Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
Ahame asihame haituhusu tunachotaka ni katiba mpya!!!!!!!!!!!!!!
 
Wakuu habari za punde ni kwamba Zitto Kabwe atahamia NCCR mageuzi, na kwamba atagombea ubunge kigoma kaskazini kwa chama hicho. kwa hiyo basi atakua ametimiza kazi yake ya kuivuruga cdm na mafisadi watashangilia. ila cdm itaendelea kuwepo na kuendelea kufanya kazi uzuri.
Habari hii imekaa kiuchochezi, hata kama what is the big issue kuvuja kwa pakacha nafuu ya mchukuzi.

Tunachotaka ni katiba mpya kwani atahama na Katiba ya Tanzania? Let Him Go.
 
Zito ulianza taratiibu.
Mara ukatetea mitambo ya dowans inunuliwe.
Hadi Mwakyembe wa ccm akakushangaa.
Leo unajifanya wewe ndio wewe chadema hawana sauti kwako.
Yuko wapi Lawrence Masha?
Na wewe utapotea kama yeye.

He better go out he is the obstacle to our move. Alipopewa mlungula huyu kijana alisema sitaki tena ubunge maana alijua jamaa wameshampa pesa ambazo zitamfanya asiongee aliyoweza kuongea na akaota its better i step out akaja kuona bado he needs money akagombea. Sasa anaharibu tu, shame on you.......
 
Pamoja na yaliyoandikwa kwenye magazzette Mh Zitto hajafanya kosa la kufanya uongozi wa Chadema umfukuze uanachama. Endapo angekuwa ndani ya Ukumbi wa Bunge na akabaki ndani wakati wabinge wa CHADEMA walipotoka nje hapo angekuwa amekiuka msimamo wa chama chake
 
wakuu habari za punde ni kwamba zitto kabwe atahamia nccr mageuzi, na kwamba atagombea ubunge kigoma kaskazini kwa chama hicho. Kwa hiyo basi atakua ametimiza kazi yake ya kuivuruga cdm na mafisadi watashangilia. Ila cdm itaendelea kuwepo na kuendelea kufanya kazi uzuri.


aende kwa amani akiendelea na mchezo wake tuta mhaleluya
 
Kwani zito ni nani mbona utafikiri ni kama Mbowe nanataka kuihama chadema, zito ni kama mbunge kati ya wabunge wale 45 wengine wa chadema sioni ajabu kuhamia NCCR maana watu hawakuipenda chadema kwa ajili ya zito kabwe, na wale watu mil. 2.2 hawatoki kigoma wote kwa hiyo anauhuru kwa kuhamia NCCR au CCM akipenda ni chaguo lake.

Watu wanachopenda kwa chadema ni Ubora wa Sera na si kwamba ukihamia NCCR/CCM ndo itakuwa kama chadema hiyo isahau.

Embu angalia kitendi cha mwenyekiti wa chama Mbowe mwaka huu kutogombea na kumpisha Dr Slaa huwezi kuta kwenye chama kingine. mfano NCCR, wakati mbowe kwa nafasi ya umwenyekiti anampa tafu Slaa, Mbati kajichimbia Kawe hata kumpa tafu Rungwe hataki sasa kigoma imetoa wabunge wanne wa NCCR ukimwuliza Mbatia hawajui hata kwa majina.

Kwa hiyo issue ni Sera ya chama inakubalika kwa wasomi, na wananchi wa kawaida?

Ni hayo tu
 
Wakuu habari za punde ni kwamba Zitto Kabwe atahamia NCCR mageuzi, na kwamba atagombea ubunge kigoma kaskazini kwa chama hicho. kwa hiyo basi atakua ametimiza kazi yake ya kuivuruga cdm na mafisadi watashangilia. ila cdm itaendelea kuwepo na kuendelea kufanya kazi uzuri.
Na hilo fungu la kufanya uchaguzi tena litatoka wapi au ndio kuchezea pesa ya wananchi,kwa hilo sheria za uchaguzi zinasemaje iwapo Zitto atakiacha solemba CDM,kwa maoni yangu CDM wamtose Zitto,kwani keshakuwa kero kwa uongozi wa CDM,ajue CDM kaikuta na itakuwepo asijione yeye ndio mwanzo na mwisho,CDM ni zaidi ya Zitto
 
Umenena kama real great thinker

Zitto ana uhuru wa kufanya lolote lile, kuwa msaliti, fisadi, kujiunga CCM, kubaki chadema, hatakuwa wa kwanza, wala taarifa hiyo haitakuwa nja uzito wa kusimamisha jua lisiendelee kuzunguka dunia!

Cha muhimu ni kuwa tunahitaji katiba mpya na tume huru ya uchaguzi, kuvitafuta hivi au kuvipigani hakujalishi Zito atakuwa upande wetu au la! tuwaze makubwa jamani!![/Q







Ni kweli mkuu. Zito si Mungu ambaye habadiliki. Kama uko CHADEMA kumfuata zito imekula kwako. Imeondoka miamba ilokuwa upinzani na waliodhaniwa kuwa wao ndio jiwe kuu la pembe katika upinzani. Tusiwasahau kina Lamwai, Kabourou nk. Kama kina Kaborou zituksa kwenda anakoona kwamfaa. Huenda kaahidiwa uenyekiti kama Mrema!
 
Chadema is not an individual put a party with its ideology, so why is zitto's claim/action such an issue? Are we loosing focus to continue our ideology? Can't Chadema survive without given individuals? Plus if zitto is really up to something fishy, let us wait instead of predicting this and that; plus, as others have already mentioned, he has his constitutional rights to speak and do as he wants; bora asivunje sheria. Chadema stands for truth and justice, it represents the grassroots whose plight has been overshadowed by greedy and corrupt leaders of this nation. People who use others to climb to power to benefit more and more at the expense of others. So Chadema is there to stay to its principles.......
 
Huyu anayejiita Zitto amekuwa akizua migogoro mingi ndani ya chama kwa nini?kila chama kina matatizo yake sa kinachomfanya kuropoka ropoka ni nini?Mi simwelewi ana nia gani kama sio kukiangamiza chama
 
Wakuu habari za punde ni kwamba Zitto Kabwe atahamia NCCR mageuzi, na kwamba atagombea ubunge kigoma kaskazini kwa chama hicho. kwa hiyo basi atakua ametimiza kazi yake ya kuivuruga cdm na mafisadi watashangilia. ila cdm itaendelea kuwepo na kuendelea kufanya kazi uzuri.

Unachoeleza hapa ni kuwa Jimbo la Kigoma Kaskazini lina mwanachama mmoja tuu ambaye ni Mh Zitto ndiye anayeweza gombea ubunge akashinda, katika hao waliompigia kura hakuna ambaye anaweza kugombea akashinda kama Zitto ataondoka?
 
Bora kwa kweli JK aliwachakachua, mmeanza kutoana NGEU asubuhi kweupe namna hii, mhhmmmm. Tatizo tu ni viji ruzuku vimeongezeka hakuna kingine hapo.
 
Kutokana na kichefuchefu (haswa baada ya kusema anamtambua JK ni amiri jeshi mkuu na alama ya bunge na hivyo si vizuri kutoka bungeni na kwa kiburi kabisa kusema anasubiria hatma yake chamani kutokana na uamuzi wake huo) ambacho mh. Zitto Kabwe ameendelea kuleta ndani ya CHADEMA wana JF wenzangu nilikuwa ninatoa mapendekezo kuwa huyu jamaa ni wa kuogopwa kama ukoma, na ni kidudu hatari kuliko KIRUSI CHA UKIMWI kwa wana upinzani, wapigania haki na kwa wananchi wa Tanzania waliodhulumiwa haki zao kwa muda mrefu na chama tawala cha CCM. Kwangu mimi namwona ni msaliti mkubwa wa Watanzania na upinzani. Hivyo ni nilikuwa napendekeza aondolewe CHADEMA haraka kwani amepandikizwa na CCM. Nakishauri CHADEMA kimvue uanachama ili kunusuru upinzani wa ukweli ambao umebaki peke yake CHADEMA. Je wana JF wenzangu mnaonaje? Je aendelee kubaki CHADEMA au aondolewe. Ushauri utakaopatikana hapa ukiambatana na sababu za msingi, naomba CHADEMA waufanyie kazi.
Zito of late amekuwa a controversial figure, na amekuwa mtu anayetaka kuonyesha misimamo yake tofauti na msimamo wa chama. Hili ni jambo la ajabu ukizingatia kuwa yeye ni kiongozi katika chama. Misimamo ya chama inakuwa reflected kupitia maamuzi ya chama na maamuzi ya viongozi wake. Sasa Zito anapoamua hivi na chama kinaamua vile hilo ni suala la mafahari wawili hawakai zizi moja. Ni dhahiri fahari mmoja hana budi kuondolewa atafute zizi lake. Zito anataka aonekane kama yeye na sio kuwa chama ndio kionekane. Mtu wa aina hii hatawasaidia chadema kwani wanahitaji kujenga chama imara mpaka huko vijijini. Ni kwa njia hiyo tu ndio wataweza kuchukua dola. Umaarufu wa Zito peke yake tena unaotokana na decions zina seek cheap popularity hautawasaidia chadema sana Zito atazidi kuwa chanzo cha migogoro chadema. Now the question is how to deal with this problem. Kumfukuza Zito is one way of dealing with it. The other way is stripping him those positions he is holding in the party so that when he diarhoea through his mouth he will do so as an individual and not a chadema official
 
Kwani zito ni nani mbona utafikiri ni kama Mbowe nanataka kuihama chadema, zito ni kama mbunge kati ya wabunge wale 45 wengine wa chadema sioni ajabu kuhamia NCCR maana watu hawakuipenda chadema kwa ajili ya zito kabwe, na wale watu mil. 2.2 hawatoki kigoma wote kwa hiyo anauhuru kwa kuhamia NCCR au CCM akipenda ni chaguo lake.

Watu wanachopenda kwa chadema ni Ubora wa Sera na si kwamba ukihamia NCCR/CCM ndo itakuwa kama chadema hiyo isahau.

Embu angalia kitendi cha mwenyekiti wa chama Mbowe mwaka huu kutogombea na kumpisha Dr Slaa huwezi kuta kwenye chama kingine. mfano NCCR, wakati mbowe kwa nafasi ya umwenyekiti anampa tafu Slaa, Mbati kajichimbia Kawe hata kumpa tafu Rungwe hataki sasa kigoma imetoa wabunge wanne wa NCCR ukimwuliza Mbatia hawajui hata kwa majina.

Kwa hiyo issue ni Sera ya chama inakubalika kwa wasomi, na wananchi wa kawaida?

Ni hayo tu


well said..mwache aende tena anachelewa sana kuondoka amekuwa mzigo tu
 
Kwani zito ni nani mbona utafikiri ni kama Mbowe nanataka kuihama chadema, zito ni kama mbunge kati ya wabunge wale 45 wengine wa chadema sioni ajabu kuhamia NCCR maana watu hawakuipenda chadema kwa ajili ya zito kabwe, na wale watu mil. 2.2 hawatoki kigoma wote kwa hiyo anauhuru kwa kuhamia NCCR au CCM akipenda ni chaguo lake.

Watu wanachopenda kwa chadema ni Ubora wa Sera na si kwamba ukihamia NCCR/CCM ndo itakuwa kama chadema hiyo isahau.

Embu angalia kitendi cha mwenyekiti wa chama Mbowe mwaka huu kutogombea na kumpisha Dr Slaa huwezi kuta kwenye chama kingine. mfano NCCR, wakati mbowe kwa nafasi ya umwenyekiti anampa tafu Slaa, Mbati kajichimbia Kawe hata kumpa tafu Rungwe hataki sasa kigoma imetoa wabunge wanne wa NCCR ukimwuliza Mbatia hawajui hata kwa majina.

Kwa hiyo issue ni Sera ya chama inakubalika kwa wasomi, na wananchi wa kawaida?

Ni hayo tu

Hao wa4 aliwafanyia campaigne kwa kuwa yeye si mali ya CHDEMA, Aende tena na tena, hatuhitaji vigeugeu kwenye chama. Na asidhani Tanzania ni Kigoma. Msaliti mkubwa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom