Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limezua Mkutano wa Hadhara wa Mbunge wa Kibamba John Mnyika na Wananchi wake, Uliokuwa ufanyike leo Feb 8, 2020 kata ya Mbezi njee kidogo na Jiji la Dar es salaam.
Polisi wamedai kuwa eneo la stendi ya zamani ulipotakiwa kufanyika mkutano huo kuna...
Kikosi cha Jeshi cha Anga za Juu cha Marekani ambacho ni tawi jipya la Jeshi la Marekani kimefanya jaribio la kombora la balistiki la Minuteman III.
Kikosi hiki cha masuala ya kijeshi katika anga za juu kiko chini ya Jeshi la Anga la Marekani na kilianzishwa mnamo Desemba 20 mwaka jana, 2019...
Wakuu,
Unajua haya mambo ya Jeshi sijui inakuaje kama mtu ukifiwa. Juzi tumepata msiba wa Vijana wetu zaidi ya kumi walikuwa kwenye Mazoezi. Leo ndo tunaaga hapa Lugalo Dar, kwa anayetaka kushiriki mazishi aje.
Naamini Jeshi litatolea ufafanuzi taarifa hii ili kuondoa sintofahamu.
Baada ya...
Iran, Korea Kaskazini wamemudu kuwadhibiti wamarekani
Nashauri tuunde umoja wa kushirikiana katika mambo mbalimbali
Pia jeshi letu like mkao wa kula kumnyuka mmarekanj endapo ataendelea kushambulia viongozi wa serikali
Kwanza nianze kwa kukupongeza jinsi unavyotimiza wajibu wako wa kuliongoza taifa hili kwa ufanisi mkubwa na wa hali ya juu.
Wewe ni mtu muwazi, unayepokea maoni ila ni kiongozi shupavu asiyeyumbishwa.
Tumeona msimamo wako thabiti kwa mfano katika jitihada zako za kuhakikisha watoto wa kike...
Watu wawili wamethibitishwa kufa baada ya ndege ya jeshi la watu wa Uganda kuanguka katika mji wa Gomba. Kwa mujibu wa Msemaji wa Jeshi la Wananchi wa Uganda, Brigedia Brigedia Richard Karemire, amesema ndege ya jeshi AF 302 ilikuwa kwenye na watu hao kwenye mafunzo.
“Ilikuwa na watu wawili...
Naomba niweke wazi hapa nahitaji kueleweshwa juu ya hili suala. Katika hotuba yake Waziri wa mambo ya ndani alidokeza juu ya utawala ndani ya wizara ya Mambo ya ndani, akadai hana nyota na wala yeye si Amiri jeshi mkuu. (Hili nakubali asilimia mia). Hivyo ameonyesha wazi kuwa hatakuwa...
Nakupongeza kwa kuteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi. Kumbuka Wizara yako ndio Wizara inyohusika na kusimamia haki za msingi za maisha ya Watanzania ya kila siku. Pia ndio Wizara inayowajibika kusimamia usalama wa Wananchi na Mali zao.
Hivi karibuni kumekuwa na shutuma nyingi dhidi...
Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma Tungu Mgaya, anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Dodoma tangu jana kwa kutuhuma za kupiga na kusambaza picha inayoonesha shida ya maji chuoni hapo.
--+
MWANAFUNZI MUYAGA TUNGU ANAYEDHANIWA KUPIGA PICHA ZA KUONYESHA TATIZO LA MAJI UDOM MIKONONI MWA POLISI...
Dr. Osatohanmwen Osemwengie ni mtengenezaji wa drones za jeshi la marekani. Mtu huyu anayetoa huduma kwenye jeshi lenye nguvu zaidi duniani ni mzaliwa wa Edo State, Nigeria. Ana masters degrees 7 and PhD 3.
Vilevile anamiliki kampuni ya kutengeneza drones na ni muanzilishi wa the Open Robotics...
Natoa pongezi kwa RPC wa mkoa mjini magharibi unguja kwa kufanya kazi kwa weledi na kumfukuza kazi askari ambaye alimkamata mtuhumiwa na kumpeleka kwa wananchi wenye hasira na kisha kumuua mtuhumiwa.
Imekuwa ni tabia mbaya sana wananchi wamekuwa wanachukua sheria mkononi na kuua watuhumiwa bila...
Jeshi la Sudan linayashikilia makao makuu ya kikosi cha usalama wa taifa cha nchi hiyo ambacho awali kilikuwa kitiifu kwa rais aliyepinduliwa Omar al-Bashir, ripoti zinaeleza.
Mapambano yalianza Jumanne katika jiji la Khartoum ambapo milio ya milipuko ilisikika.
Kitengo hicho cha usalama wa...
Nilishangazwa mno na vitisho alivyotoa Rais Magufuli majuzi kwenye sherehe za mapinduzi kuwa wale wote wanaovishutumu vyombo vyetu vya ulinzi nchini, kwa kupotea watu mbalimbali, wakamatwe na walete ushahidi!
Hivi katika mazingira haya yanayotokea nchini chini ya utawala huu wa awamu ya tano wa...
Mkuu wa Jeshi la Niger, jenerali Ahmed Mohamed amefukuzwa kazi zikiwa zimepita siku tano tangu wanamgambo wa kigaidi kuwaua wanajeshi 89 walipovamia kambi ya jeshi la Niger, ikiwa ni idadi kubwa zaidi ya wanajeshi kuuawa kwa siku moja.
Mbali na jenerali Mohamed, viongozi wengine waandamizi...
Shirika la upelelezi nchini Marekani, FBI liliwakamata raia wawili wa China mwishoni mwa juma kwa kosa la kupiga picha kinyume cha sheria kambi ya Jeshi la majini la Marekani huko Florida.
Hili ni tukio la pili kufichuliwa na mamlaka hiyo, matukio ambayo yamekuwa yakitekelezwa na raia wa China...
Jeshi la Iran limesema kuwa limejipanga kutumia makombora ya masafa ya kati na ya mbali kuzishambulia kambi za kijeshi za Marekani zilizopo Mashariki ya Kati ikiwa ni mpango wa kulipa kisasi kutokana na mauaji ya jenerali wa kikosi maalum cha Iran, Qassem Suleiman aliyeuawa na Marekani wiki...
Wanajeshi wa Kenya Alhamisi wamewaua washukiwa wanne wa wapiganaji wa kikundi cha Al-Shabaab na kumkamata mmoja wao baada ya tukio la kushambuliwa basi katika Kaunti ya Lamu.
Mratibu wa Mkoa wa Pwani John Elungata ametoa ripoti hiyo masaa kadhaa baada ya shambulio la kushitukiza katika eneo la...
Jeshi la Polisi nchini kupitia kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), kwa kushirikiana na Government e-Payment Gateway (GePG), limeanzisha mfumo wa upatikanaji wa fomu ya upotevu (Police Loss Report), kupitia mtandao wa https://Lormis.tpf.go.tz na kufanya malipo kwa njia ya...
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Selemani Jafo amekerwa na utendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Mbinga vijiji kwa kuchelewa kukamilisha ujenzi wa kituo cha Afya Mapera.
Jafo ametoa siku 17 majengo yote ya kituo hicho yawe yamekamilika.
Kituo hicho kilipokea fedha mwezi Mei 2019 na...
Waasi wa kundi la ADF wameshambulia tena mji wa Beni katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, na kuuwa watu 22 katika eneo la Ndombi na Kamango.
Waasi hao wanaelezwa kuwashambulia wakaazi hao kwa risasi na kuwauawa wakiwemo wanawake na watoto huku wengine wakijeruhiwa hata hivyo jeshi la...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.