Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
Wewe huna hoja Jasusi wa taarabu,, kama ni tofauti na enzi za nyerere kwa nini wote mna-muattack toka alipotoa mawazo yake yasiyo ya kinafiki?? At the end of the day inabidi na nyie muwanyooshee kidole hao waliotoa hilo wazo la kitoto la kutoka nje wakati mkuu wa nchi anaanza kuongea. Watanzania hatuko hivyo. Wanaume hatuko hivyo. Ninatoa wito kwa mkuu wa kambi ya upinzani bungeni ajiuzulu wa sababu ameonyesha hana Leadership quality, na pia ajiuzulu Uenyekiti wa chama kwa sababu yeye kama baba ameshindwa kuwaongoza vyema watoto wake. hafai

Posts 420

Thanked twice!
 
I am convinced and always been skeptical on this body referred to as ZITO. He is the same person since then, has never been different. Anyway time will tell
 
Wala msishituke kwani aangalie ushindi alioupata mwaka huu huko Kigoma Kaskazini. Namba za Zitto Kabwe zinahesabika. Atachoka mbaya!!!
 
Nyinyi munapenda Zitto aseme yes sir! kila wakati? Anayo haki ya kukataa kuunga mkono kitu kama hawafikiani nacho na huo sio usaliti.

Usaliti ni ile kujidai umekubali kumbe rohoni mwako hupendi kile kinachofanyika.

Jaribuni kufikiri nje ya boksi jamani!
 
Nyinyi munapenda Zitto aseme yes sir! kila wakati? Anayo haki ya kukataa kuunga mkono kitu kama hawafikiani nacho na huo sio usaliti.

Usaliti ni ile kujidai umekubali kumbe rohoni mwako hupendi kile kinachofanyika.

Jaribuni kufikiri nje ya boksi jamani!

Tumia ubongo mkuu kuelewa na sio damu, yes kukataa au kukubali hiyo ni democrasia yake lkn swali ni kwa vipi anakuja median kutangaza yote yalojiri katika kikao cha chama? Ni wote waliomchagua Kikwete CCm au wanaomuunga mkono MAKAMBA pumba zake?Je umesikia hata siku moja Kada wa sisiemu kuja mediani na kulopoka kama huyu ZITTO? mkuu think twice nadhani ni wanamziki kibao wameimba hivi...
 
nimependa zaidi jinsi chadema walivyomuignore so far hasa kwenye media

he wants something, but he wants someone else to "get the monkey off his back"... chadema leadership keep quiet, let this pass and after baraza la mawaziri take charge, he has some expectatiosn from January and Jussa. together with him, the trio who think they are the smartest tanzanian of this generation, which unfortunately not true...

Once rais amemaliza uchaguzi, weka adhabu ya kukosa nidhamu, atoke au asitoke shauri yake, na akitoka kwenye uchaguzi yeye ni msaliti, fight... if he wins congrats, if he loses,he goes back to school

he has behaved like a wife whose love for his boss is way beyond repair
 
ZITTO KABWE hana maadili, ni mtu asiye na msimamo na kama anajidanganya kwamba iko siku atakua Rais kwa kuwa anajipendekeza kwa mafisadi amenoa!!!

Amesaliti chama hana mshikamano na wenzake( collective responsibility) kama kiongozi wa ngazi ya juu kabisa wa chadema alitakiwa kusimamia msimamo wa chama na sio wa mafisadi.

Mbona CCM wanasimamia hata upuuuzi wa kumuondoa spika SITTA?!!! zitto umenunuliwa na kwa hili wewe ni bei rahisi sana hufai. jiuzulu uondoke chadema ukaungane na Kafulila ndio mwenzako mtaweza kufanya wote unafiki.

AM SORRY TO SAY THIS. lakini sisi watu wa kigoma sasa hatueleweki kwa jamii, mana alikuepo Amani kaburu akasaliti, akafuata Kafulila na wewe uko njiani.mnatutia aibbu
 
Zitto alianza kubadilika pale alipoanza kupewa uongozi wa vikamati vya bungeni mh kazi kweli kweli
 
Jambo hili ni la kuwa nalo makini sana kwani mtu huyu ni kiongozi wa juu wa chama na mmoja kati ya viongozi wa kambi ya upinzani bungeni inaonekana si mwenye uwezo mzuri wa kutunza siri na si mtu mwenye uwezo wa kukubaliana na na demokrasia, nashauri viongozi wengine wa chama wamwite na kuongea naye juu ya nini maana ya alichokifanya na kina madhara gani ndani ya chama na katika jamii ya watanzania as well.
 
Nyinyi munapenda Zitto aseme yes sir! kila wakati? Anayo haki ya kukataa kuunga mkono kitu kama hawafikiani nacho na huo sio usaliti.

Usaliti ni ile kujidai umekubali kumbe rohoni mwako hupendi kile kinachofanyika.

Jaribuni kufikiri nje ya boksi jamani!

Bintimkongwe, unaweza kuwa ni shabiki wa Zitto na tunaelewa ana mashabiki wengi. Lakini usiwe shabiki kipofu. Kwa vyovyote vile, lazima ukiri kuwa Zitto amekosa maadili kwa kutoa siri za chama hadharani. Alikuwa na kila haki ya kupinga uamuzi huu akiwa ndani ya vikao vya chama. Lakini uamuzi wa mwisho ulipochukuliwa, alitakiwa kukaa kimya. Hata kamati kuu ya CCM wenyewe ilipoamua kumfukuza Spika Samuel Sitta kulikuwa na mvutano mkubwa. Je, umemsikia Bernard Membe kwa mfano kujitokeza hadharani na kusema yeye alipinga uamuzi wa kumfukuza Sitta?

Kwa kweli Zitto lazima alaaniwe kwa kujaribu kuleta mtafaruku ndani ya CHADEMA, ambacho ndiyo chama sisi Watanzania tunakitegemea kituokoe kwenye janga la utawala wa CCM.

Kwa maslahi ya taifa, tuweke ushabiki wa majina ya wanasiasa fulani pembeni na tuangalie masuala kwa upana wake.
 
Kama nilivyosema katika post nyingine, huyu bwana mdogo ama ni mchanga kiasi cha kutisha na hatui maana ya uwajibikaji wa pamoja (colective responsibility) au ni mtu ajipendekezae kwa ccm. Mbunge ni mtu potential kuwa waziri. Sasa kama hawezi kutunza siri za vikao atawezaje huyo kuwa waziri? Nanyi wengine mnaofikiri demokrasia ni uhuru wa kuropoka siri za ndani za chama kaeni chini mfikiri. Demokrasia inamruhusu mtu kutofautiana na wenzake na kutetea kile anachoamini. Lakini watu mkishafikia maamuzi ya pamoja yanakuwa yenu wote hata kama wewe hukuafiki. Huwezi kujitoa wewe na kutangaza kuwa hukukubali. Kama unaona huwezi kuchukulianna na wenzako basi unajiuzulu, ndio uweze kusema hukubaliani. Sasa kama Zito haelewe kanuni rahisi hizi za uongozi ni kiongozi gani. Nasema Zito sio reliable, ana element ya rebellion na disloyalty kwa viongozi. Viongozi kama hawa ndio walioifanya NCCR-MAGEUZI ionekane kuwa haifai walipoanza kupingamana wenyewe kwa wenyewe. Na kama mnakumbukuka, hapo ndipo ulipokuwa mwisho wa chama hicho. Hii ni njanja ya ccm, kukisambaratisha chadema. WAMESHINDWA. Chadema mwangalieni huyo bwana mdogo, hana adabu huyo, msimwonee haya mkalisheni, kama hasikii mfungulieni mlango arudi kwa hao waliomtuma.
 
Nyinyi munapenda Zitto aseme yes sir! kila wakati? Anayo haki ya kukataa kuunga mkono kitu kama hawafikiani nacho na huo sio usaliti.

Usaliti ni ile kujidai umekubali kumbe rohoni mwako hupendi kile kinachofanyika.

Jaribuni kufikiri nje ya boksi jamani![/QU
Issue kutoa siri, kwani ye peke yake ndio alikataa? Wabunge 11 walikataa iweje ye aongee, mbona wenzake hawakusema.
 
Huyu Nyerereist amekuwaje akawa JF senior Expert member na utumbo huu? how? inakuwaje awe amepost posts 420 lakini amekuwa thanked mara moja tu? nadhani huyu ni junior member tu kama siye au ni mropokaji tu!

Ningekuona una busara endapo ungejibu hoja nilizozitaja toka mwanzo kuliko kuanza kunivamia mie, wewe umejiunga 2010 mie 2007 na ninajua huu ni mtandao wa Small mind people, wasioweza kujadili maswala, nabadala yake neno lao ni Ufisadi na kumtaja makamba, lowasa kila saa,, grow up. Ukifuatilia kwa makini huu mtandao ni wa MASHABIKI WA CHADEMA na pia watu waliokua very biased kwa hiyo huwezi kua thanked unless uitukane CCM,, hayo ni maono ya kitoto kifikra. Kua
 
Zito nimesoma naye mlimani namjua sana wakati ule tunaendesha siasa za chuo hakika sita msahau kwamaana nimtu ambaye hakuweza kueleweka hata siku moja.Naalitusumbua sana kutokana na siasa zake sisizo eleweka,kwahiyo hii ni tabia yake toka alipokuwa mtoto hayupo tayari kukubari mawazo ya wenzake watu wa silika hii huwa na matatizo na hawafai kuwa viongozi kwasababu husababisha matatizo makubwa sehemu/organization wanazo zingoza.Tunao mfano mzuri wa lyatonga Mrema huyu naye nimtu mwenye silka ya kuamini mawazo yake na mitazamo yake kuwa ni sahihi zaidi kuliko wengine mtu mwingine ni Christopher Mtikila sikuzote mtu huyu ameonekana anajua kila kitu na huamini kuwa yuko sahihi matokeo yake ana potoka na kufikia kutukana matusi.

Kwahiyo zito sio nyoka ila ajulikane kwa misimamo hiyo na apewe uongozi kwa tafsiri ya misimamo yake, vinginevyo atakiangusha chama kama wahusika hawata mjua vizuri na kumpa madaraka ya juu sana zaidi ya hayo aliyo nayo kwasababu watu kama hawa pia si sida kugeuka kuwa vibaraka baada ya kuona kama hawasikilizwi
 
Wakati historia ya taifa hili inaandikwa upya. WAPO WALE AMBAO WATAANDIKWA KAMA MASHUJAA NA WAKOMBOZI WA KWELI. AMA KWA HAKIKA WAPO AMBAO WATAANDIKWA KAMA WASALITI.
 
Zito ni mmoja wa wapinzani wanaoheshimika sana ktk jamii.lkn sasa naanza kumtilia mashaka ana nia gani.
Mi naona kama hayuko comfortable ndani ya chadema ni bora ajitoe mapema.sitaki kuamini kuwa anatumiwa na ccm ila inaonekana ana tamaa sana ya madaraka.anatamani awe kiongozi wa chadema wakati umri wake bado unamruhusu kuvuta subira.
Akiendelea hivi ni bora chadema wamtimue maana atakivuruga chama na kuinufaisha ccm.
 
Zitto mmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhh.😛ray2:
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom