JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

On JF:

Mdau wa JamiiForums ametoa hoja yake kuwa watu wanaokula dagaa hupata faida kubwa zaidi kuliko wale wanaokula samaki wakubwa. Amedai kuwa tofauti na samaki wakubwa, mtu anayekula dagaa anakula hadi mifupa yake yenye madini mengi ya calcium hivyo kuwafanya wawe na mifupa imara kuliko alaye samaki wakubwa, hasa kwa watoto ambao wanakua. Amewashauri watu kutumia dagaa kwa wingi, ikiwezekana wawepo kwenye kila mlo. Madai haya ni sahihi?
Mdau mmoja wa JamiiForums ameelezea kuwa watu wanaokunywa pombe kupita kiasi (Ulevi uliopindukia) wakiacha ghafla matumizi ya pombe wanaweza kufa. Mdau huyu anaeleza kuwa pombe hupunguza utendaji wa akili kama yalivyo madawa mengine ya kulevya, pia huleta uraibu na utegemezi. Amewashauri walevi sugu kuacha pombe taratibu ili wasipatwe na athari kubwa kwenye afya, ikiwemo kifo kutokana na kifafa. Madai haya ni sahihi?
Zipo taarifa zinadai kuwa Jeshi la Tanzania katika wilaya ya Nangade, Cabo Delgado waliingia kwenye mtego wa Magaidi katika kijiji cha Vondanhar, eneo la Palma. Aidha inadaiwa Jeshi la Tanzania lilikuwa likisafiri kwa magari ya kivita sambamba na jeshi la Msumbiji. Magari matatu ya jeshi la Tanzania yamechomwa moto na baadhi ya Silaha kuharibiwa. Taarifa iliyotolewa na kikundi cha Kigaidi cha IS, imedai wamekamata baadhi ya Silaha ikiwemo Chinese Type 81-1 assault rifle pamoja na 12.7x108mm Type 54 HMG ya kwenye gari. Zaidi inaelezwa kuwa haya ni magari ya JWTZ yapo chini ya himaya ya magaidi.
Upungufu wa nguvu za kiume ni tatizo linalokabili wanaume wengi duniani. Kwa mujibu wa tafiti, tatizo hili linazidi kuwa kubwa miaka ya hivi karibuni tofauti na zamani. Katika kutafuta visababishi vyake, Mdau mmoja wa JamiiForums aliweka chapisho lake lenye utafiti unaotaja sigara kuwa miongoni mwa mambo yanayofanya tatizo hili litokee. Ni kweli kuwa sigara inaweza kusababisha tatizo la upungufu wa nguvu za kiume?
Miaka ya 2000s imekumba na mabadiliko mengi ya kiteknolojia ikiwemo uwepo wa safaru za kidigitali ambazo haiziwezi kudhibitiwa na mamlaka za serikali (Benki Kuu). Sarafu za kidigitali zinazotambulika hadi sasa ni pamoja na BitCoins na OneCoin. Sarafu nyingine ya Islamic Coin (ISLM) imeibuka. Hivi karibuni kumeibuka madai kuwa sarafu hiyo imetambuliwa na Fatwa kuwa ni halali kutumika na waislam.
Kumekuwepo na picha inayozunguka mitandaoni ikimuonesha mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe akizungumza na Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho huku mandhari ya nyuma ya picha hiyo yakiwa na picha yenye chupa ya konyagi. Picha inayodaiwa kuwa na chupa ya Konyagi Ukweli wa picha hii upoje? Picha 1 kati ya 4 zilizowekwa na Tundu Lissu kwenye mtandao wa Twitter
Kuna Taarifa zilizosambaa kwenye Mitandao ya Kijamii, zinazodai Tarehe 31 Januari 2023 wakati Tundu Lissu akifanya Mahojiano ya channel ya YouTube ya Jambo TV, kwamba alimpongeza Rais Samia kwa kuunda Tume mpya ya Kuchunguza Haki Jinai. Taarifa hizo ni Uzushi. Uzushi huo ulidai kuwa Tundu Antipas Lissu alisifia kuundwa kwa Tume ya Haki Jinai, hata hivyo, kwa mujibu wa video iliyorekodiwa wakati wa mahojiano hayo Lissu hakupongeza kuundwa kwa tume ya haki jinai wala hakuzungumzia kundwa kwa tume ya haki jinai bali alizungumzia mfumo wa haki jinai kwa kukosoa mfumo huo. Tarehe 31 Januari 2023 Rais Samia alizindua Tume ya Kuangalia Jinsi ya Kuimarisha Taasisi za Haki Jinai. Rais Samia alisema Tume hiyo imeundwa kutokana na kuvurugika...
Kipindi cha afya hai ya uzazi wa mwanamke hutawaliwa na mizunguko ya hedhi ya kila mwezi ambayo hukoma baada ya kupata ujauzito, muda mchache baada ya kujifungua na pia baaada ya kufikia umri wa ukomo wa hedhi. Kwa maana rahisi, mwanamke hawezi kupata ujauzito ikiwa hapati hedhi. Hata hivyo, tumesikia mara kadhaa baadhi ya wanawake wakitoa madai kuwa wamepata ujauzito muda mfupi tu baada ya kujifungua, kabla hata hedhi yao ya kwanza haijarudi. Madai haya yana ukweli kiasi gani?
Back
Top Bottom