Zitto kugombea urais 2015?

Status
Not open for further replies.
Musembi,

Usiwe mpumbavu kwa kushabikia upuuzi, werevu walio wengi wanajua ushujaa wa huyu kijana wa kigoma, na si kweli kuwa CDM imemvumilia kwa ajili ya ukomavu wa kisiasa usitudanganye we know mchezo mchafu wa viongozi wenu wanapoona mtu anae jiweza anatishiia umaarufu.

Unapotaja watu waliofulia ktk chadema na bado wamekumbatiwa na chama huwezi Mzito Kabwela ndugu, ukamuucha mwenyekiti Freeman Mbowe................. mbowe alipata umaarufu ktk bunge from 2000-2005 akautumia kugombea urais na watu mlimsifia, lakini leo dogo janja katangaza nia mnamponda kwa sababu mmelishwa sumu.

Chadema wamemkaba Zitto muda mrefu..... Tazama Mnyika alivyotengenezewa njia akiwa mgongoni kwa Zitto, kutoka kaimu naibu katibu mkuu mpaka kapora tonge la Zitto la kambi ya upinzani bungeni.............

Huyu jamaa yuko juuu hata kama CDM imeona alivyo na mlengo wa kulia coz wao ni Conservatives
 
Zitto is a quality young leader ila nadhani he is rushing na hiyo ndoto yake ya urais ya 2015
Urais hautafutwi by hook and crook kama utashi wa mtu binafsi kwa sababu tu yeye kama yeye anataka kuwa rais. Rais ni kiongozi wa jamii na jamii ndio inayoona ni nani anayefaa kuwa rais na siyo personality.

Urais anaoutaka Zitto ni kwa ajili tu ya kujiridhisha na kuandika historia lakini siyo kwa sababu anapenda sana kuwatoa watanzania point A kwenda point B hivyo tuache kumshabikia.
 

mimi sioni kama unatakiwa kutukana ndo ueleweke,kumbuka humu ndani watu wamesoma na ni watafiti wazuri sana,so be polite and wise,usikurupuke,sasa naomba ukae ulete facts ili tukujibu kwa facts,usilete taarabu

kwanza naomba nikuulize na ujibu critically,hivi wakati Zitto akihutubia na kusema 2015 yeye ndo ataipeperusha bendera ulimsikia mwenyewe ama uliipata kama SHOP TALKS? kama ulimsikia naomba utwambie alifata taratibu ZIPI na za CHAMA kipi

Pili,unasema siasa si ugomvi ndo maana Zitto anawasiliana na CCM kwa hyo tusimlaumu,mbona juzi kati Mbowe alikutana na JK wakatokea kwenye gazeti wamekumbatiana,kwanini hapa wanaCDM hawamsemi Mbowe?

Tatu,kukifanyia chama kazi haialalishi mtu atende kinyume na chama,kuna taratibu kwa viongozi na kwa wanachama,kwanini ukiuke taratibu za chama alafu ukisemwa unajitetea eti umekifanyia kazi nyingi chama kwahiyo wasikuseme?unaona sawa?
 

ndugu yangu naona umekurupuka kunijibu lakini sijaluelewa kabisa mimi naomba
1; umesema nimetukana ni wapi nimetukana?
2😛ili sijaandika sehemu yyte kuwa zitto anataka kugombea urais 20159 nilichosema alipotaka kugombea uwenyekiti wa chadema)
3:na mwisho kuhusu mbowe kukumbatiana na jk kwanini hakusemwa na zitto asemwe ni wewe wa kujiuliza kwani mimi ndiyo niliyesema kuwa na mahusiano na viongozi wengine sio dhambi. kwahiyo wewe na wengine wenye kumshutumu zitto ndio mnaotakiwa kujiuliza kwanini hamukumshutumu mbowe na mnamshutumu zitto.

MWISHO NAKUOMBA KABLA YA KUANZA KUMJIBU MTU HUMU NDANI USHIRIKISHE UBONGO WAKO VIZURI.
 


Ongea mambo ya msingi acha majungu,ndo maana hatuendelei.
 


tatizo la hili jukwaa wote sisi tunajidai ni watu wa kukosoa. Ukiuliza ebu great thinker chagua wizara , shiraka au jimbo moja unaloweza kuwa kiongozi. Taja mikakati mipango na maamuzi gani utafanya. Only few can answer this question

Most of us are just reactive waiting Ziitto to do this or kikwete to do this or Slaa to that.

Please let stop this trend.

Musembi Ungekuwa wewe ndo zitto ungefanya nini?
 
Hivi mbona Zitto anaonekana kuto kuelewana na chama chake kwa watu ambao wapo nje ya chama tu? Na nasema nje kwa sababu najua watu wengi humu ni mashabiki wa Chadema lakini hawana influence yoyote ndani ya chama kwa maana maamuzi yaki fanyika wao hawapo. Kama kweli Zitto ange kua msaliti wa chama basi angesha fukuzwa uanachama. Kama yote unayo sema ni kweli na bado Chadema hawa muondoi hiyo ina semaje kuhusu uongozi wa chama? Tusi take kujidai wote humu tupo katika inner circle wakati wengi wetu tuna leta story za vijiweni kama facts.
 

Umepatia ndugu yangu. Zito ni mwanasiasa, na siasa haziko kati ya Chama tawala na vyama tawaliwa bali hata ndani kwa ndani, yaani inaruhusiwa pia kuwa na siasa kati ya wenyewe kwa wenyewe. Zito hana kosa kufanya hivyo ni sehemu ya maisha ya siasa. Asiyekomaa kiasi hicho basi akae pembeni aepushe msongamano.
 
Agenda yenu ya kumuuwa Zitto kisiasa kamwe haitafanikiwa, kila ukifungua JF ni Zitto tu, kwani Zitto atakuwa na umri gani 2015, kama sio njama tu za kumuuwa kisiasa. Naona siasa za kupakana matope zinainyemelea CDM. Jengeni hoja mmeandaa mpango gani wa kutatua kero za wananchi mkichukua madaraka, watu wanajua ipi pumba na upi mchele, watachagua tu wanachokitaka
 

MHHH! Wengi wamesema ficha upumbavu wako usifiche hekima yako. Sina hakika kama wingi wa maneno ndo kwenye hekima ama mpangilio wa hoja ndo kwenye hekima! Weledi na ujuvi katika mambo ni vema kuendana na kauli tunazotoa kwa jamii, na wakati mwingine si vema kuwalazimisha watu kuona kijani wakati rangi iliyowazi ni zambarau. Nawakilisha
 
namkubali zitto kama mwanasiasa msomi na makini zaidi katika chadema, ila pia naukubali ukweli kwamba zitto hana msimamo na hii inatokana na kujiamini kwake kupita kiasi.
 

Ehee ebu nieleweshe

  • Right choice ya zito kuwa presdent na sio Mkuu wa mkoa au Waziri wa fedha? kwa nini ?ana siffa gani au atafanya nini?
  • Slaa ni mtedaji ina maana Zitto sio mtendaji ?
  • Kwani kazi ya president ni nini hasa na kazi ya PM ni nini hasa.
Ebu fafanua
 
MIMI NI CDM 100% YULE MNAFIKI NA MPENDA MASIFA ZITO KABWE IKIWA HIVYO MIMI NA CHADEMA BASI,NDO MAANA LINAENDESHA HUMMER NA KWAO HAMNA BARABARA YA KUENDESHEA:smile-big:
 

Zing.....nadhani unaona namna ambavyo mitazamo inapotofautiana tu, watu hupata hisia tofauti juu ya upande wa pili. Nimerejea matukio ambayo yalitokea na ambayo kila mmoja amekuwa ni shahidi, sidhani kama hapo kunakujifanya great thinker kweli? Sidhani kama nastahili hata kuigiza nafasi ya great thinker katika maigizo, kwani naamini sina nikijuacho, lakini nina uwezo wa kutunza kumbukumbu na kuoanisha na matukio yajayo, nafasi ya great thinker hiyo ni ya kwenu, huo ukuu mimi siuwezi.
Pia ikumbukwe kuwa kwa wadhifa alionao Zitto katika jamii, na mambo yanayohusishwa na yeye, anajadilika bila wasiwasi, hakuna sababu ya watu kusema ni unafiki au ni mkakati wa kumuuwa kisiasa au majungu, ikumbukwe kuwa kwa mtu mwenye akili timamu ikatokea akaongelewa kwa mazuri au mabaya, huo ndiyo wakati wake wa kujipima na kujirekebisha. Kwa wafuasi wake wanatakiwa kuwa wavumilivu na kukabili kwa umakini na utulivu hisia na hoja zote zitolewazo dhidi role model wao.
Mimi au wengine wenye mtazamo kama wangu ni kioo tu hamna haja ya kutuchukia, kwani kinachoonekana katika kioo hiki ndiyo image ya mhusika, hivyo ni wajibu wake kuji-shape upya.
Mimi binafsi huwa napenda kufanya jitihadi kufanya mambo yaliyo sahihi, lakini huwa ninasisitiza kusikia habari zilizo mbaya mbaya mapema ili nizifanyie kazi mapema, sina muda wa kusikiliza sifa au mafanikio yanayonihusu.
Kuhusu ningefanya nini? hilo lipo dhahiri, kuwa ningefanya tofauti na yale yanayoonekana kuwa ni kasoro katika mlolongo mzima niliouainisha.
Ila kwa kufupisha tu na kuwa a little obvious, kipindi hiki ningejitahidi kuwa makini na ku-walk under radar, ili ku-avoid much attention,
 
Tusimshambulie msembi hayo ni mawazo yake,pia naomba nimuunge mkono msembi,hebu niulize wapenda mageuzi ktk tanzania hii inayomilikiwa na watu wachache,yuko wapi zitto kama yule wakati ni kiongozi UDSM?yukowapi zitto kama yule kabla hajafukuzwa bungeni?yuko wapi zitto kabla hajateuliwa kuwa mwenyekiti kamati ya hesabu za mashirika ya umma?jibu siyo zitto yule tuliyemzoea kabadilika hata ufunguzi wa matawi ya chama chake UDOM,ST JOHNS,MIPANGO,na kwingineko hatujamwona akijihusisha kitu ambacho kwa miaka ya nyuma ni lazima yeye ndo angekuwa mstari wa mbele,ni ukweli usiofichika mh zitto anahitaji kurudi kundini kabla ya huo uamzi wake huo na sisi kama vijana tuko tayari kumpokea kwa gharama yoyote maana hiki ndo chama pekee chenye kutufikisha safari tuliyoianzisha.TOGETHER WE CAN.dalali
 

Wewe ndio mpuzi kwa sababu huoni madudu ya zitto, wala mnyika hajatengenezewa njia na Mwasi Zitto huyu ni mhujumu mwenye kuona zaiidi kuliko wengine. Dr ndio amewatengenezea njia wengi ndani CDM lakini kwa uelewa wako finyu hutakubali lakini habari ndiio hiyo
 

hata mimi nilimsikia kupitia runinga,issue siyo uongozi lakini anapitia njia gani?
 

zitto anautaka uwenyekiti,zitto anautaka uraisi!Mbona hautaki ukatibu Mkuu maana hata unaibu hautendei kazi?Hii inaonyesha zitto si mtendaji bali anapena atambulike.mawazo yangu
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…