Zile shuhuda kwenye maombezi ya Manabii

Zile shuhuda kwenye maombezi ya Manabii

MURUSI

JF-Expert Member
Joined
Jun 25, 2013
Posts
4,574
Reaction score
8,907
Katika vitu nilivyo shindwa kuviamini ni zile shuhuda zinazo tolewa, Ukikaa ukasoma between the line zile shuhuda kama kuna za kweli basi ni moja kati ya 1000 zinazo bakia ni za ku frame kuvutia watu.

Na cha kushangaza watoa Shuhuda wengi huwa ni wageni maachoni mwa waumini. Unakuta ni Sura ngeni au mpya.

Na huu Usanii anaufanya sana anaye jiita Mwaponsa yule Jamaa ni Master wa ku frame shuhuda
 
Unajua kuna uwongo mwingi sana kwenye haya masuala ya kiimani nowdays. Watu wanacheza na psychology yako, wakijua unataka pesa/utajiri na kuponywa certain disease. Kuna mwengine naskia Yuko pale maeneo ya lufungila anaitwa nabii Mussa.

Huyo mafuta yake ya upako yanauzwa Tshs. 15,000/= . Siwezi kuwasemea vibaya watumishi wa bwana Ila kiukweli akili yako changanya na za kuambiwa.

Siku hizi watu hatupendi injili ya kuhusu ufalme wa Mungu tunataka kupokea miujiza ya vitu vizuri vizuri tu.
 
Tatizo ni waliotutangulia wamefeli sana kutetea jamii isiangamie na mambo ya jamii mengi kupelekwa kwenye dini na kuyaondoa kwenye huduma za jamii Kama usitawi wa jamii na taasisi za jamii na kuyapeleka kwenye dini kitu kinachozipa nguvu huduma Kama hizo kuwepo na watu kukimbilia huko wakiwa wanahitaji msaada, kuna huduma zikirudi Serikalini na viongozi wa kidini wale ambao hawakuitwa na huduma ya Mungu watajitoa wenyewe na ujinga mwingi utaondoka, imagine kuwe na madirisha ya kusaidia wasiojiweza hospitalini na watu wawekeze huko kutoa Kama huduma ya damu ilivyo na mengine yakiwa serikalini hayo mambo ya kuigiza yatapotea.
 
Me kuna kipindi nilienda kwa Peter Nyaga Nabii na Dr
Wakati tupo mle ndani ghafla akaja jamaa akakaa upande wetu wakati huo msaidizi wa Dr Peter Nyaga anaendelea na mahubiri ghafla yule jamaa akaanguka chini nakuanza kugalagala kisha wakampeleka mbele, hazikupita dk2 yule jamaa akazindukika na akawa yuko fresh na kuonyesha alijipangwa alivaa nguo za kawaida
 
Wanawake wanashikiwa sana akili hadi kuvuruga mahusiano na waume zao na kuvuruga mipango ya familia, maana mwanamke akiifuma laki mbili kwenye wallet hesabu ya kwanza ni kupeleka sadaka kwa mchungaji au nabii....
 
Katika vitu nilivyo shindwa kuviamini ni zile shuhuda zinazo tolewa, Ukikaa ukasoma between the line zile shuhuda kama kuna za kweli basi ni moja kati ya 1000 zinazo bakia ni za ku frame ku attract watu.

Na cha kushangaza watoa Shuhuda wengi huwa ni wageni maachoni mwa waumini. Unakuta ni Sura ngeni au mpya.

Na huu Usanii anaufanya sana anaye jiita Mwaponsa yule Jamaa ni Master wa ku frame shuhuda
Mambo ya rohoni waachie watu wa rohoni, ukitumia utashi wako utaishia kutenda dhambi kwa kuhukumu bila kuwa na ushahidi
 
Na ni kwanini watu wote ambao huombewa na kupona ni wale wenye magonjwa yasiyoonekana / yasiyo na ushahidi dhahiri (mfano kuumwa kichwa, tumbo, matatizo ya akili nk.)

Sijawahi kuona mtu aliekatika mguu/mkono akapelekwa kwenye maombi kuombewa na mguu ukarudi! Kama Yesu alivyorudisha sikio la yule jamaa.
 
Sasa watakula wapi zaidi ya kufanya huo utapeli.? Kila mtu ashike akili zake mwenyewe.

Anaweza kwenda kilema ili apate uponyaji lakini ataambiwa hana imani wakati kuna (kilema) mwingine alipona hapo hapo.
Ushaongelea neno imani basi hayo mengine yaache
 
Na ni kwanini watu wote ambao huombewa na kupona ni wale wenye magonjwa yasiyoonekana / yasiyo na ushahidi dhahiri (mfano kuumwa kichwa, tumbo, matatizo ya akili nk.)

Sijawahi kuona mtu aliekatika mguu/mkono akapelekwa kwenye maombi kuombewa na mguu ukarudi! Kama Yesu alivyorudisha sikio la yule jamaa.
Mtu akirudishiwa mguu/kiungo cha mwili wake kilichopotea,.je,utasadiki kuwa ni YESU mnazareth ametenda..?? Au ndo mtaanza tena hapa oooh ulozi na uchawi..!?
 
Wanawake wanashikiwa sana akili hadi kuvuruga mahusiano na waume zao na kuvuruga mipango ya familia, maana mwanamke akiifuma laki mbili kwenye wallet hesabu ya kwanza ni kupeleka sadaka kwa mchungaji au nabii....
Ni Bora nisikie mke wangu amefanya hivi , kuliko kuchukua pesa hizi akapeleka kwa mganga wa kienyeji..
 
Wanawake wanashikiwa sana akili hadi kuvuruga mahusiano na waume zao na kuvuruga mipango ya familia, maana mwanamke akiifuma laki mbili kwenye wallet hesabu ya kwanza ni kupeleka sadaka kwa mchungaji au nabii....

Wanasema kwamba mtu pekee ambaye anaweza kuitafuna pesa ya mwanamke kirahisi ni:-

1. Mganga wa Kienyeji.
2. Mchungaji/Nabii.

Cc: Yericko Nyerere
 
Mtu akirudishiwa mguu/kiungo cha mwili wake kilichopotea,.je,utasadiki kuwa ni YESU mnazareth ametenda..?? Au ndo mtaanza tena hapa oooh ulozi na uchawi..!?

Mkuu kusema ukweli we mwenyewe unaweza kuona jinsi ilivyo vigumu kwa mwanadamu kuamini haya mambo. We fikiria Simon Petro mwenyewe aliishi na Yesu mda wote, aliona miujiza yote, lakini alimkana mara 3, achilia mbali kushindwa kutembea juu ya maji! Yuda Iskariote nae pamoja na kuishi na Bwana Yesu wakila na kupakua miaka nenda rudi, lakini bado alimsaliti! Tomaso aligoma katakata kwamba Yesu kafufuka, mpaka alipomuona kwa macho.

Hivi mimi ambae nakuja kusoma hadithi leo hii kwenye vitabu ni nani...??
 
Back
Top Bottom