Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
Zitto alitaka awe KUB na misimamo yake hii kwa JK. Hebu fikiria: Spika Anna Makinda; NS Job Ndugai; tungekuwa na Bunge gani? Zitto jifunze kidogo ile dhana ya UWAJIBIKAJI wa PAMOJA. Usidhani kwamba hata huko kwenye CC ya CCM wote walikubaliana kumtosa Sitta. Haujamsikia hata mmoja akijitokeza hadharani kueleza msimamo wake tofauti na ule alooueleza Makamba.
 
Katika SIASA kupingana kimtamzamo na wenzake ni jambo la kawaida ila yeye kama kiongozi alipaswa kusimamia na kutetea maamuzi ya wengi bila kuujulisha umma kura yake iliegemea upande upi. Hata hivyo bado ana uhuru wa kuzungumza yeye kama Zitto na Mbunge wa Kigoma Kaskazini
 
Kutofautiana kupo ila kwa utaratibu unaoeleweka si kila mtu anaweza kuja kwenye public kutoa msimamo wake,kwani wengine hawana tofauti na mambo ndani ya chama?Kama ni amewakilisha maamuzi ya jimbo lake mbona hakusema kabla ikajulikana?na ni kwa nini yeye tu ndio awe anawakilisha maoni ya jimboni kwake?Kijana keshalewa itategemea maamuzi ya chama kitafanya nini ila ni ukweli dogo anaporomoka.Pia anahatarisha utulivu ndani ya chama.
 
Niliandika hapa https://www.jamiiforums.com/uchaguzi-tanzania-2010/71656-msaada-kwenye-kona.html kabla ya Uchaguzi.

Tatizo la zitto ni KUTANGULIZA MASLAHI BINAFSI MBELE ya yale ya UMMA kupitia mgongo wa MSIMAMO THABITI! Na kupitia huyu huyu, ccm inaingiza VIRUS CHADEMA. HAWEZI kuondoka kwa sababu sasa kwani hata wanaomtumia wanamaximize akiendelea kuwa ndani ya chama kuliko akiwa nje. Pamoja na ukweli kwamba PUBLIC TRUST Graph yake inashuka, lakini anamomonyoa sawia UMOJA katika chama na sura ya chama inapata MAWAA katika jamii.
 
Not suprised, Where is Warid Kaborou( whatever his name), he is political dead,like Tambwe Hiza, Msabaha,Masumbuko Lamwai and other traitors, Zito go,go, join them,the birds of the similar color fly together.
 
ni kweli.zitto aondolewe chadema.ukweli chadema isipofanya hivyo sasa itakuja kufanya hivyo ikiwa imechelewa.mbona tarime siyo ngome tena ya chadema? Kigoma ndo hiyo inaenda nccr.chadema ni chama cha kitaifa sasa.aache deko.wala hana chochote zaidi ya akina mdee na sasa ndo kabisa,nyerere,mnyika,lissu,zitto nini bana.nasisitiza aondolewe
 
ki ukweli yule jamaa huwa ana vielement ambavyo bado sijavielewa vizuri


kama wengi walishinda basi angeingia bungeni na kisha kutoka.

ANA KIBURI CHA ASILI
 

WELL DONE ZITTO, kwa kusema ukweli na kutokuwa mnafiki wa dhamira ya nafsi yako kwa kile ambacho unakiamini. Huo ndio ushujaa, usiogope mtu na sema ukweli sio kuburuzwa na wachache ndani ya CHADEMA
 


zitto amekuwa msaliti wa mabadiliko maana hata anayo yafanya tangu kuingizwa kwenye kamati ile ya madini zitto amekuwa mwanachama wa chadema lakini ki uhakisia zitto yuko ccm hana tofauti na mrema wa tlp!!!! Mifno inaendelea kudhihirika.


Chonde chonde zitto tunaomba kama unadhamira ya kweli usivuruge vuguvugu la mabadiliko maana hautabaki salaama kwani adhabu ya mungu dhidi ya udhalimu unaotaka kutufanyia itakuwa kubwa!!!!!!!!!!!!
 
Tatizo la zitto ni tamaa ya madaraka, na misifa na asipoangalia umaarufu wake utadondoka
 
hata kule jimboni kwake alishinda kwa tofauti ya kura chache sana


huyu angekuwa ndo mwenyekiti angeiuza chadema....... hana maana
 

I agree with you: Kwa sasa kuna agenda muhimu za kushughulikia kwa pamoja, wasihamishe focus kutoka kwenye kudai Tume huru, Katiba mpya kwenda kwa maoni binafsi ya Kiongozi mmoja mmoja
 
Jamani,
Hichi ni kipindi cha kuimarisha na kukijenga chama kiwe thabiti zaidi.

Ishu kama hiyo sidhani kama ina uzito kiasi hicho bali ni jambo la kumkalisha/kumwonya.

Tusikubali kumpa kunguru faida kwa kunyoosheana vidole hadharani.

Ni mtazamo wangu tuu.
 
Ninaamini UONGOZI wa juu wa CHADEMA unamfahamu ZITTO. Wasimfukuze. Watampa umaarufu kama ule alioupata BUngeni kwenye suala la Buzwagi.
 
Ninaamini UONGOZI wa juu wa CHADEMA unamfahamu ZITTO. Wasimfukuze. Watampa umaarufu kama ule alioupata BUngeni kwenye suala la Buzwagi.
Mi nadhani udhuru nao una threshold yake mkulu.
 
Amri jesh mkuu ambae alishinda kwa wizi wa kura. Zitto, hoja ya kitoto. Sema nyingine.

Kwangu mimi Zito hajawahi kuwa hero kwa kuwa ni opportunist mkubwa sana. Maelezo yake ni ya kitoto sana
 

Ni kawaida kabisa kutofautiana kwenye baadhi ya mambo... Naamini hata ndani ya Baraza la Mawaziri huwa pia wanatofautiana. Lakini Sio busara kuongea "publically" kwenye kitu ambacho maamuzi yamefanyika tofauti na maoni yako., ni kuonyesha uchanga wa uhuru wa maamuzi ndani ya vikao. Naami CHADEMA wana "Code of Conduct" na hasa inapokuja namna ya kutoa matamko rasmi ya CHAMA na Maoni binafsi
 
Mi nadhani udhuru nao una threshold yake mkulu.

Nafahamu. Ataondoka mwenyewe atakapoona anatofautiana na wenzake karibu kwa kila jambo. Kaka yake, Dr Kabourou, hayuko CHADEMA. Hakufukuzwa. CHADEMA ni imara zaidi sasa kuliko wakati wowote. Misimamo ya watu wa KIGOMA, KAGERA, MBEYA,......inafahamika.
 
Zitto atueleze anaitaka CHADEMA haitaki siyo kila siku yeye tu, kama anataka kuwa mpiga debe aende huko CCM akaungane na Tabwe Hiza
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…