Revolution
JF-Expert Member
- Feb 28, 2008
- 791
- 551
Wakubwa,
Jana kwenye taarifa ya habari TBC1 nikamsikia Kanumba akitamka kuhusu habari kwamba Zitto kutishiwa kuuawa, mimi sikubaliani kabisa kwamba hivi nani amuue zitto? kwa lipi hasa?
Binafsi naona watu wanataka kuzidi kumpandisha chati kwa sababu zao binafsi, Tanzania hatuna utamaduni wa kuuwana, walikuwapo viongozi waadilifu sana na hayakuwapata haya iweje leo wewe zitto watu wakutoe roho kwa lipi hasa?
Sababu imetangazwa si jambo la kubeza tena, tujadili tuone kweli hivi kuna njama za kumtoa roho au propadanda za kisiasa tu?
Sisi watanzania tuna matatizo yetu na wala hili za Zitto naona halina umuhimu kwa sasa haya magazeti yanalikuza tu bila sababu ya msingi,hebu tumalize hili la umeme na katiba yetu tafadhali.
Kwani Kanumba ni mtangazaji wa TBC? au inawezekana alikuwa anahojiwa juu ya filamu yake yenye character anayeitwa Zito?