Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
Zitto is wrong, anapaswa apewe adhabu! Je, ambao hawakumpigia kura Kigoma, wanahaki ya kusema 'sisi hatukumpigia kura'? La, hasha. Ukishaamua demokrasia itegemee kura, HESHIMU KURA.

Ndiyo maana mzee mapesa wa UDP aliadhibiwa na Sitta kwa kosa la kutowaunga mkono wapinzanni wenzake. Je, Sitta alifanya kosa? NO! Red must be red, and bluee must be blue...Tanzania ya leo, HUWEZI KUABURUZA WATU, after all, kila mtu ni kama maua tu hapa duniani. Hakuna cha fisadi wala mzalendo, sharti tuonje kaburi.

Zitto kukaa nyumbani (if it is true) bila kuja bungeni, ni sawa. Lakini kutoa siri za vikao vyao ni kosa.

Jeshini huwa watu hawa wanaitwa VIHEREHERE. Nadhani hajapita JKT? Au ndo ile ya miezi 6?

sawa kabisa,kama yeye alikubali kupiga kura basi anapashwa kuheshimu kura maana ndio uamuzi wa mwisho,au zitto anataka kutuambia waliokuwa hawatakikuingia bungeni waliibiwa kura.hahahaha......................., yeye kama nataka kwenda aende maana maandalizi aliisha yaanza long time nadhani sasa nafasi yake ipo inamsubiri.kidemocracia anahaki ya kukubaliana au kuto kukubaliana, na hakua na haja hata ya kupiga kura,angeonyesha msimamo wake na abaki akiamini anachoamini.sasa amepiga kura alaf hakubaliani na kura ambazo ni msimamo wa chama, sioni alichofanya hapo.
 
Mkumbusheni Zitto kuwa masikio hayazidi kichwa.
Thus so.
 
Kila wakati nina wasiwasi sana na siasa za Zitto...ameshafika mahali naona anakua kama mzee wa Kiraracha...ataharibu what CDM stands for,for his personal gain....asingetakiwa kuongea chochote..angekula kimya kuheshimu kura nyingi za wenzake kutoka...hivi vidude vya huyu jamaa vinaboa sana..atakuja kuharibu move,kuna kitu flani anakitafuta huyu jamaa....
 
Kufanywa au kutofanywa wajinga inategemea mtu amnaelewaje na anatafsiri viti taratibu na sheria zinazosimamia eneo husika. Naamini mdogo wangu Zitto ana akili timamu na anafanya jambo bila kukurupuka kama unavyodhani. Demokrasia ni pamoja na kujua jinsi ya kuwa mwana dipromasia pia. Kijana huyu anajua kusoma nyakati...... big up ZITTO!!

shida ya zitto kabwe ni kujiona ana uelewa kuliko vijana wengine wa kitanzania....mbowe aliulizwa na tanzania daima kuwa watahudhuria hotuba ya kikwete bungeni akajibu kuwa watu wasubiri muda utasema....na kweli muda ulipofika tuliona...hakuzungumzia habari za kupiga kura sababu hayo ni mambo ya chama..mbona zitto hakuwaambia waandishi kwamba watapiga kura kabla ya zoezi...au alishtukizwa ghafla akiwa kwenye kikao...?ajaribu kutulia akili yake ipevuke vya kutosha...ndio maana hakuchaguliwa kuwa msemaji wa chama...hawa watu wapo makini na walishagundua tatizo la huyu dogo...
 
1. Kama ulikuwa unanisoma ungeweza kuona kwamba mgawanyiko huu ulikuwa wazi hata kabla ya Zitoo kuusema, Zitto kathibitisha.

2. Zitto talks too much, there is such a thing as "too much information". Anataka kujifanya "A Profile in Courage". Lakini kuna tofauti kati ya courage na narcisissm. Hivi kulikuwa na ulazima gani wa yeye kusema haya? Naona kwa nini Zitto hakupewa uongozi wa upinzani.

Moja ya upuuzi wa kujiunga na chams, na moja inayofanya independent thinkers kupata ugumu kujiunga na chama, ni ukweli kwamba chama kikishaamua, unatakiwa kukubali. Ndiyo maana ya "collective responsibility". Kama swala lina uzito na unatofautiana na chama unaweza hata kujitoa kwenye chama. Watu walijitoa TANU enzi ya kupiga kura iliyoruhusu wazungu na waasia kupiga kura Tanganyika.

Kwa hiyo Zitto naye ilimbidi kwenda na maamuzi ya chama, kama tofauti zitazidi anaweza kuachia ngazi kwenda kwenye chama anachokipenda au kuanzisha chake.

Kaka kula zako Tano!!!!Huyu jamaa nadhani anataka ku-run another CDM ndani ya CDM origional....kana mambo flani hivi ya ki-snitch yanaboa sana...kana uchu wa madaraka sana..na wazee wetu pale watakashughulikia kakome kua na double heads..kawe na msimamo collectively na wenzake ili tuwe na msimamo kama chama....
 
To go public and expose what happened in there meeting is the big mistake
 
Kufanywa au kutofanywa wajinga inategemea mtu amnaelewaje na anatafsiri viti taratibu na sheria zinazosimamia eneo husika. Naamini mdogo wangu Zitto ana akili timamu na anafanya jambo bila kukurupuka kama unavyodhani. Demokrasia ni pamoja na kujua jinsi ya kuwa mwana dipromasia pia. Kijana huyu anajua kusoma nyakati...... big up ZITTO!!


Taratibu. Piga hodi, andika post angalau 5 hivi halafu unaweza kula sahani moja na great thinkers. Zitto amebore beyond repairable limits
 
shida ya zitto kabwe ni kujiona ana uelewa kuliko vijana wengine wa kitanzania....mbowe aliulizwa na tanzania daima kuwa watahudhuria hotuba ya kikwete bungeni akajibu kuwa watu wasubiri muda utasema....na kweli muda ulipofika tuliona...hakuzungumzia habari za kupiga kura sababu hayo ni mambo ya chama..mbona zitto hakuwaambia waandishi kwamba watapiga kura kabla ya zoezi...au alishtukizwa ghafla akiwa kwenye kikao...?ajaribu kutulia akili yake ipevuke vya kutosha...ndio maana hakuchaguliwa kuwa msemaji wa chama...hawa watu wapo makini na walishagundua tatizo la huyu dogo...

Viherehere wapo kila mahali,kuanzia darasa la kwanza hadi chuoni,kila mtu atakubaliana na mimi kuwa kila mahali kuna visebengo,hata kwenye siasa.lazima kuna watu wanaotaka kuonekatana ni tofauti hata kama sio lazima,sasa zito anaona kafikia kileleni,lakini nadhani wataangalia namna ya kwenda nae maana walisha mjua tangu long time
 
Sasa kama Zitto anaonesha jeuri kwa viongozi wake wa chama wanasubiri nini kumpa adhabu stahiki au kumwondoa Uanachama?

Ina maana alipingana na wenzake hadi kupelekea kupiga kura? (Bravo! - ameonesha ujasiri wa kutopelekwa puta).. Je walivyofikia uamuzi wa kupiga kura na yeye alijua kuwa hataungwa mkono kwa nini alishiriki kwenye mchakato halafu baadaye anakwenda kinyume na maamuzi ya hizo kura? Kulikuwa na haja gani ya kupiga kura kama alijua kuwa hakuwa tayari kushirikiana na maamuzi ya walio wengi?

Kama jamaa anaonekana kwenda kinyume na maadili ya Chama kuendelea kumvumilia itasababisha majuto makuu huko mbeleni.. The more you tolerate him, the more he is spoiling others.
 
Eti anasubiri adhabu kumbe anajua alichokifanya ni utovu wa nidhamu, alichofanya Zitto ni kitu cha kipumbavu ni sawa na kujisaidia sebuleni eti kwa vile una uwezo wa kuyazoa watu wakikuzonga.
 
Huyu Zitto anasema eti JK amefanya mambo mengi kigoma hivyo asingeweza kutoka bungeni, hii inamaanisha hata kura aliyopiga Zitto katika uchaguzi alimpa JK na si WPS, hii inatia shaka uadilifu wa Zito kwa cham chake
 
Zitto ni kijana mzuri kwenye siasa lakini kama mnakumbuka mi nilishawahi kutamka humu wazi kua simwamini kabisa.

Ni mtu anayependa maslahi binafsi na mwepesi sana kununuliwa bila kujali maadhara kwa wananchi anaowawakilisha.

Sasa kama mnaweza kukadiria future ya upinzani tanzania ni kwamba kwa sasa atakua ameshapewa mchongo ili aende kwenye chama fulani na atakapoondoka chadema kifuatacho ccm itakuja na habari kwamba chadema si chama cha upinzani ila ni chama cha watu wa mikoa fulani na cha dini fulani. HAPO UTAKUA MWANZO WA USHINDI WA MAFISADI KUDHOOFISHA NGOME YA UPINZANI BUNGENI.

Sasa basi zitto nadhani unatakiwa kujua kwamba we sio maarufu sana au mwenye mafanikio sana ila mafanikio yako ni dhamana tuliyokupa sisi wananchi tulia na kutambua ya kua mtoto hua anatambaa kwanza then ndo anajifunza kutembea so kama unataka madaraka makubwa subiri muda wako utafika na sio kuwachanganya wenzako kwa sasa.
 
Hivi hapa pana siri gani?walipanga watoke nje na wametoka na wengine mkaanzisha chokochoko kwamba wale ambao hawakwenda bungeni na kutoka nje yaani hawakuingia kabisa bungeni ni wasaliti kwa bahati Zitto ni mmojawapo na ndiyo ameenda kujisafisha na kueleza kinagaubaga.mpaka mtakapoacha kila analolifanya Mh.Zitto kuwa ni issue nafikiri naye hataacha kuwashangaza kwani anaelewa gharama ya vijineno vyenu kwa wapiga kura wake.

sasa kama haikuwa Siri wewe ulikuwa inaijua hii?, si umeijua badala ya Zitto kuisema kwenye vyombo vya habari?, hayo yalikuwa ni mambo ya ndani ya Chama, yalikuwa yanawahusu Wabunge wa Chadema tu na ndio walioshiriki hilo zoezi la kupiga kura,
 
Paka akiondoka panya hutawala … na kutapanya. Hili ndio ninaliona hapa Tz. Zamani za chama kimoja na siasa ya ujamaa tulikuwa tuna sauti moja kukemea au kushauri kwa kutumia hekima na watu wote walikubaliana na kuandamana.

Sasa tupo enzi mpya .. enzi ya uhuru na demokrasia. Demokrasia pana ya jinsi hii ni nzuri, lakini inahitaji kusimamiwa na mtu au watu wenye hekima ya kutosha na uzalendo kwa nchi. Bila ya sifa hizo tunaweza kujikuta kwenye ile chaotic experience of the old Babylon, tutasambaratika. Kila mtu na wazo lake, lugha yake, priorities zake na kadhalika… kusambaratika ni lazima.

Mh Zito alitakiwa atumie kanuni ya opportunity cost .. kukubali maamuzi ya wengi dhidi ya hoja binafsi ili kujenga chama chake na kudai haki ya demokrasi Tza. Sasa hivi hatakwepa kufikiriwa negative na watu.. na kuna mashaka mengi dhidi yake. Lakini kwasababu we live in the new era where freedom of speech avails all, atapata watetezi wa hatua yake hiyo… utetezi huo hautasaidia sana nia ya kuimarisha demokrasi na kudai Katiba Mpya.

Mimi sijui shida ya Mh Zito! Hatua ya kutoka nje ilikuwa mkakati wa chama ambao haukuvunja katiba na sheria ya nchi (Wanasheria mbalimbali wameshalitolea ufafanuzi). Sasa kama sheria (ambayo Mh Zito anaifahamu) anaogopa nini kujumuika na maamuzi ya chama chake ku-walk out? Kama anatafuta umaarufu ataupata kutoka maadui wa chama chake… Je ni kwa faida gani sasa!

Niliwahi kusema kuwa Chadema ipo kwenye kipindi kigumu cha kufanya siasa. Ni kipindi kigumu kwasababu kuna mabomu (land mines) ambayo yametegeshewa kulipua Chadema. Yamo ndani ya Chama cha Demokrasi na Maendeleo na pia ndani ya baadhi ya vyama vingine vya upinzani. Nasema hivyo nikikumbuka kuwa nilipata kujulishwa na rafiki ya Zito kuwa, "Mh Zito ni rafiki mkubwa wa rais Kikwete,.." hivyo ni rahisi kwa Dr Kikwete na CCM kumtumia akiwa bado yuko upinzani. Na ndio maana anakimbilia vyeo vyenye sauti kubwa ili apate influence zaidi. Kwa mfano yeye angekuwa KUB asingeongoza msafara wa ku-walk out. Chadema wasingeweza kutoa hiyo pressure kwa rais na NEC... Sikuwahi kuamini jambo hilo, lakini as time goes on ninanza kuona kuna ukweli flani hivi ...

Hata hivyo, mimi naamini kuwa wote tunakubaliana na
(1) Hitaji la Katiba Mpya. Katiba ya sasa inaumiza demokrasi.
(2) Hitaji la NEC huru ili kusimamia uchaguzi ulio huru na wa haki
(3) Matokeo ya uchaguzi wa raisin a wabunge una maswali makubwa na hayajajibiwa
(4) CCM hawataki Katiba Mpya.

Hilo la No.4 sasa ni kuukuu. Prof Ibrahim Lipumba aliwahi kudai na kushinikiza katiba iandikwe upya, haikuwezekana! Wote tunakumbuka yaliyotokea Zanzibar uchaguzi wa mwaka 2000. Sasa tena mwaka huu tumeona NEC ikivuruga demokrasi wazi na ushahidi upo. Je Chadema wafanye kama CUF? Wakubali Mh Zito apewe uwaziri na hivyo iwe ndio maridhiano? Je Chadema waandamane na kusababisha kumwagika damu? Mbinu gani itumike sasa? Mimi naona Chadema wametumia njia ya kistaarabu kabisa kushinikiza hojka yao isikilizwe lakini bila kusababisha vurugu nchini. Tunahitaji kuwaunga mkono na kuwatia moyo.

Wengi wanaokosoa approach hiyo, na badala yake wanapendekeza Chadema waache kupokea mshahara, waache kuingia bungeni moja kwa moja, nk ni hoja ambazo ni za watu wanaofurahishwa na CCM kuwepo madarakani bila kujali uhalali wao. Hii haitasaidia sana. This is a paradoxical concept, na Chadema wanahitaji support, umoja wa chama na umakini mkubwa. All the best Chadema, ila mimi bado ni mwana CCM mfu.
 
Kundi la wabunge wa chadema waliokuwa hawapo bungeni wakati wa hotuba ya rais lilikuwa kubwa kiasi cha kufanya waandishi wa habari waulize masuala

Labda chama kiliridhia wabunge hao wajibu watakavyo kwa kuwa chama hakikutaka kusema moja kwa moja kuwa kundi hilo lilipinga ku walk-out mbele ya rais moja kwa moja.
 
Achaneni na Zittto sisi tunataka tume huru na KATIBA mpya hawa mafisadi wanafika kila mahali na kutufanya tusijadili mambo ya msingi!
 
Tht Zito we knew is no more, ukweli tunaujua. Whatever u do, u will never destroy ChademA! Tumeishakujua give it up Zito coz it will never work! Kama kuna ulichochukua warudishie.
 
Zitto ASANTE KWA MSIMAMO WAKO
NAJUA SIKU ZINAKUJA UTATOA TAMKO LA KUWASHANGAZA WENGI KAMA ULIVYOSEMA SIKU MOJA KUWA UTATOA UHAMZI MUGUMU

ZITTO KARIBU CHAMANI

Na akifika chamani ndio hutamsikia tena. Hilo jina unalisikia kwa sababu yupo CHADEMA, nje ya CHADEMA ni mfu, atazikwa kisiasa. And he knows that very well.
 
HATARI: Nyoka kaingia ndani ya CHADEMA

Tumepata taarifa kuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini kupitia CHADEMA, Zitto Kabwe, akiongea na TBC1 amesema kuwa yeye ni miongoni mwa Wabunge wa CHADEMA waliokuwa wanapinga ile walkout isifanyike Bungeni Alhamisi iliyopita wakati Kikwete anahutubia.

Watu wametoa mawazo mbalimbali kuhusu suala hili. Kuna waliosema ameonesha ukomavu wa kisiasa na demokrasia ndani ya CHADEMA.

Mimi nina mawazo tofauti sana. Kitendo alichofanya Zitto Kabwe ni utovu wa nidhamu wa hali ya juu kwa uongozi wa CHADEMA.

Yeye kama mwanachama wa CHADEMA, Mbunge, Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA na Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni anapaswa kuelewa kuwa maamuzi yote yanayofanywa na chama yanakuwa ndiyo msimamo wa mwisho wa chama. Hapa kuna suala la collective responsibility.

Alichokifanya Zitto kwa kuongea na TBC1 ni sawa na waziri ambaye anatoa siri ya vikao vya Cabinet kwa vyombo vya habari.

Mfano, kwenye cabinet kunatokea mvutano kuhusu suala fulani, let's say uuzwaji wa nyumba za serikali. Mawaziri wanajenga hoja zao halafu serikali inafikia uamuzi wa mwisho kuwa itauza nyumba za serikali kwa vigogo wa serikali.

Then atokee waziri mmoja aseme hadharani kwenye media kuwa yeye alipinga mpango wa kuuza nyumba za serikali kwenye Cabinet lakini akazidiwa kura na mawaziri wengine. Huyo mtu angefukuzwa kazi mara moja.

Ni jambo la kustusha sana kuona kuwa Zitto amekiri hadharani kuwa yeye alipinga jambo hili na kulikuwa na mvutano ndani ya CHADEMA. Kwa matamshi haya, ametoa siri za vikao vya ndani vya chama.

Uamuzi unapofikiwa na chama hata kama wewe binafsi haupendi unakuwa ni wa mwisho na lazima wewe uukubali, uunge mkono na uutekeleze.

Nadhani kama kiongozi wa CHADEMA, Zitto ameonesha utovu wa nidhamu kwa chama, amevunja kiapo cha kutunza siri za chama na ameonesha kukosa maadili.


Tena Zitto alienda mbali zaidi na kusema kuwa yeye aliamua kutokwenda kabisa Bungeni kwa kuwa hajakubaliana na walkout. Hili ni kosa kubwa sana la kupingana na maamuzi halali ya chama.

MASWALI YA KUJIULIZA:

1. What is Zitto Kabwe trying to achieve?

Je, anataka kuonesha umma wa Watanzania kuwa kulikuwa na mgawanyiko kwenye CHADEMA juu ya hili jambo na yeye hakuunga mkono uamuzi huu? Au pengine huenda anataka kuwaonesha vigogo wa CCM kuwa kazi waliyomtuma kuzuia walkout aliifanya kwa bidii na jitihada zote lakini akashindwa.

Kwa ufupi, kitendo cha Zitto si jambo childish tu, bali kinazidi kujenga zile hisia zilizopo mura mrefu kuwa yuko karibu mno na vigogo wa CCM na ni mtu ambaye huwa anatumiwa tumiwa hovyo kulinda maslahi fulani ya watu wachache.

CHADEMA ijihadhari na nyoka huyu hatari.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom