Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA

Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA

Chama ni watu na Zitto ni miongoni mwa wanaokijenga Chama Cha Demokrasia na Maendeleo- Kusema anautaka urais hakibomoi chama. Mwentekiti na Katibu na Baraaza la Wazee watakuwepo kukikuza chama Zitto ataongoza Nchi kupitia CHADEMa tatizo liko wapi? Au kuna mtu mmesha muandaa kugombea urais 2015? The early the better tukuze emokrasia ndani ya chama. wajitokeze wanaotaka watangaze nia, tuwachuje mapema kama walikuwa na madhambi wapiga kura tujue. Mnaogopa chama kitasambaratika, hamjakomaa kupambana na misukosuko ya kisiasa? Lazima tutofautiane mawazo, fikra, mitazamo na hisia mwisho wa siku tukubaliane kukubaliana. MAMBO YA ZIDUMU FIKRA SAHIHI ZA MWENYEKITI HATUZITAKI.

Mkuu kama ulikuwa hujui fahamu sasa kwamba CDM inaye mgombea 2015.Ni shujaa na mpigania haki za wanyonge Dr Wilbrod Slaa.
 
Zitto kaona isiwe taabu maana ilikuwa too much sasa wengine wakawa wanampa sifa za kumsanifu hadi wana CCM wakajiunga ikawa kama kum kejeri vile, lengo kumchonganisha na viongozi wakuu. Eti uongozi wa juu haufai ni Zitto tu anaweza kuwa mwenyekiti. Zitto kaliona hilo vibaraka wameachwa peupe wamebaki kulalamika pembeni labda waje na singo nyingine.

Ni kweli mkuu.Hili kundi la vibaraka na wachonganishi lilianzisha mtandao wao usio rasmi hapa JF.Kila post kumkashifu Mbowe na Slaa na hapohapo kujifanya wafuasi watiifu wa Zitto.Logically tu hapo walikuwa wanammaliza Zitto kisiasa.
 
Unalalamika post ndefu eeh...acha kusoma vichwa vya habari na magazeti ya udaku.Ndiyo maana wamewagundua wakaamua kuwatumia tu kuchafua watu hovyo hovyo.Ninyi mnakubali tu

Infact,your posts are laden with so much bigotry that it rarely makes sense for those who do not live in your mind there. only sycophants will support your malicious and scandalous post that can never make impact in the general view anyways.

You are worth to be ignored for now.....! endeleeni kumfanyia Ben monitoring!
Unaonesha uko so desperate, sawa na mtu aliyekata tamaa kwa kukosa kitu alichotumaini. Pole sana.
 
Kuutaka urais si dhambi na hakusema yeye ndiye anayefaa kuliko yeyote ndani ya chama chake, alichosema ni kwamba katiba iliyoko inawanyima fursa vijana kugombea urais na kama fursa hiyoingekuwepo naye angejitosa kuuwania. Kwa hiyo silioni kosa hapo. Nature ya binadamu ni progressive yaani ni endelevu kwa hiyo si vibaya na kuwa na malengo ya baadae. Baada ya kumpima sawasawa kijana huyu imegundua ni makini kwelikweli na yuko commited na chama chake kulikowatu wanavyofikiria. Ni mkweli, jasiri na mvumilivu na ni hazina tosha ndani ya chama chake, chama cha ukombozi mpya wa Tanzania - CHADEMA.

Kwa hiyo kwa nini nature ya Zitto kama binadamu iwe "progressive" aka "endelevu" kuutaka Urais lakini sio kugombea uongozi ndani ya chama? Au ndio ameona kwenye chama hakuna progression yoyote ya uongozi?
 
Uchaguzi wa ndani CHADEMA 2012

Wakiwafuata watu wakawashawishi kwamba wao ni wafuasi wa Zitto wakataeni kwani sina wafuasi isipokuwa waumini wa Katiba, Kanuni, Taratibu na utamaduni wa chama. Wakiwafuata watu wakawarubuni mumkatae Zitto kwa matakwa na chuki zao binafsi wakataeni pia. Msiwe wafuasi wa watu bali muwe wafuasi wa Chama kwani watu tutapita lakini chama kitadumu.

Tunataka kujenga cha...ma imara chenye demokrasia na kinachotoa fursa kwa kila mwanachama bila kujali mkoa atokao, dini aaminiyo au rangi ya ngozi yake.

Tunataka utii kwa chama na sio utii kwa watu binafsi.

2012 timu nzima ya CHADEMA ndani na nje ya Bunge iwe kitu kimoja. Tusaidiane, tusishindane. Tuinuane, tusiangushane. Tuambiane, tusisemane. Majungu huua umoja. Kuambiana ni kuimarishana. Daima mbele Nkrumah alisema. 'hakunaga timu mahiri kama sisi'



ZKZ.jpg


ZZK.jpg
 
Nafikiri huu uamuzi utaongeza mshikamano ndani ya chama. hongera kamanda kwa kuwa muwazi.
 
Kasoma alama za nyakati kajifunza kwa kakaye shibuda mambo ya kuropoka ropoka yamemgharimu na chama kipo juu kina naelekea ikulu. Kafulila kafulia vibaya na njama za kumpindua chairman, hakuna rafiki labda magamba.
 
Kamanda Zitto hongera kwa ujumbe wako ila inabidi na ww ujirekebishe mienendo yako ya kuwa na kauli tata kama za huko nyuma pia jitahidi safar hii uwe na teamwork na sio kushinda na magamba manafiki kama jmakamba na lile limbunge la kigoma mjini ambao hutumia daraja la ukijana kuhadaa wananchi, pia Zitto hakikisha misimamo yako iliyotofautiana na chama chako unaitolea huko huko chumbani kwako au bafuni ukiwa unaoga kuliko kuitoa hadharani na kuwapa magazet ya magamba haedlines.
Ni hayo tu.
 
ZZK ni mtu makini sana, anajua fika kwamba nafasi pekee anayoihitaji ni uenyekiti wa chama, na kwa kutumia makundi hasimu ndani ya chama inngemuwia vigumu sana kupata nafasi hii, pia anaelewa kabisa kugombea uongozi chadema ni kujitangazia uadui maana nafasi za uongozi zina hati miliki.

NI uamuzi wa busara sana, lakini hautokani na ZZK kutopenda uongozi isipokuwa kuelewa kitakachomtokea.
 
Kasoma alama za nyakati kajifunza kwa kakaye shibuda mambo ya kuropoka ropoka yamemgharimu na chama kipo juu kina naelekea ikulu. Kafulila kafulia vibaya na njama za kumpindua chairman, hakuna rafiki labda magamba.

mkuu zito ni jembe kali sana ila tatizo ana siasa za kigiriki ila na imani hatorudia tena kuleta kauli tata zake.
LONG LIVE KABWE ZITTO NA YESU KRISTO AKULINDE.
 
Kamanda Zitto hongera kwa ujumbe wako ila inabidi na ww ujirekebishe mienendo yako ya kuwa na kauli tata kama za huko nyuma pia jitahidi safar hii uwe na teamwork na sio kushinda na magamba manafiki kama jmakamba na lile limbunge la kigoma mjini ambao hutumia daraja la ukijana kuhadaa wananchi, pia Zitto hakikisha misimamo yako iliyotofautiana na chama chako unaitolea huko huko chumbani kwako au bafuni ukiwa unaoga kuliko kuitoa hadharani na kuwapa magazet ya magamba haedlines.
Ni hayo tu.

Well said mkuu zito na ujanja wake wote na akili anazosisiwa anazo hili halikua hajaliona kwani yeye ametoka ukoo wa kitawalaa????mwache ajifanye na urafiki na wanafiki atajiju akipotea wenzake wanapeta wanatumwa wale halijui hilo lol
 
Zitto nimtu makini isipokuwa anakatamaa ka mambo makubwa sana. Aliamini yeye anaweza kuwa raisi. Kutoa ile kauliyake ya kugombea urais ilikuwa ni kupima upepo ndiyo maana akaitoa mapema vile. Ameshajua kuwa urais anaweza kupewa ila muda wake haujafika.
 
Mimi ni nampenda sana zito nataka nikuone ukiendelea na ukali bungeni kama kawaida yako. Usilegeze kamba, najua msimamo wako ni mzuri sana maneno yako hapo juu ni maneno ya MPIGANAJI WA KWELI. Wana cdm msikilizeni ZITTO.
 
Kasoma alama za nyakati kajifunza kwa kakaye shibuda mambo ya kuropoka ropoka yamemgharimu na chama kipo juu kina naelekea ikulu. Kafulila kafulia vibaya na njama za kumpindua chairman, hakuna rafiki labda magamba.


Wenyewe wakikusikia watakumaindi kishenzi
 
Kukitumikia chama si lazima uwe kiongozi. Zitto ana PhD kwa hili
 
ZZK ni mtu makini sana, anajua fika kwamba nafasi pekee anayoihitaji ni uenyekiti wa chama, na kwa kutumia makundi hasimu ndani ya chama inngemuwia vigumu sana kupata nafasi hii, pia anaelewa kabisa kugombea uongozi chadema ni kujitangazia uadui maana nafasi za uongozi zina hati miliki.

NI uamuzi wa busara sana, lakini hautokani na ZZK kutopenda uongozi isipokuwa kuelewa kitakachomtokea.



Duh Kaka naona umeamua kupiga kombora katikati ya Jeraha
 
Kwanini hagombei cheo chochote ndani ya chama?
 
Back
Top Bottom