Zitto Kabwe: Tukemee wabakaji kusamehewa kiholela

Zitto Kabwe: Tukemee wabakaji kusamehewa kiholela

Honestly kwa hili iam with magufuli.. they have served time jamani .. if guilty they habe repented highly i believe.. najiuliza ilikuwaje wanafanya kitendo kama hicho wakati wanawake wako wakumwaga yani hadi nimewaza
Mabey ni magizo ya kishirikina au mganga.. najaribu tuu to make sense of something that doesn’t make sense.. all in all they have lost many years of there lam sure they have changed. I hope they give us good music and proceed with there talent
 
Wanasiasa washatufanya mpira wa kona unagombaniwa kupigwa vichwa miaka 56 ya Uhuru huoni mijadala moto moto kuhusu mihimili kuingiliwa,maendeleo ya Taifa na wananchi tunapenda matukio tutapewa tu.Week ijayo utasikia usajili ndani ya vyama vya siasa
 
Kwani huyo Zito yeye aliwaona kipindi wanabaka, inawezekanaje familia nzima wawe wabakaji, ina maana familia yote wanafanana tabia na hakuna hata mwenye busara.
Yeye apambane na hali ya chama chake na aache kudandia matukio.


Walikamatwa wanne..... Wawili wakaachiwa wakabaki wawili.


Sio lazima ucomment kila jambo hata kama huna uhakika nalo.
 
Ngoma imeisha pasuka tuendeleeni kucheza mdundiko vivyo hivyo hata kukuche.
 
Wapinzani waliogeuka Mafisi, kazi kungoja Magu adondoshe neno waokote yaani ni tabu tupu...
 
Katika moja ya vitu vinavyoniwazishaga sana ni kuuaminisha moyo, akili na nafsi yangu kua baba na wanawe wanaweza kuwalawiti watoto wadogo...tena baba huyo na watoto hao kibongobongo ni maarufu na wana uwezo wakumpata mwanamke yeyote wamtakae tena bure...Mmhh bado mpaka leo sijawahi pata jibu..
 
Rais hakuwafikiria waathirika yaani kwa watoto na ndugu waliokuwa majeruhi na ulawiti huu. Tena ni watanzania na wataathirika kisaikolojia kwa maisha yao yote! Na inawezekana walimpigia kura ya kumfanya awe rais. Kaona ni bora awachie watu wawili wabakaji waliokutwa na hatia na mahakama zote. Tena wakongo warudi mtaani sababu ni wapiga magita na wamesifia! Uamuzi mbaya sana na siyo wa haki!
 
Kuachiwa kwa babu seya tena kwa kusamehewa personally bila kuwekwa kwenye group fulani la msamaha lina ukakasi....!! Kwa mtu mwenye itimamu lazima ahoji haijalishi alionewa au laa...ingekuwa mataifa mengine watu wangeandamana. Labda mtoa msamaha atoe uthibitisho kuwa alionewa..!
 
Angetumia Katiba ile ile kwa Vyama vya Siasa kufanya Mikutano ya hadhara na maandamano ya amani.

Jaribuni kuanzisha mada zenu mnatuchosha. Kwa maneno kama yenu ya kimbeya mnahitaji mikutano gani tena. Hoja hamna. Humu mna ukumbi mkubwa matusi tu na kudandia hoja so ingekuwa mikutano. Afu by the way Mbona wabunge ruksa. Mkapange ya kwenu
 
Haya mambo magumu sana, Upande wa familia za waathirika yaani kwa watoto na ndugu, Upande wa siasa na uhalisia, Pengine kuna mambo nyuma ya pazia, Lakini muda ni wakati ukweli utaonekana ,"tusubiri ukweli "
Hilo neno ni hekima
 
Jaribuni kuanzisha mada zenu mnatuchosha. Kwa maneno kama yenu ya kimbeya mnahitaji mikutano gani tena. Hoja hamna. Humu mna ukumbi mkubwa matusi tu na kudandia hoja so ingekuwa mikutano. Afu by the way Mbona wabunge ruksa. Mkapange ya kwenu
Hawa jamaa sijui wakoje. Walizungusha mikono mwezi mzima ili Lowasa awe rais na aweze kutekeleza ahadi yake ya kuwaachia akina Babu Seya. Leo Magufuli kawaachia imekuwa nongwa tena, ha ha ha.
 
Rais hakuwafikiria waathirika yaani kwa watoto na ndugu waliokuwa majeruhi na ulawiti huu. Tena ni watanzania na wataathirika kisaikolojia kwa maisha yao yote! Na inawezekana walimpigia kura ya kumfanya awe rais. Kaona ni bora awachie watu wawili wabakaji waliokutwa na hatia na mahakama zote. Tena wakongo warudi mtaani sababu ni wapiga magita na wamesifia! Uamuzi mbaya sana na siyo wa haki!


Nibora wakaachiwa watu hata mia moja wenye hata kuliko kum convict mtu mmoja asiye na hatia na kwamara ya kwanza tangu magu aingie madarakani nasema Magufuli hoyeeeeeeeeeeeee
 
Kila MTU anahitaji kusamehewa Kwa kosa lolote lile! Msamaha wowote lazima upongezwe hata kama aliyesamehewa ni mtu kama Iddi Amin!
Yeye mwenyewe kizito anahitaji sana msamaha Wa watanzania! Mikono yake si safi!
 
Msamaha ni mzuri, ila kwa upande mwingine naiona sheria ikilalamika tena kwa machozi ilivyo porwa haki yake ni kama vile imebaki yatima.
 
Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ameonekana kutofurahishwa na uamuzi wa Rais Magufuli kusamehe wafungwa ambao ni wanamuziki mashuhuri, Nguza Viking (Babu Seya) na mwanaye 'Papii Kocha'.

Tangu utangazwe msamaha huo, Zitto amekuwa akiandika na kutoa kauli zinazoonesha kupingana na jambo hilo licha ya Rais kuwa na mamlaka kikatiba kumsamehe mfungwa yeyote akiona inafaa..

Miongoni mwa kauli zake huko Twitter;

"I have read judgement that convicted Babu Seya and son. And judgements at the high court appeal, appeal at court of appeal and petition at African Court. I am appalled by decision to pardon convicted rapists. Devastated by statements to congratulate such a decision" ZZk.

"Waliozomea na kuzodoa ahadi ile walikuwa sahihi. Wanaomzomea Rais kwa kutoa msamaha wapo sahihi pia. Hakuna sababu kuzodoana. Tukemee wabakaji kusamehewa kiholela" ZZK.

KWA PIKIPIKI .... KIKI
 
Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ameonekana kutofurahishwa na uamuzi wa Rais Magufuli kusamehe wafungwa ambao ni wanamuziki mashuhuri, Nguza Viking (Babu Seya) na mwanaye 'Papii Kocha'.

Tangu utangazwe msamaha huo, Zitto amekuwa akiandika na kutoa kauli zinazoonesha kupingana na jambo hilo licha ya Rais kuwa na mamlaka kikatiba kumsamehe mfungwa yeyote akiona inafaa..

Miongoni mwa kauli zake huko Twitter;

"I have read judgement that convicted Babu Seya and son. And judgements at the high court appeal, appeal at court of appeal and petition at African Court. I am appalled by decision to pardon convicted rapists. Devastated by statements to congratulate such a decision" ZZk.

"Waliozomea na kuzodoa ahadi ile walikuwa sahihi. Wanaomzomea Rais kwa kutoa msamaha wapo sahihi pia. Hakuna sababu kuzodoana. Tukemee wabakaji kusamehewa kiholela" ZZK.
haya umesikika kiongozi mkuu, mwenyekiti, katibu mkuu, mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na fedha, katibu wa itikadi na uenezi na mwanachama pekee wa EISITII-Wazalendo
 
Back
Top Bottom