Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
inawezekana amefanya hivyo kulinda mahusiano yk binafsi na jk labdaalimpigia akawa hapokei ikabidi atumiemedia kumfafanulia kuwait anamtambua cdm ndiyo inamsukuma vinginevyo
 
Yeye ndiye mwenye mawazo mazuri na ndiye yeye aliyekifanya Chadema kionekane chama cha kisomi zaidi. Namlaumu Slaa, kwa kugombea Urais kwa sababu kaharibu muongozo halisi wa Chadema. Zitto ataleta upinzani zaidi kama atagombea urais 2015.

nimekugongea ka kidole kekundu. angalia
 
Mbona sielewi? Hivi kuna mtu aliyewahi kusema hapa kwamba zitto ni ccm? Eti ni kweli ztto aliwahi kutaka kuwa Mkiti wa chadema? Eti aliwahi kutaka kuwa KUB?
 
kwa siasa za Zitto sidhani kama chama kinaweza kufanikiwa katika adhima yake ya kufikia malengo ya katiba mpya na tume mpya si vizuri kuwa-let down wenzio

sina imani sana na zitto,naona msimamo wake unalega now days
 
Zitto ASANTE KWA MSIMAMO WAKO
NAJUA SIKU ZINAKUJA UTATOA TAMKO LA KUWASHANGAZA WENGI KAMA ULIVYOSEMA SIKU MOJA KUWA UTATOA UHAMZI MUGUMU

ZITTO KARIBU CHAMANI
 
Jamani hili ni moja tu mnashtuka saa hizi, ZITTO NI KIBARAKA WA CCM. Mwenye masikio na asikie. Ni mtu hatari sana kwa CHADEMA.
 
kwa hili Zitto umewapa maksi CCM na wanakugongea senksi kwa upumbavu ulioufanya na wenzio. Shame on you!!
 
jamani Zitto ni jasiri kwani wale wote ambao hawakuingia Ukumbini (gazeti la Mwananchi Ijumaa 18 Nov. 2010) walikaa kimya kwa hofu na wote ni wasomi na maprofessor kwani wamejua ni nini kitatokea iwapo Bunge lijalo itakuwepo hoja ya adhabu kwa wote waliotoka (tusuburi) na bila kumsikiliza humo Bungeni itakuwa ni vituko kwani wataijadilije Hotuba ya Rais? au kuchukua posho na mshangingi?

Mkumbuke Wabunge wanapitisha Bills (waraka) Rais anasaini (Act) Sheria Siasa si Ugomvi wa Simba na Yanga au Tambaza na Azania (sijui km walishamaliza miaka ya 70s)

Heri kuwa kondoo katika msafara wa wanyama wote ukae nyuma kuliko kuwa mbweha (kiherehere\chambo) kutangulia mbele usikokujua uendako
 
Go go go zitto, chadema wasije kukuponza bwana zako mafisadi wakutose. Linda maslahi yako baba achana na wanaopoteza muda wao wakitetea maslahi ya taifa. Wewe ni mbunge kijana machachari bana
 
Zitto ASANTE KWA MSIMAMO WAKO
NAJUA SIKU ZINAKUJA UTATOA TAMKO LA KUWASHANGAZA WENGI KAMA ULIVYOSEMA SIKU MOJA KUWA UTATOA UHAMZI MUGUMU

ZITTO KARIBU CHAMANI
Unamkaribisha kwa mara nyingine? We know he's already there. Pia aliwahi kusema yeye si mali ya CHADEMA. Poleni wananchi anao wawakilisha
E
 
Jamani hili ni moja tu mnashtuka saa hizi, ZITTO NI KIBARAKA WA CCM. Mwenye masikio na asikie. Ni mtu hatari sana kwa CHADEMA.
 
Dogo asituzingue anataka kuwa KIHEREHERE sana km amechoka atimuke walikuja na wakaondoka kwani yy nani? Mwenendo alionao sasa unmpeleka pabaya km hakukaa chini na kufikiria cha kusema kbla hajaulizwa. Umaarufu wake naona unazidi kushuka kila siku na ataishia km kina TUNTEMEKE SANGA .
kama Walid Kaburu!! Muha ni muha tu, hata akisoma anabakia tu kuwa kalumanzira!!!!

wumvishije Mutani?
 
Kuanza kutofautiana mapema ni dalili mbaya sana kwa chama makini kama CHADEMA, ambacho kimeaminiwa na wananchi kwa imani kubwa sana. Ukichukulia hali ya kutokuwa na msemaji mkuu wa chama, kama Zitto anaweza akaenda kwenye media na kuongelea mambo ya ndani ya Chama ni hatari sana kwa chama kilicho makini. Chama cha CHADEMA niliamini ni chama makini kisicho hata na doa ya kukosa uadilifu na kuaminiana.

Kauli ya zitto kwa media kuongelea mambo ya chama kwamba waligawanyika katika msimamo wa kutoka nje wakati rais anaongea lina faida kwa nani? Na kusudi lake ni nini? Kwani nini maana ya demokrasia pale kura zinapoamu?, Je kuna haja ya kugoma kufuata maamuzio ya kura? Je Hio ni demokrasia gani? Hakuna tofauti ya kupinga demokrasia huku ukiubili Demokrasia.

Hapa CHADEMA wanajikoroga tena sana tu. Hakuna haja ya kuwa Mwanachama wa chama kisicho kuwa makini kama CHADEMA. Nimekuwa mwanachama wa muda mrefu wa Chadema, Nimeihubiri CHADEMA lakini kwa haya ya akina zitto ni bora kujiweka pembeni.

Hapa tusifanye tunatetea kwa maoni ya kutifautiana kwa mtazamo na kimawazo. Hapa ukweli watu tunaujua kuwa Umakini ndani ya CHADEMA umepotea, Kwa mitazamo hii Tutarajie kusambaratika kwa CHADEMA.

Mimi binafsi naomba kujiondoa Kabisa kuwa mwanachama hai wa CHADEMA mpaka hapo tutakapo kuwa tumekomaa kisiasa. Nahisi kwa vijana makini kujiunga na CHADEMA ni uamuzi wa kurisk mno, kwani uchanga wa chama na kuwa na watu waoga kama Zitto, Mtu ambaye hawezi kuheshimu demokrasia ndani ya chama ni hatari isiyovumilika na watu makini. Hivyo mimi kama mtu makini nahisi kabisa nilikosea kujiunga na CHADEMA ni heri kuwa mtu asiye na CHAMA kiliko kuwa mwanachama wa CHAMA chochote kwa Tanzania yetu hii.

Kwa hili CHADEMA wapoteza tumaini langu kwao.
 
Zitto arudi ccm..its time for him to go...mpuuzi huyu kijana
 
Yeye ndiye mwenye mawazo mazuri na ndiye yeye aliyekifanya Chadema kionekane chama cha kisomi zaidi. Namlaumu Slaa, kwa kugombea Urais kwa sababu kaharibu muongozo halisi wa Chadema. Zitto ataleta upinzani zaidi kama atagombea urais 2015.

Kama atagombea kupitia CCM!!!! ila nina wasiwasi kama anaweze kudumu huko CCM maana hawajui kumvumilia mtu yeyote, wenyewe wanajua kumlamba tu miguu mwenyekiti wao!!!
 
Zitto Kabwe ameeleza kuwa ni kweli walipiga kura na kukubaliana watoke wakati Rais akizungumza, lakini wao walipinga na ndiyo maana aliamua bora asiingie ndani ya Bunge, amesema kuwa yeye kama Zitto na wenzake aliona ni bora kutoingia kuliko kuingia na kutoka wakati Rais ambaye ndiye alama ya Bunge na Amiri jeshi mkuu akiongeaa.

Kwa vile kutoka ulikuwa msimamo wa chama, basi yeye na wenzake wamekosea na hilo ni swala la Chama kwani wanaweza kuadhibiwa na chama kwa vile kura za kukubaliana kutoka ilishinda.

Zitto alisema kuwa wanasubiria hatma yake katika chama na kusema kuwa hiyo ndiyo gharama ya Demokrasia. Ila amekanusha kuwa jambo hilo lisifikiliwe ni mgawanyiko bali mtazamo tofauti wa mawazo.

Source: TBC 1 News Bulletin

- Well, wakuu haya ndio tulisema mapema kwamba Chadema wametafuta unwanted political National attention ambayo ndio njia rahisi sana kutumika kwa siasa zetu Africa kwenye kuwajibu, bila kujali tatizo la kweli huu sasa ni mwanzo tu. I mean CCM kuna ambayo hawakubaliani lakini sio kwenye mazito kama haya, huwa wote wanakubaliana halafu sometimes wengine wanakuja kutudanganya huku public, kumbe wote ni wamoja tu!

- Chadema mnahitaji kuamka kwamba this is not very good, hasa inapotoka kwa kiongozi wenu wa pili wa upinzani, bungeni!


William.
 
Mtazamo tu: Mhe Zitto ungenyamaza kimya otherwise unajimaliza wenyewe wala usijetafuta mchawi.

Tujadili
 
Hakuna mgombea binafsi kwa sasa bungeni-ule ni msimamo wa chadema kwa maslahi ya taifa sio ya mtu mmoja, tunaunga mkono hatua ya wabunge wa chadema na tunasubiria mambo mengi zaidi very united, keep figting guys hawa mafisadi cant put new nec and consitution without pressure of this nature.

Kama wabunge wachache wana msimamo wao lakini nilifurahi hawakingia kutii msimamo wa maamuzi ya chama. Zitto should back up the decision to achieve the target -akumbuke alipigwa bomu kigoma mjini akatuambia ni hao hao so please bro zitto stand as usual for CHADEMA
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom