Ukiamua kutoka bungeni, fanya kweli. Toka bungeni kwa msingi wenye mantiki, shikilia msimamo wako, chukua hatua zitakazoleta mabadiliko. Sio unatoka bungeni kuuza sura kwenye magazeti na kupiga "kelele" ukiulizwa legal strategy huna much less political. Unabaki kupigwa checkmate !
Mi naona badala ya kuleta mchezo wa kuigiza wa kutoka bungeni, mara humtambui rais, mara unamtambua lakini hutambui matokeo (WTF is that ) CHADEMA wangeamua moja, kama wanao ushahidi hamna kushughulika na shughuli zozote za bunge mpaka waweke mpango kabambe wa angalau kubadilisha katiba, sheria za uchaguzi na NEC, au kukubali kuingia bungeni, kumtambua rais na kushinikiza mambo kutoka bungeni na kwa kuwahamasisha wananchi.
Sasa hivi walichofanya ni kujipunguzia heshima tu, kwenye kumtambua rais wametoka, kwenye kutomtambua rais wametoka, ilimradi wamebaki wanaelea elea tu kama ndumilakuwili wasio na msimamo wanaangalia upepo wa siku unaenda vipi, kama leo kutomtambua rais ndiyo dili basi hatumtambui, kesho tukiona kinaweza kutuwakia ikala kwetu tunamtambua bila aibu tunaweka spin za kitoto eti "rais tunamtambua, hatuyatambui matokeo". Utamtambuaje rais aliyewekwa madarakani kwa matokeo bila ya kuyatambua matokeo?
Mi naona katika strategies hizi mbili, yenye akili ilikuwa ile ya Zitto, ya kuuchuna wamtambue rais kwa sasa wakati wanapanga mipango ya kubadili sheria na katiba. CHADEMA walikuwa hawajajiandaa kwa kitu kikubwa kama kutomtambua rais, rais mwenye dola na bunge. Kwa hiyo kukurupuka na kufanya mambo half baked kumewaumbua tu.
Of course siasa za ushabiki zitaona kutoka ndani ya bunge ni ushindi hata kama hakuna sheria yoyote iliyobadilika na actually hata in the court of public opinion ambako mtu ungeweza kusema CHADEMA wamepeleka kesi yao, watu kibao wanaona hii move fyongo.