HATARI: Nyoka kaingia ndani ya CHADEMA
Tumepata taarifa kuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini kupitia CHADEMA, Zitto Kabwe, akiongea na TBC1 amesema kuwa yeye ni miongoni mwa Wabunge wa CHADEMA waliokuwa wanapinga ile walkout isifanyike Bungeni Alhamisi iliyopita wakati Kikwete anahutubia.
Watu wametoa mawazo mbalimbali kuhusu suala hili. Kuna waliosema ameonesha ukomavu wa kisiasa na demokrasia ndani ya CHADEMA.
Mimi nina mawazo tofauti sana. Kitendo alichofanya Zitto Kabwe ni utovu wa nidhamu wa hali ya juu kwa uongozi wa CHADEMA.
Yeye kama mwanachama wa CHADEMA, Mbunge, Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA na Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni anapaswa kuelewa kuwa maamuzi yote yanayofanywa na chama yanakuwa ndiyo msimamo wa mwisho wa chama. Hapa kuna suala la collective responsibility.
Alichokifanya Zitto kwa kuongea na TBC1 ni sawa na waziri ambaye anatoa siri ya vikao vya Cabinet kwa vyombo vya habari.
Mfano, kwenye cabinet kunatokea mvutano kuhusu suala fulani, let's say uuzwaji wa nyumba za serikali. Mawaziri wanajenga hoja zao halafu serikali inafikia uamuzi wa mwisho kuwa itauza nyumba za serikali kwa vigogo wa serikali.
Then atokee waziri mmoja aseme hadharani kwenye media kuwa yeye alipinga mpango wa kuuza nyumba za serikali kwenye Cabinet lakini akazidiwa kura na mawaziri wengine. Huyo mtu angefukuzwa kazi mara moja.
Ni jambo la kustusha sana kuona kuwa Zitto amekiri hadharani kuwa yeye alipinga jambo hili na kulikuwa na mvutano ndani ya CHADEMA. Kwa matamshi haya, ametoa siri za vikao vya ndani vya chama.
Uamuzi unapofikiwa na chama hata kama wewe binafsi haupendi unakuwa ni wa mwisho na lazima wewe uukubali, uunge mkono na uutekeleze.
Nadhani kama kiongozi wa CHADEMA, Zitto ameonesha utovu wa nidhamu kwa chama, amevunja kiapo cha kutunza siri za chama na ameonesha kukosa maadili.
Tena Zitto alienda mbali zaidi na kusema kuwa yeye aliamua kutokwenda kabisa Bungeni kwa kuwa hajakubaliana na walkout. Hili ni kosa kubwa sana la kupingana na maamuzi halali ya chama.
MASWALI YA KUJIULIZA:
1. What is Zitto Kabwe trying to achieve?
Je, anataka kuonesha umma wa Watanzania kuwa kulikuwa na mgawanyiko kwenye CHADEMA juu ya hili jambo na yeye hakuunga mkono uamuzi huu? Au pengine huenda anataka kuwaonesha vigogo wa CCM kuwa kazi waliyomtuma kuzuia walkout aliifanya kwa bidii na jitihada zote lakini akashindwa.
Kwa ufupi, kitendo cha Zitto si jambo childish tu, bali kinazidi kujenga zile hisia zilizopo mura mrefu kuwa yuko karibu mno na vigogo wa CCM na ni mtu ambaye huwa anatumiwa tumiwa hovyo kulinda maslahi fulani ya watu wachache.
CHADEMA ijihadhari na nyoka huyu hatari.