Zitto: CCM inachonganisha viongozi wa CHADEMA

Zitto: CCM inachonganisha viongozi wa CHADEMA

Kwa sisi wataalamu wa kugundua tabia za watu wakiongea ukweli, hapa Zitto kasema ukweli...lkn alitakiwa aendlee mbele kidogo tu kusema ni kwanini CCM wamemlenga sana yeye na si mtu mwingine..pia ni wakati sasa aseme wazi uhusiano wake na Jack Zoka ulikuwa katika misingi gani ilhali inaaminika wazi kuwa TISS inatumika kuihujumu CDM ? akisema hilo na tutamuelewa....lkn pia awe mkweli?

mshauri Mbowe amruhusu ajielezee kwenye vikao vya Ndani si magazetini kuepusha malumbano, Hizo tuhuma mbona hazipelekwi kwenye vikao vya ndani zinaishia kwenye mwana halisi? Zitto Zubeir Kabwe unakubalika sana wabaya wako hivi sasa wamechanganyikiwa wanatembea na vibatari mchana kweupeee hawaoni mbele!
 
Naibu Katibu Mkuu - Bara - CHADEMA, Mh. Zitto Kabwe amenukuliwa akisema ndani ya CHADEMA kuna magomvi ya kipuuzi, na ugomvi huo wa kipuuzi ndio ulipelekea vijana wake kuhamia NCCR na kuwa wabunge.

Nukuu

"Upinzani ni asili ya Kigoma, ila ninataka kusema hata hawa wabunge wa NCCR-Mageuzi wote walikuwa ni vijana wa chama chetu. Lakini kutokana na ugomvi wetu wa kipuuzi, wakaona ni bora watafute ubunge kwa kukimbilia NCCR-Mageuzi."

hivyo magomvi yote yanayoendelea ndani ya CHADEMA ni ya kipuuzi na hayatasaidia chama.




Source: Mtanzania 31st January 2013
 
mods unganisha hii kitu na ile ya kufanya maamuzi magumu na ile ya ugomvi wa CHADEMA unachochewa na CCM
 
Dah! tumuamini nani? Kila neno analoongea Zitto kama ni kweli vile. Tulioko nje hatujui kwa yakini ukweli ni upi na uongo ni upi. Tutajua tu

hivi kweli unasubiri kujua kilicho jili ndani ya CHADEMA juzi..? kama wewe ni mwana CHADEMA kweli huwezi utafuta ukweli hapa..
 
mkuu chambua zaidi iyo 'kipuuzi'.. napata wapi iyo source:Mtanzania
 
Nafurahia kwa Zitto kuzungumza kama kiongozi anayejenga timu na si anayebomoa timu. asante Zitto!
 
Nawashauri wana-CHADEMA (akiwemo ZZK) waachane na malumbano ya urais na kushutumiana...time is running out! Kuna mambo mengine ya msingi ya kimkakati yanayohusu hatima ya tz come 2015. Kwa mfano, wapiganaji kama Lema, Mnyika, Zito etc watagombea ubunge 2015 na CDHADEMA ikatoa Rais(uhakika wa kushinda ubunge upo) na katiba mpya ikatamka kwamba mawaziri wasitokane na wabunge, CHADEMA itaundaje serikali bila majembe haya? Na kama wataacha kugombea ubunge (wakitegemea kuteuliwa uwaziri kama CHADEMA itaibuka kidedea) na CHADEMA ikashindwa kiti cha urais, nini hatima ya chama? Haya ndiyo ya kuumiza kichwa kwa sasa......nawatakia siasa njema wapenda mabadiliko wote.
 
Halafu hili la urais si alisema mwaka huu hatalizungumzia tena?
Kweli kasuku ni kasuku tu.

"Nitalipia ada wanafunzi wote waliofaulu kwenda kidato cha kwanza katika kata ya Kagera". Hili nalo alihitaji kujitangaza hadharani? Mbona hasemi hao wanafunzi wako wangapi?

Ada yenyewe sh. 20,000/-. Mbona hata mimi nalipia wanafunzi 20 kila mwaka kule kijijini kwetu.

Halafu hayo mambo kama walishayamaliza ndani ya chama, kwa nini anayafufua tena?

Nimeamini huyu jamaa anapenda sifa za kijinga. Au ana lake jambo.
 
Wanabodi kwa wale watu ambao ni wataalamu wa saikolojia namuono ndani najaribu kumtazama Zitto kwamtazamo huu.

Zitto ni kijana shupavu na mwenye ambisheni za kuwa na mafanikio katika siasa hata hivyo mafanikio yake kisiasa pamoja na kwamba ameyapata akiwa CHADEMA lakini kwakuwa anamatamanio ya kutimiza ambisheni zake lazima apate sapoti hata nje ya CHADEMA ili kufikia lengo alioijiapiza kulifikia hii inamlazimu awe karibu kimtazamo (aonekane yupo nao na haungi mkono CHADEMA kwenye mambo kadhaa) aidha na watu wa CCM wenye msukumo katika jamii au taasisi ambazo anajua pia zinaweza kumsaidia kufikia malengo yake na hii nimbinu ni ya kawaida katika kufikia malengo ya kisiasa ingawa kuichagua mbinu hii huenda ikakusababishia majeraha ya kisiasa kwa pande zote na hili ndilo linamkumba ndugu yetu kaka Zitto.
 
inaoneka yoote yanayoletwa hapa kuhusu Zitto ni uongo.
ndio maanaake.kama wana ukweli wowote wa tuhuma zao mbona wameshindwa kuuweka wazi kwenye kikao,badala yake wanakuja JF na ID fake kumchafua Zitto!
Tumesha washtukia na hatutaki ungese wao, Ben Saanane na kundi lake waache kutumiwa kiakili mwisho wake mtatumiwa kimwili na upumbavu wao

[TD="class: bold l pu"]
[/TD]

[TD="class: l pd w"]This is the peak of hypocritical-deception.

People are scheming for mass sympathy. They are playing a game of ''give a baby some candy so as to collect the knife in his hand''.

[/TD]
 
Kwa sisi wataalamu wa kugundua tabia za watu wakiongea ukweli, hapa Zitto kasema ukweli...lkn alitakiwa aendlee mbele kidogo tu kusema ni kwanini CCM wamemlenga sana yeye na si mtu mwingine..pia ni wakati sasa aseme wazi uhusiano wake na Jack Zoka ulikuwa katika misingi gani ilhali inaaminika wazi kuwa TISS inatumika kuihujumu CDM ? akisema hilo na tutamuelewa....lkn pia awe mkweli?

hivi haya yote c aliyaweka waz wakati wa mahojiano ya siku nzima na asha dii kweli jf viazi wengi nashauri wamiliki waondoe hiyo kauli ya great thinker koz hao magreat thinker wamekaa kimajungumajungu
 
Maneno yake yanauzito unaostahili kupangua hoja hii, lakini pia inawezekana wamepima upepo wakaona wanazidiwa kete na kundi pinzani na lengo halijafikiwa kwahiyo wameamua kutoka kivingine kwa kukana uasi ili ajipange upya. huwa siamini sana kauli ambazo sio tamko rasmi la chama wakati wa migogoro ya vyama ! kwanini lisitoke tamko la viongozi kuhusu huu uvumi au ukweli wa kumhusu zit o ?
 
Kama ni uhusiano na usalama wa Taifa, basi uongozi mzima wa CHADEMA unahusika. Dr Slaa mara ngapi amesema habari zote za kiintelejensia anazipata kupitia jamaa zake wa usalama wa Taifa??. Wasimsingizie ZZK.

Zitto anajaribu kuruka kimanga. Unategemea akubali kuwa anakisaliti chama au lazima atafute wa kumbebesha mzigo. Nadhani angeelezea uhusiano wake na jamaa wa Usalama wa Taifa ingeleta maana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom