Mzukulu
JF-Expert Member
- Feb 14, 2020
- 1,401
- 2,631
Ilikuwa ni mida ya Saa 5 asubuhi kuelekea Saa 6 mchana ambapo Mzukulu nilikuwa napita zangu ndipo nikashikwa na butwaa hadi Masikitiko makubwa baada ya kuona Kijana (nadhani alikuwa nae ni Askari) akiwa amelazwa chini katika Geti la Kuingilia TPDF Golf Club huku amebebeshwa bonge la chuma na Kuambiwa alinyanyue juu huku anayemwambia hivyo akiwa anafagia zake taratibu Kuzunguka kile Kibanda cha Walinzi.
Sikatai na wala sipingani na utaratibu wa JWTZ (TPDF) katika kuwaadabisha kwa kuwapa Adhabu Maaskari (Wanajeshi) wao kwani najua ni kitu cha kawaida Kwao na kwa Majeshi mengi duniani ila kilichonisikitisha Mimi ni Mazingira husika ya tukio lenyewe ambapo kwa uelewa wangu (na hapa nakaribisha kukosolewa) nadhani halikuwa na uungwana na ni kama vile lilikuwa la kukomoa vile.
Kwanza Mhusika alikuwa akihenyeshwa hivyo Getini kabisa (tena Geti Kuu) la Kuingilia TPDF Golf Club halafu katika Kuonyesha kuwa mtoa hiyo adhabu alikuwa na lake jambo alikuwa kama akiona wanaopita nje (Raia) ni wanaume alikuwa anamwambia ainue lile chuma na atulie nalo tuli lakini akiona tu raia wanaopita nje ni akina dada basi Mtoa adhabu ndiyo alikuwa anapata Morali (Moto) wa kumuamrisha na kumuadabisha yule askari kiasi kwamba nilijisikia vibaya mno.
Hivi huyo mtoa adhabu alishindwa nini kumuadhibu yule Afande sehemu nyingine ambayo wangekuwa wao wawili tu au kule nyuma ambako watu huwa hawapiti ili aweze kumuhenyesha vizuri kuliko kuja kumhenyesha askari pale getini kabisa ambako kila mtu alikuwa akimuona (hasa Sisi Raia) akina Mzukulu kiasi kwamba nahisi yule afande mhenyeshwaji alijisikia vibaya sana?
Na sijui yule askari aliyekuwa akihenyeshwa vile alifanya nini masikini ya Mungu. Kweli cha moto askari kakiona na kakoma!
Sikatai na wala sipingani na utaratibu wa JWTZ (TPDF) katika kuwaadabisha kwa kuwapa Adhabu Maaskari (Wanajeshi) wao kwani najua ni kitu cha kawaida Kwao na kwa Majeshi mengi duniani ila kilichonisikitisha Mimi ni Mazingira husika ya tukio lenyewe ambapo kwa uelewa wangu (na hapa nakaribisha kukosolewa) nadhani halikuwa na uungwana na ni kama vile lilikuwa la kukomoa vile.
Kwanza Mhusika alikuwa akihenyeshwa hivyo Getini kabisa (tena Geti Kuu) la Kuingilia TPDF Golf Club halafu katika Kuonyesha kuwa mtoa hiyo adhabu alikuwa na lake jambo alikuwa kama akiona wanaopita nje (Raia) ni wanaume alikuwa anamwambia ainue lile chuma na atulie nalo tuli lakini akiona tu raia wanaopita nje ni akina dada basi Mtoa adhabu ndiyo alikuwa anapata Morali (Moto) wa kumuamrisha na kumuadabisha yule askari kiasi kwamba nilijisikia vibaya mno.
Hivi huyo mtoa adhabu alishindwa nini kumuadhibu yule Afande sehemu nyingine ambayo wangekuwa wao wawili tu au kule nyuma ambako watu huwa hawapiti ili aweze kumuhenyesha vizuri kuliko kuja kumhenyesha askari pale getini kabisa ambako kila mtu alikuwa akimuona (hasa Sisi Raia) akina Mzukulu kiasi kwamba nahisi yule afande mhenyeshwaji alijisikia vibaya sana?
Na sijui yule askari aliyekuwa akihenyeshwa vile alifanya nini masikini ya Mungu. Kweli cha moto askari kakiona na kakoma!