Ndio hapo sasa tunarudi kwenye uhalisia wa swala zima la imani. Mimi nafikiri kuna tatizo kubwa sana kwenye uumbaji, au la basi kuna tatizo kwenye maandiko!
Haiingii akilini kwamba eti Malaika walioumbwa na Mungu, wakaishi nae mbinguni, eti wanaweza kufika mahali wakamgeuka na kuanza kupigana nae vita!!! Ina maana malaika wenyewe hawakua wanamuamini Mungu, walikua wanamuona anazingua maana otherwise kwanini waingie msituni kama kila kitu kilikua poa?
Adam na Hawa, wameongea na Mungu ana kwa ana kama mimi na wewe tunavyoongea hapa, wanapiga stori, wanacheka fresh, ila mwisho nao wakaona huyu anazingua wakamgeuka!!
Akina Musa, mfalme Daudi, Sulemani nk mpaka hao wa agano jipya kina Petro, Yuda, Tomaso na wengine wengi hatukutegemea kabisa wawe na chembe ya mashaka kwani wao waliona "first hand" kila kitu Mungu alichofanya!
Sasa kama hao walishindwa kuwa na imani, hivi sisi huku madongokuinama tunawezaje kujidai kua na imani?? Hiyo imani tunaitolea wapi kwa mfano? Huku wengi tunazuga tuu hamna cha imani wala nini.