1. Amani pasipo haki, Ni wapi umeiona?,
Kwa hadithi sikumbuki, Ajabu'li kuliona,
Walo juu mishikaki, wa chini hakuna dona,
Haki Ikikosekana, Amani I Mashakani
2. Wanahubiri Usawa, wanaiba wakigawa,
Mifumo imepagawa, Dhoofu yataka dawa,
Wamewajaza machawa, waimbe nchi I Sawa,
Haki Ikikosekana...