Zitto, Kitila na Mwigamba wajisalimisha CHADEMA

Zitto, Kitila na Mwigamba wajisalimisha CHADEMA

Status
Not open for further replies.
Ha ha haaa nimelewa kwanini watu wa Kigoma walimuita muheshimiwa MINI KABANG kamanda umejibu vizuri nilikuwa sijui maana yake!

Bado jitahidi tena kujenga hoja Boko haram maana hapo pia inaonyesha udhaifu wako wa kuandika na kukomalia kitu usichokijua na kutokujua hata maana yake
 
Last edited by a moderator:
Ule usemi samaki ana ujanja akiwa ndani ya maji umetimia.

Baada ya kushindwa kukihujumu chama kwa mbinu mbalimbali ikiwemo ya kushambulia mikutano ya Dr Slaa na kutoa matamko ya kipuuzi wakiqatumia viongozi mbalimbali wale wasaliti waliokwapuliwa vyeo vyao ndani chadema na kinachosubiliwa ni kupokonywa uanachama wao Zitto, Kitila na Samson Mwigamba wamejisalimisha jana baada ya kujibu barua waliyotumiwa na kuomba wasamehewe na wasinyang'anywe uanachama kuwa wana mapenzi na chama.

wanataka kupika propaganda mpya ya 'chama cha wasiotoa msamaha'.
 
Heeee wewe vipi unataka tuongelee jambo moja mpaka lini? Mbona mkuu huwa anaanguka jukwaani lakini siku hizi haisemwi tena? Maisha lazima yasonge mbele ndugu.... Haya wewe unataka turudi nyuma tuuuu... Wa wapi wewe, tutolee ushamba wako hapa

Umesahau daktari alianguka toilet hivi ule mkono ulipona au uzee ngumu kuunga.
 
Chadema wakiwasamehe wanajitakia wenyewe kama walivyo jitakia uko nyuma.

Wanaomba muda wa kusahihisha makosa yao.Siku ikitokea mgogoro mwingine ndio mwisho wa Chadema.
 
Sio kila taarifa ya chama iwekwe hapa, chadema ijifunze kutunza siri. Lakini pia kama zitto ana mapenzi na chama chake, kwa nini asikanushe uovu uliotokea kigoma? Binafsi napata shida sana juu ya uzalendo wa zitto kwenye chama chake!

Labda ukiiangalia hii picha na kujaribu kuiwekea maneno utapata jibu
ImageUploadedByJamiiForums1386747544.511258.jpg
 
Ukuu wa katiba unapotumika watu wanaanza ooh unajua nilijiunga nikiwa na miaka 16 .Who cares?


Kwanza I wish to congradulate all my fellow Tanzanian on our Jamhuri Day, Mungu atupe uwezo na Busara za kujenga na kulinda nchi yetu tukufu.

Pili Vijana mnajua ukomavu hauletwi na Ubabe au na maneno ya kebehi, Mhe Zitto Hakuomba Msamaha wowote na hakuna sababu yoyote inayomlazimisha kuomba msamaha, kwani hakuna hatia ya kosa hata moja inyo mhusu yeye, yote ni ya hearsay. Yeye amejibu Barua ya Chama na amejibu vizuri sana na kwa heshima inayopaswa kukipa Chama chake.

Zitto hawezi kujitoa kwenye chama chake, na itakuwa weakness akifanya hivyo, lakini Chama kinawe kumfukuza wakiweza kuthibitisha kama mwanachama wake amefanya mbinu la kukihujumu chama, Na lazima Jamani tuwe watu makini, mara nyingi katika mikakati ya wanasiasa kuvutana na kuwa na ushindani wa kutafuta fursa za uongozi , huwa wanafanya makosa ambaye huyumbisha chama, na hao pia wanastahiki kutizamwa kwa makini na ikiwezekana wawajibike.

La muhimu hizi hikaya za Uzi huu kuwa wamejisalimisha ni uzuushi na cheap propagandur, nawe Bw Saanane chuki zako kwa Mhe Zitto zinajulikana kwa hivyo utakalo sema kuhusu huyu mwanasiasa anayeheshimiwa na wa Tanzania wengi , hawezi chafuliwa na mtu kama wewe. Bora utafute Kibarua kingine
 
"Mtoto akinyea mkono haukatwi bali unaoshwa" huu ni usemi maarufu sana unaopendwa kutumiwa na wazee wetu. Maana yake ni kuwa anayekosa basi asamehewe, lakini wakati mwingine mikono huwa haiwezi takata hasa kama "mtoto" huyo anajinyea mara kwa mara na dawa hapo ni Kuikata mikono hiyo.
Hawa jamaa hawastahili kusamehewa kwani ni wasaliti. Let them go.....

Kuna wakati ambao inakuwa ni lazima kuukata mkono huo. Je, kama una kansa je? Utaiachia kansa hiyo iutafune mwili wote?
 
Unafiki wa chadema kwa hiyo kila kitu mnakiweka hadharani?
Hivi akina Zitto wakiamua kuweka kila jambo uchi mtabaki salama?

Kama kuna mambo ambayo hadi sasa akina Zitto hawajayaweka hadharani, basi huo ni unafiki. Hawafai.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom