Kitendo cha Naibu Katibu mkuu wa CDM Zitto Kabwe kusema yeye anapinga msimamo wa chama chake wa kutoka nje wakati Rais anajiandaa na hotuba inaonyesha huyu bwana ni mtu asiyefuata maadili na uwajibikaji katika chama ( ethics and code of conducts).
Kumekuwepo na sintofahamu kuhusu msimamo wa Zitto kabwe katika masuala mengi mara anasema hagombei ubunge, mara naenda kinondoni,geita,kahama! hana msimamo!!
Mara hii CDM imekuja na mipango ambayo wengine tunaiona ni mizuri mana hawawezi kwenda mahakamani kupinga matokeo ambayo dhahiri yaliibiwa na hata huyu Zitto anajua hilo.
Kitendo chake alichosema TBC, kwamba ni haki yake ni kweli lakini kama kiongozi wewe ndio unaongoza mapambano, hatutegemei tena uje kuwambia askari wako kwamba adui ana jeshi kubwa ama amejipanga sana tusimshambulie!!
kwa hiyo kauli yako Zitto ingekuwa jeshini wewe unafanya haya huku mkiwa mstari wa mbele askari wako wangekugeuka.
Unatajwa kama rafiki wa Rostam na mafisadi wengineuko nao jirani sana, sasa wewe hufai kuwa kiongozi cdm, mana mtazamo wako na cdm ni tofauti sasa hamia ccm ama tawi la nccr basi ukamalizie siasa zako pale maana kisiasa huo ndio mwisho wako.
Kuwa mstarabu kwa kujiuzulu mana wewe ni mamluki hufai.