BAHATI ZURI CHADEMA Hakina Jeshi Binafsi, Genge la Ki-Gaidi cha Green Guard Cha Kuweza kutumia Kuua Mtu na Serikali Isijua Hadi Leo Hii
Napenda niamini kwamba huyu mwenzetu Zitto anazipata maoni hizi tunazozitoa humu.
CHADEMA haina jeshi, taasisi yake binafsi ya kijasusi wala vijana waliopewa mafunzo ya ki-gaidi (The CCM Green Guard) wa kuweza kumua hata INZI tu na serikali isijue mpaka leo hii.
Wananchi wa sasa nchini Tanzania si wa miaka ile, wanajua ukweli kuhusu vifo mbali mbali vilivyotekelezwa kimya kimya gizani na hata kwamba ni nani hasa aliyefanya nini, wapi na muda gani lakini uamuzi umekua ni wa kukaa kimya.
Lakini tangu UFISADI uiteke CCM taifa linaendelea kwa kasi kubwa mno kupoteza watu wake kwa mtindo huu huu ikiwa ni furaha kwa mafisadi. Wazee hutuambia kwamba enzi za Mwalimu Nyerere TISS kutumika kuchukua uhai wa watu wake ilikua ni jambo ambalo halipo.
Lakini leo ukiona watu wanavyopuputishwa gizani na wauwaji kurudi kukaa na sisi kama waungwana vile, wananchi tunawasanifu tu. Wasomi mbali mbali na hata Maprofesa waliosomeshwa kwa gharama kubwa ukiona wanavyoondolewa mithili ya inzi mtu unabaki unajiuliza kama taifa tunakwenda wapi hasa.
Hata hivyo mpaka sasa mauaji ya kijanja janja yakitokea tena, either in private or public, na wananchi tukapata japo hata fununu tu, basi MAFISADI na ndugu zenu wote patakua patamu.
Licha ya madhambi ya Zitto ambazo CHADEMA kwa busara wa hali ya juu wameshaumaliza kwa kuridhika kwa Umma wa Tanzania bila ya maswali zaidi, maadam kapeleka ripoti yake rasmi polisi na Manumba naye kakiri hivyo basi tangu sasa ni jukumu la vyombo hivyo hivyo kumlinda masaa ishirini na nne kwa kuwa kadai maisha yake yako hatarini.
Isitoshe, tangu Mbunge apigwe na kudhalilishwa kule Arusha, ni vema Ofisi ya Mhe Spika wa Bunge letu Mamaakinda kwa kushirikiana na Mhe Celina Kombani wakapeleka muswada mpya bungeni ya kuwapa wabunge wote, wakuu wa mashirika ya umma na taasisi zetu nyeti kitaifa na viongozi wa taifa wa vyama mbali mbali ULINZI WA KUTOSHA KABISA WA MUDA WOTE ili taifa tuondokane na mashaka mashaka na hata walipa kodi kubebeshwa gharama za ghafla za kurudia chaguzi zinazotokana na vifo vinavyozuilika kabisa. Hatua hii itakua na maana kwamba tangu hapo kukitokea kifo chochote ambacho chanzo chake si cha kwaida basi moja kwa moja mwenye kuubeba mzigo huo ni serikali.
Ingawaje huu utakua ni utamaduni mpya na wa aina yake Tanzania kuona viongozi kila wanapokwenda kuna walinzi lakini lazima wananchi tukubaliane na hiyo hali halisi kwa sababu MDUDU MBAYA UFISADI umeshaingia katikati yetu na kwa kuwa KUSUDIO YA MTU YEYOTE FISADI NI KULA KILE AMBACHO HANA HAKI NACHO basi ndipo VIFO vya ajabu ajabu vinapoanzia pale wenye mali au waliopewa dhamana wanaposema hapana.
Tafakarini hili.