Zile shuhuda kwenye maombezi ya Manabii

Zile shuhuda kwenye maombezi ya Manabii

Mkuu kusema ukweli we mwenyewe unaweza kuona jinsi ilivyo vigumu kwa mwanadamu kuamini haya mambo. We fikiria Simon Petro mwenyewe aliishi na Yesu mda wote, aliona miujiza yote, lakini alimkana mara 3, achilia mbali kushindwa kutembea juu ya maji! Yuda Iskariote nae pamoja na kuishi na Bwana Yesu wakila na kupakua miaka nenda rudi, lakini bado alimsaliti! Tomaso aligoma katakata kwamba Yesu kafufuka, mpaka alipomuona kwa macho.

Hivi mimi ambae nakuja kusoma hadithi leo hii kwenye vitabu ni nani...??
"Yesu akamwambia, Wewe, kwa kuwa umeniona, umesadiki; wa heri wale wasioona, wakasadiki."
Yohana 20:29.
 
Unajua kuna uwongo mwingi sana kwenye haya masuala ya kiimani nowdays. Watu wanacheza na psychology yako, wakijua unataka pesa/utajiri na kuponywa certain disease. Kuna mwengine naskia Yuko pale maeneo ya lufungila anaitwa nabii Mussa. Huyo mafuta yake ya upako yanauzwa Tshs. 15,000/= . Siwezi kuwasemea vibaya watumishi wa bwana Ila kiukweli akili yako changanya na za kuambiwa. Siku hizi watu hatupendi injili ya kuhusu ufalme wa Mungu tunataka kupokea miujiza ya vitu vizuri vizuri tu.
We hupendi vizuri mkuu? Au unaishi kwenye nyumba ya makuti na taa za vibatari?!
 
Me kuna kipindi nilienda kwa Peter Nyaga Nabii na Dr
Wakati tupo mle ndani ghafla akaja jamaa akakaa upande wetu wakati huo msaidizi wa Dr Peter Nyaga anaendelea na mahubiri ghafla yule jamaa akaanguka chini nakuanza kugalagala kisha wakampeleka mbele, hazikupita dk2 yule jamaa akazindukika na akawa yuko fresh na kuonyesha alijipangwa alivaa nguo za kawaida
Yaani kwenye shuhuda kuna usanii wa kutisha, mimi sitakagi hata kuzisikia
 
Wanawake wanashikiwa sana akili hadi kuvuruga mahusiano na waume zao na kuvuruga mipango ya familia, maana mwanamke akiifuma laki mbili kwenye wallet hesabu ya kwanza ni kupeleka sadaka kwa mchungaji au nabii....
Na wanawateka sana akili,
 
Na ni kwanini watu wote ambao huombewa na kupona ni wale wenye magonjwa yasiyoonekana / yasiyo na ushahidi dhahiri (mfano kuumwa kichwa, tumbo, matatizo ya akili nk.)

Sijawahi kuona mtu aliekatika mguu/mkono akapelekwa kwenye maombi kuombewa na mguu ukarudi! Kama Yesu alivyorudisha sikio la yule jamaa.
Ndo trick zenyewe, utasikia nimeteseja na uvimbe tumboni miaka 10 anajua ili kuona huo uvimbe lazima utumir mitambo.

Licha ya hivyo, wanao toa hizo shuhuda ni wageni machoni mwa wengi
 
Ni Bora nisikie mke wangu amefanya hivi , kuliko kuchukua pesa hizi akapeleka kwa mganga wa kienyeji..
Kwenda kununua Chumvi ya Upako kuna tofauti gani na Uganga wa kienyeji?
 
Unajua kuna uwongo mwingi sana kwenye haya masuala ya kiimani nowdays. Watu wanacheza na psychology yako, wakijua unataka pesa/utajiri na kuponywa certain disease. Kuna mwengine naskia Yuko pale maeneo ya lufungila anaitwa nabii Mussa. Huyo mafuta yake ya upako yanauzwa Tshs. 15,000/= . Siwezi kuwasemea vibaya watumishi wa bwana Ila kiukweli akili yako changanya na za kuambiwa. Siku hizi watu hatupendi injili ya kuhusu ufalme wa Mungu tunataka kupokea miujiza ya vitu vizuri vizuri tu.
Napenda Sana kuwafatilia watumishi kujua yupi sahihi na yupi janja janja nyingi, huyu Musa alooh ana kelele nyingi kuliko kusikiliza ibada na neno lenyewe, kwenye ushuhuda sasa muumini anapiga kelele sana na yeye kelele Kama wanagombana.
 
Haya mambo ni magumu sana mkuu. Mimi nna ndugu yangu tangu mwaka 1995 ame paralyze miguu. Hakuna maombi ambayo hajapelekwa, mafanikio hakuna na always kisingizio kimekua "hana imani"! Hivi mtu mwenye imani anatakiwa aweje?
Wale wanao ombewa wakapona huwa ni maigizo si kwamba ni Vilema wala viwete, njia wanayo tumua ni kwamba kama Mahubili yako Arusha basi watu wa kufanya hayo maogizo watatolewa hata Shinyanga,
 
Me kuna kipindi nilienda kwa Peter Nyaga Nabii na Dr
Wakati tupo mle ndani ghafla akaja jamaa akakaa upande wetu wakati huo msaidizi wa Dr Peter Nyaga anaendelea na mahubiri ghafla yule jamaa akaanguka chini nakuanza kugalagala kisha wakampeleka mbele, hazikupita dk2 yule jamaa akazindukika na akawa yuko fresh na kuonyesha alijipangwa alivaa nguo za kawaida
Nyaga namfaham kitambo tangu 2010 kanisa lake alianzia baa ya MTAANI kwetu.
 
Mtu hataki kuachana na michepuko wala kuacha madhambi yake mengine lakini anategemea miujiza kisa tu eti kaenda kwa Mwamposa. Kwa kweli hata mimi naunga mkono kabisa: Acha wapigwe tu kwa sababu hakuna namna...
Na huwezi sikia Akihubilia watu waache Dhambi na wajiandae na siku za mwisho
 
Kwa siku moja mtume na nabii mwamposa. Anaingiza Zaid ya watu elf 15 kwa siku ibada iko mbili pale ..najuulizaga hv kweli watu wote hao hawashtuki kuwa wanatapeliwa ...na kila siku watu utoa ushuhuda pale kwake ..nashindwa kuelewa na kuamini kuwa mtu huyu Kuna kitu nyum ya Kaz zake hiz za ibada mnk watu wanajah haswaa haswa .....

Huwenda. Ikawa Ni mpakwa mafuta kweli
Ni ngumu Sana kumshuhudia uongo ..
Kuna madawa pia ya kupumbaza mkuu, ndo maana wale waumini huwa wanawatetea sana hata wakisikia Nabii kafumabiwa watamtetea kwa nguvu zote
 
Mkuu kusema ukweli we mwenyewe unaweza kuona jinsi ilivyo vigumu kwa mwanadamu kuamini haya mambo. We fikiria Simon Petro mwenyewe aliishi na Yesu mda wote, aliona miujiza yote, lakini alimkana mara 3, achilia mbali kushindwa kutembea juu ya maji! Yuda Iskariote nae pamoja na kuishi na Bwana Yesu wakila na kupakua miaka nenda rudi, lakini bado alimsaliti! Tomaso aligoma katakata kwamba Yesu kafufuka, mpaka alipomuona kwa macho.

Hivi mimi ambae nakuja kusoma hadithi leo hii kwenye vitabu ni nani...??
Mkuu mambo ya Imani ni magumu Sana , hata hvyo Mungu ni mmoja na Imani ni moja kwanini kuwepo na Imani nyingi nyingi , vikanisa vingi vingi, huyu anajiita mtume , huyu nabii , huyu mchungaji , na totally wapo against each other tena hawapatani .....hata hvyo wanafanana kitu kimoja wote mahubiri Yao ni toa ubarikiwe na Bwana 🤣 ..... Mi Biblia inanitosha kabisa
 
Back
Top Bottom