwa kulingana na unyeti wa rasilimali bandari kwa taifa na ukizingatia kuwa ni lango kuu la uchumi, na maswala ya ulinzi na usalama. Na zaidi sana kuwa mchakato wa kuridhia mkataba wa aidha kuuzwa (opion ya wapingaji) au kupangishwa (opinion ya wa wasiopinga)...
  4. Pascal Mayalla

    JamiiForums Tanzania Kwa la Bandari, Pongezi TLS. Katiba yetu imenajisiwa. Bunge limetunga Sheria batili. Haki za Watanzania zimeporwa. Kwanini TLS wamenyamaza kimya?

    Wanabodi, Nikiwa ni mwanachama wa TLS, nimeisoma taarifa ya TLS kuhusu issue ya Bandari na DPW, kiukweli kabisa TLS inastahili pongezi za dhati!, imefunga huu mjadala, ingekuwa mimi ni Mnyamwezi, Kinyamwezi hii inaitwa "funga kalomo", yaani funga mdomo!. Taarifa hii ya TLS ni funga kazi, na...
  5. T

    JamiiForums Tanzania Kutopandisha walimu madaraja kwa kuwa na mashauri ya kinidhamu ni kukiuka katiba ya Nchi, Ibara ya 13: 6(b)

    Baadhi ya walimu waliositahili kupanda madaraja ya kiutumishi 2023 hawajapandishwa vyeo vyao kwa sababu mbalimbali. Baadhi ya sababu ni walioko masomoni, walio likizo bila malipo na walio mashtaka katika kamati za kinidhamu katika wilaya mbalimbali kwa makosa mabalimbali. Kutompandisha mwalimu...
  6. Pascal Mayalla

    JamiiForums Tanzania Watanzania ni Watu wa ajabu. Wanapigiaje kelele jambo dogo la Bandari, lakini Mambo Muhimu ya Msingi kama Katiba na Uhuru wao wapo Kimya?

    Wanabodi Nipashe la leo, Kama kawaida yangu kila Jumapili, huwaletea makala zangu za Kwa Maslahi ya Taifa, kuzungumzia jambo lolote la kisiasa, kiuchumi na kijamii lenye maslahi kwa taifa. Mada hizi huwa zina, swali , na hoja, kisha jibu, utalitoa wewe msomaji mwenywe. Swali la leo ni kutuhusu...
  7. Mwande na Mndewa

    JamiiForums Tanzania Mwambieni Zitto IGA ni sawa na Katiba ya nchi na HGA ni sawa na sheria ya nchi. Sasa ipi inamtegemea mwenzie?

    Zitto anasema IGA ni sawa na karatasi ya kufungia vitumbua, je anajua uzito wa IGA? Kwamsiojua Intergovernmental Agreement tunaweza kuitafsiri kwamfano kwenye NCHI tungeita ni KATIBA YA NCHI. Kisha Host Gorvanment Agreement au Mikataba ya Utekelezaji, tunaweza kuitafsiri kwamfano kwenye NCHI...
  8. T

    JamiiForums Tanzania Sasa tunaitaka Katiba iwe kwa mchana na ama usiku!

    Tunaitaka katiba itakayoondoa ukiritimba na udikiteta wa viongozi Tunaitaka katiba ambayo itakuwa ni ya wananchi na siyo kuwa ya viongozi Tunataka katiba itakayoondoa udikiteta wa viongozi kupola mali zetu kwa kutumia mamlaka yao Tunataka katiba itayowapa wananchi mamlaka ya kuwawajibisha...
  9. T

    JamiiForums Tanzania Maswali yatokanayo na katiba! Mambo yasiyo ya muungano huwa ya muungano katika kipindi gani? Au ni ubovu wa katiba?

    Wasalaam Mara nyingi huwa nasikia huko Bungeni na kwa wanasiasa mbalimbali kwamba, Muungano wetu ni wa kipekee, umezifanya nchi hizi mbili kuwa na mambo ambayo hayawezi kuingiliana na yale ambayo yanayoingiliana Kuna yale yanakuwa ya Zanzibari pekee na yale yanakuwa ya Watanganyika pekee...
  10. Dr Matola PhD

    JamiiForums Tanzania Napinga mchakato wa kupata katiba mpya kabla ya uchaguzi wa 2025, Watanzania tukatae maigizo ya wanasiasa. Imetosha

    Bila kutumia Maneno mengi wote tunajuwa mabilioni ya pesa za walipa kodi yalivyohujumiwa na wanaccm kukwamisha katiba pendekezwa ya tume ya Warioba. Sasa kuna wanasiasa wanadhani tumesahau au sisi ni wajinga, eti wanataka katiba mpya kabla ya uchaguzi wa 2025 halafu bunge hili la DP ndio...
  11. Ileje

    JamiiForums Tanzania Bajeti ya mchakato wa katiba mpya iko wapi?

    Nimefuatilia hotuba yako ya bajeti ya 2023/24 lakini sikumbuki kusikia bajeti kwa ajili ya mchakato wa katiba mpya, je mchakato huo utafanyika kwa kutumia kifungu gani cha fedha? Wananchi wanasubiri kwa hamu kubwa kuanza kwa mchakato huo ili hatimaye tupate katiba ya wananchi.
  12. Mayor Quimby

    JamiiForums Tanzania Katiba ya Samia

    Katiba ya Warioba ilikwama kwa sababu mbili; Moja: Masharti ambayo utekelezaji yanahitaji mapato mengine. Pili: Masharti ya muungano ambayo CCM isiyoweza vumilia isipokuwa kwenye kuvunja muungano tu. Katiba ya Samia: Wala usipoteze muda wako; yote ya awali ndio yale yale. Ziada ni yeye...
  13. Mag3

    JamiiForums Tanzania Danadana ya kupatikana Katiba mpya lengo ni kuhalalisha mikataba mibovu

    Baada ya Bunge la CCM kupitisha azimio la kuunga mkono mkataba wa Tanzania na DP World ya Dubai hakuna tena shaka kuwa adui wa taifa hili ni CCM. Kumbe ile dana dana iliyokuwa ikipigwa kuchelewesha upatikanaji wa Katiba Mpya, ilikuwa kuwezesha Tanzania kuingia laini katiba mikataba ya aina...
  14. JF Member

    JamiiForums Tanzania Serikali Tatu ni mhimu. Katiba ya Warioba iendelee

    Salam zangu ziwafikie Kabudi, Warioba na Polepole. Sasa nawaelewa rasmi kwamba maoni ya wananchi yalikuwa sahihi. Muundo wa Serikali tatu Sasa unaanza kuonekana ni mhimu ukawepo. Serikali Moja na hii ya Sasa zinamapungufu mengi.
  15. President of China

    JamiiForums Tanzania Maswali ya mdau katika forum ya Katiba ya Watu kuhusu mikataba na mabadiliko ya Katiba katika mchakato wa kisiasa na kisheria

    Swali la kwanza Ni aina gani za mikataba ambayo inaweza kusababisha upungufu wa uhuru wa kitaifa? Majibu tota kwa mdau @G na wadau wengine Swali la kwanza. Kuna aina mbalimbali za mikataba ambazo zinaweza kusababisha upungufu wa uhuru wa kitaifa ni kweli. Hapa kuna baadhi ya mifano: 1...
  16. R

    JamiiForums Tanzania Katiba Mpya inakuja kutusaidia nini kama tumeuza madini, gesi, mbuga, visiwa na bandari?

    Tumeuza visiwa, tukauza gesi, tukauza madini na sasa bandari; je, hii Katiba mpya inakuja kusimamia nini au kutusimamia tusipingane na wanunuzi? Tunaposema Katiba mpya huku tukiwa tunaingia mikataba ya kuuza rasilimali zetu, means Katiba haitasema jambo na ikisema jambo halitatekelezeka.
  17. Mpwayungu Village

    JamiiForums Tanzania Mwenye katiba ya CWT na Sheria ya vyama vya Wafanyakazi Naomba tafadhali

    Habari za mda huu ndugu zangu. Ombi langu ni moja. Nahitaji vitu viwili 1.KATIBA YA CWT 2.SHERIA YA VYAMA VYA WAFANYAKAZI Nitumie hapa hapa au PM
  18. PSPA Pure'12 udsm

    JamiiForums Tanzania Mchakato wa katiba mpya unapaswa kuanzia hatuza za awali.

    Sababu kubwa inayotolewa ya kwanini tunahitaji katiba mpya na si kufanya marekebisho kwenye katiba ya sasa, ni kwamba Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 haikushirikisha wananchi. Kama ni mapungufu yangefanyika marekebisho na kukidhi mahitaji ya sasa kama ambavyo Katiba ya...
  19. BARD AI

    JamiiForums Tanzania Dkt. Slaa: Katiba haipaswi kutungwa kwa maagizo ya Rais, kinachofanyika ni kiinimacho

    Wakati safari ya Watanzania kwenda kupata Katiba mpya ikiendelea, Balozi Willibrod Slaa ameukosoa mchakato huo, akisema kinachofanyika ni kiinimacho na hakina uhalali kisheria. Hoja ya mwanasiasa huyo aliyewahi kuwa katibu mkuu wa CHADEMA, inajengwa kwenye msingi kwamba “Katiba haipaswi...
  20. Librarian 105

    JamiiForums Tanzania Jaji Mutungi: ni kweli bila shaka katiba mpya haitatekwa na wanasiasa?!

    Alitoa kauli hiyo baada ya ofisi yake ya msajili wa vyama vya siasa kuelekea kukutana na baraza la vyama vya siasa nchini (bila ushiriki wa Chadema). Kujadili hatua za mwanzo za utekelezaji wa agizo la Rais la kuagiza kuanza kwa mchakato wa katiba mpya. Rais Samia alimtaka kuitisha mkutano...
Back
Top Bottom