Zitto Kabwe: Tukemee wabakaji kusamehewa kiholela

Zitto Kabwe: Tukemee wabakaji kusamehewa kiholela

Angetumia Katiba ile ile kwa Vyama vya Siasa kufanya Mikutano ya hadhara na maandamano ya amani.
Kwani Kazuia?
si tutumie NGUVU YA UMMA kama enzi zile?
au sikuhizi UMMA hautuamini tena tangu tuwauzie CCM chama 2015 na kuwafanya wasimamishe wagombea wawili wa URAIS washindane wenyewe kwa wenyewe?
 
I believe all legal options have been considered during the process. Justice will always find its way. That's undoubtedly. Time is the best teacher.
 
Zitto anatafuta kiki tu,wameachiwa wauaji 61,hapigi kelele
 
Ni upumbavu kupinga uamuzi wa rais alioufanya kwa nguvu alizopewa na katiba.

Ni bora upinge rais kuwa na nguvu hizo kikatiba nitakuelewa, lakini, ukishaikubali katiba na kuapa kuitetea, rais akiitumia kusamehe wafungwa, kumpinga rais ni kuipinga katiba hiyo.

Zitto asifikiri kupinga kila kitu ndiyo umahiri.

Magufuli ana makosa mengi.

Lakini, kutumia nguvu zake za kikatiba si kosa.
 
Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ameonekana kutofurahishwa na uamuzi wa Rais Magufuli kusamehe wafungwa ambao ni wanamuziki mashuhuri, Nguza Viking (Babu Seya) na mwanaye 'Papii Kocha'.

Tangu utangazwe msamaha huo, Zitto amekuwa akiandika na kutoa kauli zinazoonesha kupingana na jambo hilo licha ya Rais kuwa na mamlaka kikatiba kumsamehe mfungwa yeyote akiona inafaa..

Miongoni mwa kauli zake huko Twitter;

"I have read judgement that convicted Babu Seya and son. And judgements at the high court appeal, appeal at court of appeal and petition at African Court. I am appalled by decision to pardon convicted rapists. Devastated by statements to congratulate such a decision" ZZk.

"Waliozomea na kuzodoa ahadi ile walikuwa sahihi. Wanaomzomea Rais kwa kutoa msamaha wapo sahihi pia. Hakuna sababu kuzodoana. Tukemee wabakaji kusamehewa kiholela" ZZK.

Wapigwe PI kwani mfano mbaya kwa watanzania.
 
Kuachiwa kwa babu seya tena kwa kusamehewa personally bila kuwekwa kwenye group fulani la msamaha lina ukakasi....!! Kwa mtu mwenye itimamu lazima ahoji haijalishi alionewa au laa...ingekuwa mataifa mengine watu wangeandamana. Labda mtoa msamaha atoe uthibitisho kuwa alionewa..!

Pitia tena ile ibara ya 45 aliyotumia raisi. Inampa mamlaka ya kumsamehe mtu yeyote, mwenye kosa lolote, na haimuhitaji raisi kutoa sababu ni kwanini ameamua kumsamehe fulani na kutokumsamehe fulani.

Pia mchakato wa kusamehe ni mrefu, sio Raisi anajiamulia nani wa kusamehe, sababu raisi hawezi jua wafungwa wote nchi nzima. Kuna tume inayohusika kupendekeza majina ya wanaostahili msamaha na sababu zao. Raisi anachofanya ni kukubali ushauri na kuwasamehe waliopendekezwa wote, baadhi au kukataa kusamehe.
Nasikia tume inaundwa na wadau kama mwanasheria mkuu, jaji mkuu, mkuu wa paroli, mkuu wa magereza, waziri wa sheria na katiba, waziri wa ulinzi na usalama, waziri wa mambo ya ndani, etc.

Pia raisi anasamehe kwa kukufutia adhabu ya kifungo iliyobaki au kuipunguza. Hakufutii hatia. Yaani Babu SEYA kafutiwa kifungo lakini kisheria bado alikutwa na hatia.

Pia kila mtu hufungwa peke yake, yaani personally. Hakuna hukumu ya group, na hivyo msamaha pia ni personal. Babu Seya alitajwa kwa jina sababu ni maarufu. Kuna wafungwa wengine waliofutiwa kifo walitajwa majina, hatuyakumbuki kwa vile sio maarufu.
 
Kitendo cha Babu Sega na mwanae ambao walihukumiwa kifungo cha maisha kwa vitendo vya ubakaji wa watoto na hatimaye kuachiwa siku za hivi karibuni na kuanza kutumiwa na chama cha mapinduzi katika shughuli za kichama, inatosha kusema chama hiki kinakumbatia wabakaji?

Karibuni kwa mjadala
 
Kitendo cha Babu Sega na mwanae ambao walihukumiwa kifungo cha maisha kwa vitendo vya ubakaji wa watoto na hatimaye kuachiwa siku za hivi karibuni na kuanza kutumiwa na chama cha mapinduzi katika shughuli za kichama, inatosha kusema chama hiki kinakumbatia wabakaji?

Karibuni kwa mjadala

Mods acheni uoga na uonevu mmekuwa wepesi sana kufuta nyuzi ambazo zinakizungumzia chama cha mapinduzi lakini zile zinazoanzishwa kuzungumzia upinzani mnaziacha
Walikaribishwa Mpaka ikulu na kula chakula cha ikulu na kupiga Picha na mkulu, ikulu imekuwa ni pango la kutembelea wabakaji
 
Babu Seya aliapa akitoka atamtumikia Mungu wa Mbinguni kumbe anakuja kumtumikia mungu wake CCM, huyu mzee ni kweli alibaka nimeanza kuamini mwanzo nilijua walionewa na Waziri wa mambo ya nje wa awamu ya tatu kumbe ni kweli.
 
Back
Top Bottom