chadema

CHADEMA (Chama cha Demokrasia na Maendeleo)
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ni chama cha kiasiasa nchini Tanzania ambacho kilianzishwa tarehe 28 Mei 1992 na mwanasiasa mkongwe Edwin Mtei, aliyewahi kuwa Waziri wa Fedha katika miaka 1997 hadi 1979.

Mwaka 2000 CHADEMA hakikuwa na mgombea wa Urais. Mwaka 2005 mgombea wa CHADEMA Freeman Mbowe alikuwa namba tatu kati ya wagombea kumi akapata asilimia 5.88 za kura.

Mwaka 2010 CHADEMA ilipata asilimia 27.1% na mgombea Urais wa chama Wilbroad Peter Slaa na kura 4,627,923 kwa 31.75%.

Hata hivyo CHADEMA imekataa matokeo mengi kutokana na mchakato mzima kuwa mikononi mwa Tume ya Uchaguzi isiyo huru.
  1. kindikinyer leborosier

    CHADEMA kuweni makini, mnademka sana na ngoma za CCM

    Assalam wanajamvi! poleni na majukumu ya kila siku ya kujikwamua kisiasa, kiuchumi, na kiutamaduni! Niende moja kwa moja kwenye hoja, neno kudemka lilipata umaarufu miezi kadhaa likiwa na maana ya kucheza sana ngoma inayopigwa, ndugu zangu CHADEMA mnademka sana et sasa mpo huru sasa mnafanya...
  2. Erythrocyte

    Video: CHADEMA wafanya sherehe Mjini Morogoro

    Huu ndio uzuri wa Chama cha siasa kinachosimamia misingi ya haki, huwa mnajiachia tu kwa vile hakuna kulogana wala kinyongo. Hebu jionee mwenyewe.
  3. Lyetu

    Kampeni dhidi ya Diamond Platnumz: Wanaharakati kuweni serious kidogo

    Habari za wakati huu wakuu. Naomba kuzungumza nanyi mnaojiita wanaharakati pamoja na wafuasi wenu. Hiki kinachoondelea huko mitandaoni sio tamko rasmi la Chama kuwa sasa wameamua kufanya vile, ila ukimya wa viongozi juu ya hili jambo unanambia kuwa chama kimebariki. Mi naomba mnifafanulie...
  4. W

    CHADEMA in Limbo: Makundi, njaa, upendeleo vyatajwa kuwa chanzo cha sintofahamu

    Ndugu zangu, Wakati umefika sasa baadhi ya viongozi wamemweleza Mbowe aache kuhadaa makamanda "kukubaliana na njaa, kuendesha chama kwa hela zao" ilihali yeye anatumia rasilimali za chama kuaafiri, kujilipa posho nk. Kiongozi mmoja ambaye ni mwandamizi alisema "huwezi kuwaambia wenzako...
  5. Nigrastratatract nerve

    Ally Bananga: Nina kiapo na mke wangu, nitamlinda kwa gharama ya damu yangu

    "Mimi ni mwanachama wa CHADEMA, Suala la wabunge 19 wa viti maalumu ambao Chama chetu kinasema hakiwatambui, mke wangu (Hawa Bananga) pia ni miongoni mwao na katika vitu ambavyo nimekuwa nikijiepusha kuvizungumza ni suala hili kwasababu bado maamuzi yako ndani ya chama, Kuliweka hili kwa...
  6. fasiliteta

    Hivi kampeni ya CHADEMA kututoa line za Vodacom iliishiaga wapi?

    Jamaa wanaongozwaga na emotional mbaya sana. Kina Lema na viongozi wake walianzishaga hii kampeni, cha ajabu haijulikani iliishiaga wapi. CHADEMA kuna umber la viongozi sanaaaa,ni kama kichaka chaajizi, manyang'anyi,watu wa visasi, CHUKI, hilba na kukata Tamaaa Sanaa. CHADEMA wanahitaji...
  7. Riz king

    Yuko wapi Dkt. Vincent Mashinji?

    Huyu ndugu yetu kipindi cha jiwe alimkimbia Mbowe, akaelekea Kawe kuomba ridhaa ya CCM akapigwa chembe la kidevu na Gwajiboy. Baadaye jiwe sijui alikuwa na mpango gani nae, nikaona kampiga kimya. Sijamsikia huyu Dkt. wa binadamu au atakuwa kaamua kurudi kwenye tiba huko kulikojengwa mashine ya...
  8. Kamanda Asiyechoka

    Tabora: Freeman Mbowe kuongoza Oparesheni Haki Kanda ya Magharibi

    Maandalizi ya kikao cha Mkutano Mkuu wa Jimbo la Tabora Mjini yamekamilika, ambapo leo Juni 06, 2021 mwenyekiti wa Chadema Taifa Mhe. Freeman Mbowe ataongoza kikao hicho. Hii ikiwa ni mwendelezo wa Oparesheni Haki Kanda ya Magharibi.
  9. J

    Kwa mara ya kwanza nimejiunga Rasmi na Chama cha Siasa nchini

    Kuanzia leo tarehe 6-6-2021, kupitia CHADEMA Digital App, nimefanikiwa kwa mara ya kwanza kuwa mwanachama wa chama Cha siasa hapa nchini kwetu Tanzania. Mwaka jana, 2021 ilikaribia kidogo niwe mwanachama wa CCM, lakini kwa muda wa miezi isiyopungua mitatu, hakukuwa na kadi mahala nilipo. Sasa...
  10. Mmawia

    Asante sana Mbowe, umeibeba CHADEMA hadi sasa imekua. Kapumzike

    Mwenyekiti wa CHADEMA na gwiji wa siasa za kistaarabu barani Afrika, mheshimiwa Mbowe ametangaza kustaafu. Mh Mbowe ameweka wazi kusudio lake pale ifikapo mwaka 2023 atastaafu nafasi ya uwenyekiti wa chama na kumkabidhi kijiti mwana CHADEMA mwenye uwezo. Kama Taifa tumepokea maamuzi yake kama...
  11. J

    Mchungaji Msigwa apendekezwa kumrithi Mbowe nafasi ya mwenyekiti CHADEMA 2023 atakapostaafu!

    Wanachama wa CHADEMA mkoani Iringa wamependekeza mchungaji Msigwa agombee uenyekiti wa CHADEMA 2023. Joseph Kibiki anasema CHADEMA Iringa na kanda ya Nyasa kwa ujumla watafanya kila linalowezekana kuhakikisha mchungaji Msigwa anakuwa nahodha wa CHADEMA baada ya mh Mbowe kustaafu kwa mafanikio...
  12. Ileje

    Freeman Mbowe kung'atuka uongozi wa CHADEMA mwaka 2023

    Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe ametangaza kuachia uongozi wa chama mwaka 2023 Pia, amewataka viongozi wa chama hicho Kanda ya Magharibi kutodumazwa na changamoto zilizojitokeza katika uchaguzi uliopita bali wajipange upya kudai na kusimamia haki
  13. MamaSamia2025

    CHADEMA na Wanaharakati kuonesha chuki dhidi ya Diamond ni ukosefu wa ajenda

    CHADEMA NA WANAHARAKATI KUONYESHA CHUKI DHIDI YA DIAMOND NI UKOSEFU WA AGENDA Natumaini mko wazima. Kwa wiki hii mitandaoni kumetokea vituko vya wanaharakati pamoja na baadhi ya viongozi wa CHADEMA kuongoza kampeni ya kuhakikisha mwanamuziki komredi Diamond Platnumz hashindi kwenye tuzo za BET...
  14. J

    Sera ya CHADEMA inasemaje kuhusu Wasanii hususani wa muziki wa kizazi kipya?

    Nafahamu sera ya CCM inahimiza kuwalea wasanii katika tasnia zote ili waweze kufikia viwango na mafanikio ya kimataifa. Ndio maana unawaona akina Samatta, Msuva, Diamond nk nk wakitoboa. Sera za Chadema sijajua zinasemaje. Mwenye nazo atujuze Tafadhali. Nawatakia Sabato yenye baraka!
  15. Erythrocyte

    CHADEMA kuitisha Baraza Kuu mwezi Julai, suala la Wabunge 19 wa Viti Maalum kumalizwa rasmi

    Hii ndio Taarifa ya Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe au waweza kumuita Mtemi Isike aliyoitoa kwa waandishi wa habari, alipokuwa kanda ya Magharibi katika ziara yake ya Operesheni Haki. Amesema baada ya vikao vya Baraza Kuu ratiba ya Mikutano ya hadhara nchi nzima itapangwa.
  16. W

    Bananga kumpigia kura Diamond

    Wakuu, Duniani kuna watu na viatu, Bananga aamua kuwa mtu. ===== Nadeclare interest Mimi ni mshabiki wa diamondplatnumz Nitapiga kura Nitaomba kura kwa ajili yake Kwangu mm michezo, muziki na starehe hazina itikadi. Huwa nachagua vita vya kupigana Vita ndogo ina gharama kubwa kama hupigani...
  17. Mindi

    Hivi tuseme ukweli, kati ya CCM na CHADEMA ni nani hasa chama imara cha siasa?

    CCM pamoja na historia ndefu ya kutokea TANU, Pamoja na kwamba ipo madarakani miongo kadhaa, haijui maisha nje ya utawala, bado ni chama dhaifu sana kiasi kwamba hakiwezi kusimama chenyewe bila kubebwa na baiskeli ya wagonjwa ya Polisi, msukumaji usalama wa taifa. Haiwezi kufanya chochote bila...
  18. kipara kipya

    CHADEMA operesheni zenu ni maigizo ya mafanikio ni Sangara tu

    Ukweli unauma lakini ni lazima muelezwe ili mjitathimini na muda mnaoupoteza katika hiyo misafara yenu ya kufuja pesa za wananchi maskini mnaowalazimisha kuwachangia mafuta. Lazima mkubali operesheni yenu iliyokuwa na malengo na ikafanikiwa na ikavuna wanachama ni moja tu ile operesheni...
  19. Idugunde

    TAKUKURU tupeni mrejesho wa kesi zote mlizokuwa mnashughulikia

    Kwanza kabisa mtambue kuwa mnatumia kodi za Watanzania kufanya shughuli zenu. Kwa hiyo kufanya maigizo yasiyo na kichwa wala miguu sio jambo jema. Sakata la Mbowe kujilipa bil 8 liliwekwa wazi na wanachama waliokuwa wanakatwa hizo pesa na mpaka leo mliishia maigizo ya kuhoji wanachama bila...
  20. Jumbe Brown

    CHADEMA na kutochukua tahadhari ya Corona katika mikutano yake

    Wameendelea kutovaa barakoa. Ni CHADEMA hawahawa walioishinikiza serikali ya awamu ya 5 itoe takwimu za kila siku za wagonjwa wa UVIKO-19. Ni CHADEMA hawahawa walioupinga msimamo wa jemedari Hayati Dkt. Magufuli juu ya kutowekwa lockdown nchi nzima/maeneo yenye msongamano. Kipi kilitarajiwa...
Back
Top Bottom