Siasa za kiTanzania ni rahisi sana kama kumsukuma mlevi vile. Kuna mambo huwa yanafanywa na hawa tunaowaita wanaSiasa huwa najiuliza ingekuwa ni Marekani, Japan, Uingereza au China ingekuwaje?
Ntaendelea kuamini Zitto na Mbowe ndo msingi wa uimara wa Chadema, nakubaliana na zitto kwamba Chadema ikivunjika leo itachukua miaka 20 mingine mbele kwa watu kukiamini chama cha upinzani kufikia imani hii waliyonayo leo kwa Chadema..
Ni rahisi sana kukipasua Chadema kuliko wengi wanavyodhani, ukitaka kukimaliza hiki chama fukuza kati ya hawa wa3, Zitto, mbowe au dr slaa, basi! Umeshinda.
Mie niko kijijini na pia nazungumza sana na vijana juu ya siasa za Chadema kwahyo nafahamu nguvu ya hawa watu kwenye fikra za vijana wengi wasiotumia mitandao na tv, kwao siasa za upinzani ni Chadema ya Zitto,slaa na mbowe..
Ondoa mmojawapo umeua upinzani kwa nusu ya wapenda mabadiliko nchini..
CCM badala ya kutafuta mbinu ya kukuza uchumi kama chama tawala wanatafuta mbinu za kuua vyama vya upinzani.
Mbinu hizi zitaendelea kudumaza fikra za watawala na hatimaye uchumi wa nchi.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.