Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
Jamani naombeni wana JF msimlaumu huyu Zitto Kabwe ila muilaumu CCM kwa kutufanya watanzania tuwe masikini na kuwa na tamaa za kijinga kama ya Zitto Kabwe. Ikiwezekana kuanzia sasa moderator azuie thread zote zenye jina 'Zitto' kwasababu zinaboa.

sORRY. hUKU NI KURIDHIKA KUISHI NA WASALITI KWA SBABU YA UMASKINI? No way. SA wangekuwa wanawatetea ma-traiters wasingepata uhuru. msaliti anapaswa kuvuna kadri ya usaliti wake na siyo kwa sababu ccm. CCM ni sawa na kaburu, hivyo anayerudi nyuma kmtetea kaburu anapaswa kuchomwa moto.
 
Siku zote chama ni taasisi na huwa inaheshimika kuliko mtu au mwanachama,
siku zote epuka kuwa extrovert(kulazimisha watu wakujue au kukuzungumzia wewe sana na haswa kwa mabaya).
Zitto watu wanakutakia mema ndio maana wanapiga kelele za kukuktaka ubadilike,urudi kwenye mstari na taswira yako ya awali kwa jamii,
mvuto wako unafifia kwa kasi,jamii haitasita kukutema ikiendelea na hisia hizi ilizonazo kwa sasa juu yako.
Heshima hainunuliwi dukani,chama kina wazee na watu wengine wa heshima,
si jambo la busara ukatoa tamko lolote ambalo viongozi ndani ya chama na wanachama hata wapenzi wa chama wakatilia shaka,kamwe zitto hautaweaza kuwa juu ya chama au wanachama,siku zote heshimu hisia za wanachama.
Nimesoma kwenye mwananchi la jana ukisema kuwa masuala yote yatatatuliwa ndani ya chama,sasa kama unaelewa chama ndio chenye uwezo wa kutafuta ufumbuzi wa kila kitu ni bora ukawa na heshima hiyo kwa chama na hata maamuzi yanayofikiwa na vikao halali vya chama
iwe mwiko kwako kutoa tamko lenye utashi binafsi huku ukisahau nafasi yako kama kiongozi ndani ya chama,zitto kumbuka,lolote utakalosema halitachukuliwa kama ni mtazamo wa zitto kama zitto bali ni mtazamo wa moja ya viongozi wa juu wa chadema.
Mdomo uumba,hakuna silaha kali na ya maangamizi kama ulimi,jifunze kuutumia vizuri ulimi wako kwani umri wako ni bado ktk harakati au safari za kisiasa,nikikulinganisha na mzee sitta au dr slaa umri wako ni nusu ya umri wao.kwa mapenzi mema kwako na safari yako ya kisiasa zingatia hayo na ukumbuke chadema haitapita wala kufa kwani ni taasisi ila mimi na wewe tutapita na kufa,
pamoja tunaweza
 
kumekuwa na habari kwenye magazeti kitambo sasa zenye kuonyesha mgogoro ndani ya CHADEMA. Napenda kuwajulisha marafiki zangu kuwa hakuna mgogoro wowote. Sihami wala sifukuzwi CHADEMA. Tuna kazi moja tu, nayo ni kuimarisha chama kuelekea 2015 wakati tukipigania mabadiliko ya Katiba. Tusiyumbishwe!

Source: Zitto Kabwe Facebook Status, Twitter
 
Tamko zuri maana limetoka kwako mwenyewe Zitto imarisha chama chako
 
Mheshimiwa Zitto kamuulize yule jamaa, mzungu mwafrika, mheshimiwa Charles Njonjo kule NRB Kenya-yeye alileta usemi kuwa "politics is dirty game"-ni mchezo mchafu!!!!!!! Wewe bado mtoto sana kiumri na kisiasa!!!!!! Sasa mbona unataka kutumia udini Tanzania hii kujijenga kisiasa???????,that is cheap and stupid politics???????? Hapo Chadema hapatatosha!!!!!!; tafuta kwingineko uende!!!!!; hizo brain zilizopo hapo unaziona??????!!!!!;Hayo majamaa ni labda uanzishe chama chako ambacho kitakuwa na watu wa dini moja tu????? Anayehubiri udini Tanzania ni mufilisi kisiasa!!!!!!!Tangu Kikwete aanze kupiga kelele za udini kiwendawazimu je umeona ukuta hata mmoja umetikisika????? Thubutu!!!!!; sahau!!!!!!!Kwa kuoana na kuishi pamoja bila kujali kabil, dini, rangi,nk kwa takriban nusu karne, Watanzania wamekwisha ingiana kikabila/kimila/kiutamaduni/kiuelewa kiasi kwamba kudhani siasa nyepesi za udini zitawagawa unajidanganya!!!!!!!-hii siyo Nigeria bwana-peleka siasa hizo nyepesi huko Nigeria-kaanzishe chama chako huko na udini wako!!!!!!! Mbona huwasemi Kikwete na serikali yake na chama chake cha sisiemu-kule top layer yote Bara na ZBR ni dini moja-je umesikia Watanzani wanaona hilo kama ni tatizo????? sema Zitto!!! Usituletee uchuro wako hapa!!!!!! Wewe kama Kikwete na wizi wake wa kura kakukosha hamia sisiemu kimya kimya , uone kama atakupa hata ukatibu kata!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Siasa za Chadema huziwezi wewe!!!!!!!!!!!!!!!!! Wewe ukitaka kufanya experiment toka Chadema uone-CDM itabaki stronger ;na wewe uta-perish kisiasa; kila chama watakukataa-labda nccr?????!!!!!!!!😛eace:
 
Natoa tamko kuwa habari ya Jamboleo ni ya kutunga yenye lengo la kugawa uongozi wa CHADEMA na kuleta mgogoro.

Kumekuwa na habari kwenye magazeti kitambo sasa zenye kuonyesha mgogoro ndani ya CHADEMA.


Napenda kuwajulisha marafiki zangu kuwa hakuna mgogoro wowote. Sihami wala sifukuzwi CHADEMA.

Tuna kazi moja tu, nayo ni kuimarisha chama kuelekea 2015 wakati tukipigania mabadiliko ya Katiba.

Tusiyumbishwe!

Zitto Zuberi Kabwe



Written by zittokabwe
December 7, 2010 at 10:06 AM


HABARI HII INAPATIKANA KATIKA BLOG YA MH. ZITTO

Zitto na Demokrasia

_______________________________________
***************************************
----------------------------------------------------

NA HABARI HII PIA IMEKUJA WAKATI AMBAO KUNA HABARI ZA KUSIKITISHA NA KUTISHA ZILIZOANDIKWA KATIKA BAADHI YA MAGEZETI KWAMBA KUNA UJUMBE WA MANENO (SMS) UMEKAMATWA JUU YA KUMUUA ZITTO KABWE, BINAFSI SIAMINI KABISA HIZI HABARI AMBAZO ZIMEANDIKWA KWENYE MAGAZETI AMBAYO SIKU ZOTE YAMEKUWA YAKIJITAHIDI KUIPAKA MATOPE CHADEMA.

NASEMA SIAMINI KWA KUWA KATIKA HALI YA KAWAIDA NAMBA ZA SIMU ZOTE ZIMESAJILIWA, NA INAFAHAMIKA KABISA KWAMBA KAMPUNI ZA SIMU ZINA DATABASE AMBAYO INAHIFADHI TAARIFA ZOTE ZA KILA MTEJA (CALLS AND TEXT MESSAGES).

SASA HUYO MTU ATAKUWA NI MBUMBUMBU KIASI GANI HATA KUWEZA KUWATUMIA WATU UJUMBE WA MANENO TENA WA SUALA ZITO NA KUBWA KAMA HILI?

NADHANI SASA MAFISADI WANATUMIA MBINU ZOTE KUFANIKISHA AZMA YAO JUU YA KUWAONYESHA WANANCHI KUWA CHADEMA HAIFAI.

HABARI ZA SMS YA KUMUUA ZITTO ZIMEANDIKWA HAPA:
SMS ya kumuua Zitto yanaswa - Global Publishers
 
Huu ni mtazamo wake na unapaswa kuheshimiwa!magazeti yaendelee na hila zao za kuandaa mgogoro ndani ya CHADEMA!!!
 
Good. Magazeti nayo yaandike tamko ilo. Nimefurahi Mwananchi la jana lilikua na ilo tamko,ingawa habari yenyewe ilichukua coverage ndogo.
 
Zitto is now old enough to know that YOU CANNOT EAT YOUR CAKE AND STILL HAVE IT!!
 
hivi kuna mtu anaamini habari za magazeti kuwa zitto kabwe angeondoka chadema au kufukuzwa?

chama ambacho ameshiriki kukijenga tangu akiwa shule ya sekondari? na afukuzwe na nani? na hao ambao mpaka 1995 walikuwa ccm damu na waliingia upinzani baada ya kunyimwa nafasi ya kugombea ubunge huko ccm?
 
endelea kumwogopa kama ukoma muda ukifika utamjua ni nani@@
 
Jambo leo nalo ni gazeti nilidhani ni kipindi katika radio fulani dsm
 
Angalau sasa inatia moyo kidogo!
...Nimekuwa naombe Zitto atoe kauli yeye mwenyewe binafsi, na ndiyo njia pekee ya kurudisha imani ya watu, hasa kipindi hiki anachoonekana kama anapishana na wenzie!...Zitto, wewe ni mwanaume, jaribu kubehave accordingly, kuwa na msimamo, ondoa hili wingu la mashaka linalokuzunguka broda!.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom