Kwa karibu mwaka mmoja, Hellen Rono, mkulima kutoka Kaunti ya Bomet magharibi mwa Kenya, amefanikiwa kuzuia ugonjwa wa mnyauko wa nyanya kwa kutumia teknolojia ya kupandikiza iliyoanzishwa kupitia ushirikiano wa kilimo kati ya China na Kenya, baada ya miaka mingi ya kuona mazao yake yakiharibika...