Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
Zitto Kabwe ameeleza kuwa ni kweli walipiga kura na kukubaliana watoke wakati Rais akizungumza, lakini wao walipinga na ndiyo maana aliamua bora asiingie ndani ya Bunge, mesema kuwa yeye kama Zitto na wenzake aliona ni bora kutoingia kuliko kuingia na kutoka wakati Rais ambaye ndiye alama ya Bunge na Amiri jeshi mkuu akiongeaa.

Kwa vile kutoka ulikuwa msimamo wa chama, basi yeye na wenzake wamekosea na hilo ni swala la Chama kwani wanaweza kuadhibiwa na chama kwa vile kura za kukubaliana kutoka ilishinda.

Zitto alisema kuwa wanasubiria hatma yake katika chama na kusema kuwa hiyo ndiyo gharama ya Demokrasia. Ila amekanusha kuwa jambo hilo lisifikiliwe ni mgawanyiko bali mtazamo tofauti wa mawazo.

Source: TBC 1 News Bulletin

Huyu Mh huwa simuelewi at times, hii information ni ya kubomoa chama na sioni mantiki ya yeye kuisema hadharani. Zitto ni liability kubwa kwa Chadema. At times simuelewagi maamuzi yake anayatoaga wapi na anashauriwa na nani.
 
inasikitisha sana hasa kwa mtu tuliyemwamini alafu anafanya vitu vya ajabu, Mbowe ,Mnyika ,Slaa kazeni Buti
 
Kuna wakati nilikuwa nashirikiana na vijana fulani wa Kigoma katika kutatua tatizo lao, sasa mambo yalikuwa kama haya tunakubaliana hivi wao wanakwenda kinyume na makubaliano. Mtu mmoja akanishauri ya kwamba watu wa Kigoma wana kawaida ya kuwa kigeugeu hivyo niachane na shauri lao, sijui kuna ukweli juu ya hili? Maana tabia wakati mwingine zinaweza kutegemeana na asili yetu (mother land).

Wewe ni mkabila, mtu wa hovyo kabisa. Na inaelekea wewe ni shabiki wa CHADEMA inayolea watu wanaopenda kujudge watu na vitu kwa ukabila. Wewe unatakiwa ulaaniwe kabisa katika nchi yetu inayokua.. Zitto ana akili nyingi CHADEMA nzima na kwa vile sio mchaga basi mnamuita bwana mdogo, He's better than Slaa mna muita DR japo hajawahi kupractice accademics. Hovyo na ukabila wako, ingekua inaruhusiwa ningekurushia tusi zito hadi ukaenda kuoga
 
Nadhani Zitto aanchojaribu ni kuwafundisha nyie mashabiki wa CHADEMA kwamba msiwe watumwa wa mawazo, mitazamo na miongozo ya wachache. Kwa nini awe mtumwa wa mawazo ya Mbowe na Dr Slaa wakati yeye msomi na mwenye exposure ya siasa ya kimataifa.. Nyie lazima mkubwali kile kitendo kilikua cha kitoto na kilidhihirisha kutokua nna malengo ya muda mrefu ya chama.

Hilo jina unalotumia haliendani na wewe kabisa,
Hebu elewa hivi
Watu hawamlaumu Zitto kupingana na wenzie, hiyo ni demokrasia na ndio maana Chadema waliitisha kura
WATU WANAMLAUMU ZITTO KUKIMBILIA KWENYE VYOMBO VYA HABARI NA KUROPOKA SIRI ZA CHAMA, KWANI ZITTO ALIKUWA PEKEYAKE ALIYEPINGA?, MBONA WENGINE HAWAKWENDA KWENYE VYOMBO VYA HABARI? YEYE NI NANI? NI MSEMAJI WA CHAMA?
 
inauma eee?? Toka mwanzo nilishasema. Kigoma wanatoaga vifaa. Kgm hatuchagui chama bali mtu. Ndio maana kgm ina karibu vyama vyote kasoro cafu.zito ni kichwa. Very brilliant. Ni mtanzania. Ni mzalendo. Hekima na busara na utaifa kwanza. Sio kususa tu. Yatawatokea puani wale wanaoshabiokia bila kufikiri. Sasa habari hii inawauma. Wanajuta aliyeileta jamvini. Lakini si ndio ukweli?? Kwani zito sio kiongozi wa upinzani bungeni? Kwa nini achicheme yaliyo moyoni mwake???

i fully support him 100%.

besides chadema bila dr. Mfuko wa cement 5000/= inaweeekana!

Punguza ushabiki; hapa JF watu wanafikiri zaidi kabla ya kuandika badala ya kuleta ushabiki tu wa kijinga. yaelekea huyajui hayo maana umejiunga JF juzi tu na kuingia kichwa kichwa.
 
Pia nimemsikia Zitto akihojiwa na Tbc akikubaliana na hotuba ya Kikwete ya kuwa kwenye uchaguzi kulikuwa na udini.
 
Zitto is hypocrite,coward,an imposter and of course he is just one of those guys...piece of shit!
 
Hilo jina unalotumia haliendani na wewe kabisa,
Hebu elewa hivi
Watu hawamlaumu Zitto kupingana na wenzie, hiyo ni demokrasia na ndio maana Chadema waliitisha kura
WATU WANAMLAUMU ZITTO KUKIMBILIA KWENYE VYOMBO VYA HABARI NA KUROPOKA SIRI ZA CHAMA, KWANI ZITTO ALIKUWA PEKEYAKE ALIYEPINGA?, MBONA WENGINE HAWAKWENDA KWENYE VYOMBO VYA HABARI? YEYE NI NANI? NI MSEMAJI WA CHAMA?

Jina langu linaendana na mitazamo endelevu kabisa, sio ushabiki wa kitumwa kama wewe.

Yes zitto anastahili kutoa tamko lake kwa sababu yeye ni Naibu katibu mkuu, Naibu mkuu wa kambi ya upinzani bungeni, ni mbunge anayewakilisha wananchi wa jimbo lake. Kwa nini mnataka kumfanya mtumwa as if amechaguliwa na Dr Slaa na Mbowe.. Nyie wenyewe mnasisitiza haki sawa na uwazi,, halafu zitto anapofuata haki na democrasia anaonekana mkorofi.. kwa mtu mstaarabu na uliye elimika katika siasa ya dunia ya leo, lazima utakubali walichofanya ni kitu cha kitoto sana kufanywa na chama cha pili kwa ukubwa, rubish
 
Zitto ni very smart ndani ya Chadema. Huyu jamaa ndiye aliyetakiwa agombee Urais kupitia Chadema.
 
Zito umechelewa sana kwenda zzm ,usikumbuke shuka wakati kumekucha,wameshatafuna kila kitu.
 
Ina maana Zitto anamtambua JMK kama rais "halali" wa JMT?
naomba kuelimishwa hapa.
 
Hilo jina unalotumia haliendani na wewe kabisa,
Hebu elewa hivi
Watu hawamlaumu Zitto kupingana na wenzie, hiyo ni demokrasia na ndio maana Chadema waliitisha kura
WATU WANAMLAUMU ZITTO KUKIMBILIA KWENYE VYOMBO VYA HABARI NA KUROPOKA SIRI ZA CHAMA, KWANI ZITTO ALIKUWA PEKEYAKE ALIYEPINGA?, MBONA WENGINE HAWAKWENDA KWENYE VYOMBO VYA HABARI? YEYE NI NANI? NI MSEMAJI WA CHAMA?

Yeye ndiye mwenye mawazo mazuri na ndiye yeye aliyekifanya Chadema kionekane chama cha kisomi zaidi. Namlaumu Slaa, kwa kugombea Urais kwa sababu kaharibu muongozo halisi wa Chadema. Zitto ataleta upinzani zaidi kama atagombea urais 2015.
 
zitto ni mnafiki na msaliti.siku moja ndo mtaliona hili ingawa mmeng'ang'ania kuwa ni demokrasia!
 
Pia nimemsikia Zitto akihojiwa na Tbc akikubaliana na hotuba ya Kikwete ya kuwa kwenye uchaguzi kulikuwa na udini.
Kwani hili halikuwa wazi? Wangapi walisikika wakipiga kampeni kwa visingizio vya elimu ya kiraia?
 
Ina maana Zitto anamtambua JMK kama rais "halali" wa JMT?
naomba kuelimishwa hapa.
Sio Zitto tu hata Dr Slaa alikiri hilo kwenye clip. Haka kamchezo walikoanza CHADEMA bila kujipanga kanawaharibia saana na huenda kakaharibu zaidi.
 
Zito anajulikana kuwa ni mtu amabaye anapenda sifa na kujikomba kwa CCM na mafisadi nani hasiyekumbuka alivyo shabkia ununuai wa mitambo mibovu ya umeme toka kwa mafisadi? Si angeamua tu kwenda CCM thats where he belongs.
 
Du!
Ustaadhi, Inaonekana unajua kuliko wanachadema wenyewe!

Ktk safari zake za nje, niliwahi kuonana naye akielezea kuhusu uchumi, demokrasia, nk. Aliweza kujibu vizuri sana kuliko viongozi wengi wa CCM, na Chadema. Alikuwa na nafasi nzuri sana ya kuchuana na JK. Kama Chadema inataka kiwe chama cha upinzani, inatakiwa iwe na watu wasomi kama Zitto.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom